KITUO CHA POLISI CHASHAMBULIWA AFRIKA KUSINI, POLISI WAUAWA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:43 AM
Watu waliokuwa na silaha wameshambulia kituo
cha polisi katika mji mdogo wa Nqcobo nchini Aftrika Kusini na kuua
polisi wasiopungua 5 na mwanajeshi mmoja.
Polisi ya Afrika Kusini imetangaza kuwa, askari polisi na
mwanajeshi huyo wameuawa leo wakati waliposhambuliwa na kundi la watu
waliokuwa na silaha katika kituo hicho cha polisi.
Msemaji wa Polisi ya Afrika Kusini, Brigedia Vishnu Naidoo amesema
kuwa shambulizi hilo limefanyika mapema leo katika mji wa Nqcobo ulioko
umbali wa yapata kilomita 800 kutoka Johannesburg.
Ameongeza kuwa watu hao wanaoshukuliwa kuwa ni majambazi walifyatua risasi ovyo na kuiba silaha na gari moja la polisi.
Waziri wa Polisi wa Afrika Kusini, Fikile Mbalula amelitaja shambulizi hilo kuwa ni janga la kitaifa.
Afrika Kusini inahesabiwa kuwa miongoni mwa nchi zenye viwango vya juu zaidi vya uhalifu duniani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: