Latest Articles

BENKI YA CRDB YAKABIDHI MADARASA YA SEKONDARI KILOLO

 
Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.












read more

AGENDA YA KUTOKOMEZA MALARIA IWE YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYA MAAMUZI

 Na WAF, TABORA


Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameziasa Kamati za Ulinzi na Usalama nchini kuona umuhimu wakuifanya ajenda yakutokomeza Malaria iwe yakudumu kwenye vikao vya maamuzi.

Dkt. Mollel ameyasema hayo leo, Aprili 25, 2024 akiwa amemwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwenye kilele cha Siku ya Malaria Duniani iliyofanyika mkoani Tabora na kusema kuwa kama nchi imeendelea kupiga hatua katika vita hivyo ikilinganishwa na miaka zaidi ya ishini iliyopita ambapo maambuki na vifo vya Malaria vilikuwa kati ya asilimia 45 hadi 50.

Aidha Dkt. Mollel amesema azma ya Serikali ni kufikia asilimia 3.5 ifikapo 2025 na kuwa na ziro Malaria 2030 huku akisisitiza kwa kusema itafikiwa endapo juhudi za Makusudi zitafanywa kwa ushirikiano baina ya Serikali na wadau

"Leo tunazungumza asilimia 8.1 kama nchi lakini miaka ya 1998, tulikuwa na kiwango cha juu sana, hivyo ili tuweze kufikia adhma yakumaliza kabisa malaria ifikapo 2030 kila mmoja wetu anawajibu wakufanya" amesema Mollel.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI Samsoni Maella, amesema Utumiaji wa Mifumo ya GoTHOMIS na FFARS imekuwa chachu ya kukusanya takwimu sahihi kwa ajili ya ngazi ya maamuzi, hali iliyochangia kufanya maamuzi sahihi kutokana na kuwa na takwimu sahihi.

"Kama Ofisi ya Rais TAMISEMI, tumefanikiwa kuimarisha miundo mbinu ya Afya na Rasilimali watu mathalani miaka mitatu nyuma tulikuwa na Hospitali za Wilaya 77 leo hii tunazo 177 hizi zimechochea sana uimarishaji wa huduma” amesema Mahela.

Naye Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI Dkt. Hamis Kigwangala ametoa wito kwa serikali na wadau kuongeza afua za kutibu watoto Shuleni, pia wafike maeneo ya Migodi, Mashamba Makubwa na maeneo ya Wafugaji.

Awali Msimamizi wa Miradi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Catherine Joachim, akiwa amemwakilisha Katibu Mkuu, amesema kuchaguliwa kwa mkoa wa Tabora kuwa mwenyeji wa Maadhimisho ya Wiki ya Malaria, ni pamoja na kuongeza nguvu ya afua za kupambana na Malaria kutokana na Mkoa huo kuwa na Maambukizi ya juu ya Ugonjwa huo ya asilimia 23.4 kwa sasa kutoka asilimia 11.7 kwa mwaka 2011.

read more

AIS SAMIA AKIWA KWENYE SHEREHE ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Afrika Mashariki ukiimbwa katika Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kushuka kwenye gari Maalum la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.
read more

MKUTANO MKUU WA ALAT 2024; WAZIRI MCHENGERWA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF

 ZANZIBAR

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma umeshiriki kwenye Mkutano Mkuu wa 38 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Zanzibar na kupata fursa ya kuelimisha kupitia maonesho na uwasilishaji wa mada kwa wajumbe wa mkutano Mkuu.

Mkutano huo muhimu hujumuisha Wenyeviti wa Mikoa na Halmashauri zote nchini, Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa zote nchini, Mameya, na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya ALAT.

Meneja wa Ofisi ya Zanzibar wa PSSSF, Bi. Amina Kassim aliwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuhusu maboresho ya kidijitali yaliyofanywa na PSSSF ili kuboresha huduma kwa wateja ikiwemo kuhusu mfumo mpya wa kupokea madai ya mafao mtandaoni na usajili wa wanachama mtandaoni.

Aidha aliwaomba waendelee kutoa ushirkiano ili kutatua changamoto za kiutendaji kwa wakati.

Mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa na kufungwa na Waziri wa Nchi Ofisi yanRais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud Ali Mohamed.

Mkutano Mkuu umehudhuriwa na wajumbe na taasisi wadhamini takribani 450.




read more

LENGO LA SERIKALI NI KUBORESHA MAISHA YA KILA MWANANCHI TARAFA YA NGORONGORO-NCAA


SERIKALI kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesema kuwa ina lengo la kuboresha maisha ya wananchi wa tarafa hiyo kwa kuwaelimisha na kuwahamisha wananchi waliojiandikisha kuhama kwa hiyari kwenda Kijiji cha Msomera Handeni Mkoani Tanga na maeneo mengine nchini.

