Latest Articles

BURIANI MZEE MWINYI

Allah ajaalie roho ya Kipenzi chetu Mzee Mwinyi. Aiweke mahala Pema Peponi" Mwenyekiti CCM mkoa wa Dar es Salaam Mtemvu

read more

MUFTI KUONGOZA SWALA YA JENEZA YA HAYATI RAIS WA AWAMU YA PILI. MZEE MWINYI.

  Taarifa ya Mh. Waziri mkuu Kassim Majaliwa imesema Mwili wa Hayati Alhaj Ali Hassan Mwinyi utawasili Msikiti wa mfalme Mohammed VI Bakwata makao makuu Saa tano asubuhi hii.


Kwa upande mwingine katibu mkuu wa Bakwata Alhaj Nuhu Mruma amesema Maandalizi kupokea mwili wa Kipenzi cha watanzania yamekamilika na kwamba Swala ya jeneza itaswaliwa mara tu baada ya swala ya Ijumaa ikiongozwa na Samaha Mufti Dr. Abubakar Zubeir

.....

Dr. Harith Nkussa

Na. 

Mwandishi wetu. 

Ijumaa 1.3.2024

Dar es salaam.

read more

JKCI DAR GROUP KUPIMA MAGONJWA YA MOYO

 

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Idd Lemmah akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba itakayofanyika tarehe 2 na 3 Machi 2024 katika viwanja vya Hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Kaimu mkuu wa huduma za tiba wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Eva Wakuganda akielezea huduma zitakazotolewa katika kambi maalumu ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani. Kambi hiyo itafanyika tarehe 2 na 3 Machi 2024 katika viwanja vya Hospitali ya JKCI Dar Group iliyopo Tazara jijini Dar es Salaam.

 Mwakilishi wa umoja wa wanawake Hospitali ya JKCI Dar Group Debora Mkemwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba itakayofanyika tarehe 2 na 3 Machi 2024 katika viwanja vya Hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani.


Mwakilishi wa umoja wa wanawake Hospitali ya JKCI Dar Group Debora Mkemwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kambi maalumu ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba itakayofanyika tarehe 2 na 3 Machi 2024 katika viwanja vya Hospitali hiyo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

Picha na: Khamisi Mussa

************************************************************************************************* 

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Hospitali ya Dar Group kuadhimisha siku ya wanawake duniani kwa kufanya kambi maalumu ya upimaji na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa wananchi.

Kambi hiyo ya siku mbili itafanyika katika viwanja vya Hospitali ya JKCI Dar Group tarehe 2 na 3 Machi 2024 kwa kufanya uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto na watu wazima.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya JKCI Dar Group Idd Lemmah alisema upimaji huo unafanyika kupitia kambi maalumu ijulikanayo kama Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tiba mkoba iliyolenga kuwafikishia watanzania huduma za matibabu karibu.

“Tunawakaribisha watanzania mjitokeza, hususani watu wanaoizunguka Hospitali hii wa Tazara na Temeke mfike katika siku hizi mbili mchunguze afya zenu”, alisema Lemmah

Kwa upande wake Kaimu mkuu wa huduma za tiba wa Hospitali ya JKCI Dar Group Dkt. Eva Wakuganda alisema kupitia kambi hiyo wananchi watapata fursa ya kutibiwa na wataalamu wa afya mabingwa wa magonjwa ya moyo.

Dkt. Eva ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto alisema wanawake wa JKCI Dar Group wameona umuhimu wa kuadhimisha siku ya wanawake duniani kwa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwasababu wagonjwa wengi wamekuwa wakichelewa kufika hospitali kwaajili ya kupata matibabu.

“Kila watoto 100 wanaozaliwa mtoto mmoja uzaliwa na magonjwa ya moyo lakini bahati mbaya hawafiki hospitali mapema kwaajili ya kupatiwa matibabu hivyo kupitia kambi zetu za matibabu tunawatambua mapema na kuwapa huduma mapema”, alisema Dkt. Eva

Dkt. Eva alisema kupitia kambi hiyo wananchi hupata elimu ya lishe na elimu ya kutambua magonjwa ya moyo hivyo kuwapa nafasi kujilinda na magonjwa hayo na pale wanapoyapata kuweza kuona dalili zake mapema hivyo kuwahi hospitali.