Akizungumza na wananchi wa tarafa ya Ngorongoro kwa nyakati tofauti katika zoezi la uelimishaji, uhamaishaji na uandikishaji kaimu meneja wa Uhusiano kwa Umma wa mamlaka hiyo Hamis Dambaya amesema zoezi la kuwaelimisha wananchi hao litaendelea ili kuhakikisha kila mkazi wa tarafa ya Ngorongoro anahama kwa hiyari.

Amewaeleza wananchi hao kwamba serikali haina nia mbaya kwa kuwashawishi kuhama kutoka ndani ya hifadhi kwani inatambua kuwa iwapo wananchi hao watakubali kuhama wataweza kuboresha maisha yao katika maeneo mbalimbali watakayoamua kuelekea sambamba na kulinda usalama wao kutokana na uwepo wa matukio ya wanyama wakali ndani ya hifadhi.

“Mnaishi katika mazingira magumu hasa kutokana na kukosa uhuru wa kuingia na kutoka ndani ya hifadhi, kuhofia Wanyama wakali ambao wamekuwa hatari kwa mifugo na baadhi ya wananchi, serikali imefanya uamuzi sahihi wa kuwahamasisha ili kuwa na Maisha bora na huru nje ya hifadhi,”alisema bwana Dambaya.

Bwana Dambaya amesisitiza kuwa serikali imejipanga vizuri katika kuhakikisha kila mwananchi anayekubali kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi anapata stahiki zake zote za kisheria ikiwemo kitita cha shilingi milioni kumi wanaohamia msomera na shilingi Milioni kumi na tano wanaohamia maeneo mengine ambapo fedha hizi zinatolewa kama motisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Amewataka wananchi hao kuachana na propaganda za baadhi ya wanasiasa na wanaharakati wasiowatakia mema kwa kuwashawishi kuendelea kubaki ndani ya hifadhi huku wao na familia zao wakiishi katika miji mbalimbali nchini na kufanya shughuli zao katika mazingira magumu.

“Msihadaike na watu wenye nia ovu wanaowashawishi mbaki ndani ya hifadhi, hameni kwa hiyari kuelekea katika Kijiji cha Msomera na maeneo mengine ambayo huduma za kijamii zimeboreshwa kwa mustakabali wenu na vizazi vyenu”,alisema bwana Dambaya.

Katika ziara hiyo ya tarafa ya Ngorongoro timu ya uhamasishaji imeweza kutembelea kaya mbalimbali katika Kijiji cha Naiyobi, Kapenjiro na endulen ambapo wananchi kadhaa walielimishwa na kukubali kuhama kwa hiyari na kuamua kujiandikisha.
read more

NMB YADHAMINI MKUTANO MKUU WA ALAT TAIFA

 


NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR
 
BENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. Mil. 120 kudhamini Mkutano Mkuu wa 38 wa Mwaka wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT Taifa), unaofunguliwa Jumanne Aprili 23 na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ukiwakutanisha washiriki zaidi ya 600.
 
Kiasi hicho kinachodhamini mkutano wa mwaka huu unaofanyika chini ya kaulimbiu; ‘Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Jambo Letu; Shiriki kwa Maendeleo ya Taifa,’ kinafanya udhamini wa NMB kwa ALAT Taifa kufikia Sh. Bil. 1.2 katika kipindi cha miaka nane.
 
Mkutano Mkuu wa ALAT, unaowapa fursa viongozi wa Serikali Kuu kutoa Maelekezo na Miongozo ya Kisera kwa Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, wakiwemo Mameya wa Majiji na Manispaa, Wenyeviti na Wakurugenzi wa Halmshauri 184 (za Tanzania Bara), utafungwa Aprili 25 na Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi.
 
Kwa miaka nane sasa, NMB na ALAT zimekuwa na ushirikiano endelevu katika masuala mbalimbali kwa maendeleo ya Halmashauri zote nchini, ikiwemo kudhamini na kufanikisha vikao na Mikutano Mikuu ya Mwaka ya ALAT, ambayo kimsingi ndio chachu ya utendaji bora kwa Halmashauri hizo.
 
Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano hayo, iliyofanyika Golden Tulip Zanzibar Airport Hotel, Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipuna, alisema wanajivunia kuwa wabia wakubwa wa ALAT, na kwamba wanathamini heshima ya kipekee wanayopewa na uongozi wa jumuiya hiyo.
 
“NMB tunajivunia ubia baina ya benki yetu na Jumuiya hii, lakini pia tunathamini sana heshima ya kipekee ambayo tumekuwa tukipewa na Uongozi wa ALAT Taifa ya kujumuika pamoja nao katika Mkutano Mkuu huu muhimu kwa maendeleo ya Halmashauri zetu nchini.
 
“Kwa siku zote za Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa, tutakuwa na banda letu nje ya ukumbi wa mkutano, ili kuhakikisha wajumbe wa kikao pamoja na wadau wengine watakaokuwa katika maeneo ya Golden Tulip Hotel, wanapata huduma za kifedha wakati wote wa kikao.
 
“Nitumie nafasi hii pia kuwaalika wote katika banda la NMB kupata Huduma Jumuishi za Kifedha muwapo katika mkutano huo, na niwakikishie tu kwamba wafanyakazi wetu watakuwepo kutoa huduma na ushauri kwa wajumbe kwa wakati wote,” alisema Bi. Zaipuna.
 
Aidha, sambamba na udhamini huo, Bi. Zaipuna alibainisha kuwa, NMB imeandaa mchapalo kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa, ambako aliwakaribisha kushiriki chakula cha jioni, pamoja na kujadiliana machache baina ya Wajumbe ALAT na wafanyakazi wa NMB.
 
Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Bw. Sima Constantine Sima, aliishukuru NMB kwa ubia endelevu unaowawezesha kufanikisha vikao na Mikutano Mikuu ya kila mwaka kwa kipindi cha miaka nane sasa ya udhamini wao.
 
“Shukrani za Jumuiya yangu ziifikie Benki ya NMB kwa hiki inachofanya katika kufanikisha Mikutano Mikuu ya ALAT Taifa kwa miaka nane sasa na hii ndio tafsiri sahihi ya mahusiano mema na ya muda mrefu, ambayo sisi ALAT ndio wanufaika wakuu.
 
“NMB sio tu wadau wetu kibiashara, bali wao wamekuwa moja ya sehemu kuu za sisi kutolea huduma zetu. Mambo mengi yanayoendelea kufanyika katika Halmashauri zetu yanapitia kwao na ndio ushuhuda wa hili na mahusiano haya ndio tafsiri sahihi ya tunayoyaona kwa miaka nane ya udhamini wao.
 
Nichukue nafasi hii kuishukuru NMB kwa kutafsiri kwa vitendo juu ya mahusiano mema, ambapo leo pia imedhamini uzinduzi wa kimapinduzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa Zanzibar (ZALGA), ambayo ni mamlaka sawa na ALAT kwa huku visiwani Zanzibar,” alisema Sima.
 
Aidha, aliishukuru NMB kwa kuandaa hafla ya chaklula cha usiku baina ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa na Wafanyakazi wa NMB, na kwamba anaamini mchapalo huo utakuwa fursa nzuri sio tu ya kubadilishana Mawazo, bali kufurahi pamoja baada ya kazi.
read more

BIMA YA AFYAPASS KUTOKA VODABIMA

 Mwamko mdogo wa Watanzania kuhusu bima ya afya ni mojawapo ya changamoto katika kutoa huduma bora za afya kwa wote kutokana na idadi ndogo ya Watanzania wenye bima. Takwimu za Wizara ya Afya (2022) zinaonesha kuwa asilimia 15 tu ya Watanzania, sawa na watu milioni 9.1, walikuwa na bima ya afya mwishoni mwa mwaka 2021, ikishuka kutoka asilimia 32% mwaka 2018.


Vodacom Tanzania PLC imeungana na Assemble Insurance na kuja na bima ya afya ya kijiditali kupitia simu ya mkononi iitwayo AfyaPass ambayo ni rahisi, nafuu, na inapatikana kwa Mtanzania popote pale alipo nchini. Bima hii inapatikana kwa bei nafuu ya Shilingi 70,000 kwa mwaka kwa mtu mmoja na vifurushi vya familia kutoka TZS 105,000 kwa watu wawili hadi TZS 385,000 kwa watu sita kwa mwaka na inapokelewa katika hospitali binafsi na za serikali. Kwa malipo kidogo ya nyongeza, mtumiaji anaweza kupata huduma za uzazi, radiolojia, mazoezi tib ana nyingine nyingi.

Unaweza kujiunga na AfyaPass kupitia M-Pesa ikiwa ni moja ya aina za bima zinazotolewa kupitia VodaBima yenye lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa kila mtu bila kujali kipato chake au umbali wa eneo anapotoka nchini Tanzania.
Kamishna wa Bima kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Dk. Baghayo Saqware (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa M-Pesa, Epimack Mbeteni (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Assemble Insurance, Tabia Massudi (kushoto) wakiwa na vipeperushi kuashiria uzinduzi wa kampeni ya “VodaBima kidigitali, Ni Chap, ni Nafuu” inayohamasisha matumizi ya Bima Kidigitali uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kampuni ya Vodacom Tanzania kupitia huduma zake za VODABIMA zinazopatikana kwa M-Pesa, itanufaisha wagonjwa wa kulazwa na kutwa, vyombo vya moto na bima ya maisha kwa mtu mmoja mmoja na vikundi kwa gharama nafuu.
read more