“Dalili za magonjwa ya moyo kwa watoto ni pamoja na kubadilika rangi kuwa wa bluu kwenye midomo na vidole, kushindwa kupumua vizuri, kutokuongezeka uzito, mapigo ya moyo kwenda mbio, kuchoka na kutokwa na jasho mara kwa mara”, alisema Dkt. Eva

Naye mwakilishi wa umoja wa wanawake Hospitali ya JKCI Dar Group Debora Mkemwa alisema wanawake wa Hospitali hiyo wameona umuhimu wa kuadhimisha siku ya wanawake duniani kwa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi kwani wanawake ndio nguzo ya kujenga familia bora.

“Wanawake ni msingi wa kuhakikisha familia zetu zinakuwa bora na imara kama ambavyo kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani ya mwaka huu inavyosema ‘Wekeza kwa wanawake kwaajili ya maendeleo endelevu”,alisema Debora

Debora alisema wanawake watakapofikiwa na taarifa za upimaji huo watoe taarifa ndani ya familia zao, kuwahamasisha watu waliopo katika familia zao ili kwapamoja waweza kupata fursa ya kupima moyo.

“Kambi kama hizi zinapofanyika zinampa mwananchi fursa ya kujijua, kupata matibabu kwa wakati, kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu tofauti na mtu anayefika hospitali kwa kuchelewa”, alisema Debora
read more

RAIS SAMIA ATANGAZA KIFO CHA ALI HASSAN MWINYI

  RAIS Samia Suluhu Hassan ametangaza msiba wa Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi kilichotokea majira saa 11 jioni katika Hospitali ya Mzena, jijini Dar es Salaam 

Amesema kuwa Mzee Mwinyi alikuwa anasumbuliwa na saratani ya mapafu anatarajiwa kuzikwa Unguja- Zanzibar Machi 2, 2024.


Wakati wa maombolezo bendera zitapepea nusu mlingoti kwa siku 7.

read more

WAAJIRI WAASWA KUTII SHERIA ZA KAZI

 Na Mwandishi Wetu


Waziri wa Nchi - Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako amewataka wawekezaji wa maeneo ya kazi nchini kutekeleza sheria na miongozo mbalimbali ya masuala ya kazi ikiwemo Sheria Na.5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya Mwaka 2003.

Ndalichako ametoa agizo hilo mara baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika kampuni za usafirishaji za FAA Logistics, RAPHAEL Logistics pamoja kiwanda cha kutengeneza viroba cha MJM Manufacturing Ltd vya jijini Dar es salaam na kubaini mapungufu makubwa katika usimikaji wa mifumo ya kuwalinda wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vya magonjwa na ajali, wafanyakazi kutokuwa na mikataba, waajiri kutowasilisha michango katika mifuko ya hifadhi, pamoja na kutokulipa mishahara kwa wakati na ulimbikizaji wa madeni ya mishahara kwa wafanyakazi wao.

“Tumefanya ziara ya kushitukiza na tumebaini changamoto mbalimbali kwa wafanyakazi wa maeneo haya ya kazi hivyo basi napenda kutoa wito kwa waajiri na wawekezaji wote kuhakikisha wanazingatia sheria na miongozo mbalimbali ya masuala ya kazi lakini pia baada ya ziara hii naziagiza taasisi za OSHA, WCF, NSSF na Idara ya Kazi kurudi mara moja kuendelea na ukaguzi mpaka kufikia ijumaa ya machi 1 ili kushughulikia changamoto hizi kwa kuainisha wafanyakazi wangapi ambao michango yao haiwasilishwi katika mifuko ya hifadhi za jamii na wangapi hawakatwi kabisa lakini pia kushughulikia usimikaji wa mifumo madhubuti ya masuala ya usalama na afya mahali pa kazi” alisema Prof. Ndalichako, akiongeza kuwa

“Pia ­mfanye ukaguzi ili kutambua malimbikizo ya mishahara na stahiki zingine pamoja na wafanyakazi wasio na mikataba ili baada ya ripoti ya ukaguzi huu tuweze kutoa amri tekelezi kwa wawekezaji hawa na ndani ya siku thelathini tuweze kufikia makubaliano juu ya utatuzi wa changamoto hizi ”

Aidha ­Profesa Ndalichako amewahasa wafanyakazi katika maeneo yote ya kazi kutoa ushirikiano wa kueleza changamoto zinazowakabili bila uoga huku akiwataka waajiri kuacha mara moja tabia ya kuwaandama wafanyakazi wanao eleza changamoto zao wakati wa ziara za viongozi mbalimbali.

Kwa upade wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda amesema kuwa sekta ya usafirishaji ni sekta yenye mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi yetu lakini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali hivyo ziara hiyo ililenga kubaini changamoto hizo na kuona namna gani zinaweza kutatuliwa huku akibainisha kuwa kwa upande wa masuala ya usalama na afya katika kampuni hizo wakaguzi wa OSHA wabebaini kuna mapungufu makubwa katika utekelezaji wa sheria na miongozo ua masuala husika na tayari wametoa hati ya maboresho kwa wawekezaji hao.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako ( katikati mstari wa mbele ) akiwa pamoja na Wakuu wa taasisi za OSHA, WCF, NSSF na Idara ya Kazi wakisikiliza kero mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi katika utekelezaji wa majukumu yao wakati Walipotembelea katika kwanda cha RAPHAEL Logistics kilichopo Ubungo Jijini Dar es alaam.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi Khadija Mwenda akizungumza na mfanyakazi wa kampuni ya FAA Logistics wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako (kushoto kwake) pamoja na wakuu wa taasisi zilizochini ya ofisi yake iliyolenga kukagua utekelezaji wa sheria na miongozo mbalimbali ya kazi.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na mfanyakazi wa kiwanda cha kutengeneza viroba cha MJM Manufacturing Jijini Dar es salaam alipotembelea kiwanda hicho kwa lengo la kukagua utekelezaji wa sheria na miongozo mbalimbali ya kazi.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako akikagua mifumo ya usalama na afya katika kiwanda cha kutengeneza viroba cha MJM Manufacturing kilichopo Tabata Dar es salaam.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi Khadija Mwenda akisisitiza jambo kwa viongozi wa Kampuni ya usafirishaji ya RAPHAEL Logistics (hawapo pichani).
read more

RCHMT, CHMT SIMAMIENI MIRADI YA AFYA IKAMILIKE KWA WAKATI

  Na Mwandishi wetu Arusha


Timu za Usimamizi na Uratibu wa shughuli za afya ,Lishe, na Ustawi wa Jamii ngazi ya Mkoa (RCHMT) na Halmashauri (CHMT) zimetakiwa kusimamia ipasavyo ujenzi wa miradi ya afya viporo ikamilike kwa wakati ili kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Mkurugenzi wa Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais -TAMISEMI Dkt. Rashid Mfaume ametoa kauli hiyo leo Februari 26, 2024 jijini Arusha alipokuwa akihitimisha ziara yake ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya ya Afya na kukagua hali ya utoaji wa huduma za afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha na Halmashauri ya Jiji la Arusha mkoani Arusha.

Dkt Mfaume amesema kuna baadhi ya maeneo miradi ya afya inasuasua na mingine haijakamilika na kuzielekeza timu hizo kuhakikisha inakamilika na kuanza kutoa huduma kwa jamii.

"Tusingependa kuona miradi imefikia asilimia 80 hadi 95 kuendelea kubaki hivyo na haikamiliki,hii haivumiliki hakikisheni inakamilika, RCHMT na CHMT ni jukumu lenu la msingi la kuhakikisha mnasimamia miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yenu,hivyo hatutasita kuwachukulia hatua wale wote watakaolegalega katika suala hili,"amesema.

Amesema serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu, ununuzi wa vifaa, vifaa tiba pamoja na dawa hivyo ni wajibu wao kusimamia vituo vyote vya kutolea huduma vianze kufanya kazi.

Vilevile, ametaja mafanikio mengine ni kuajiri watumishi wa kada ya afya 17,000 na katika mwaka wa fedha 2023/24 tayari wameomba kibali cha kuajiri watumishi zaidi ya 10,305 na kuwataka viongozi hao kusimamia nidhamu kwa watumishi ili kutoa huduma bora kwa wananchi.
read more

KAMATI YA HUDUMA YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YATEMBELA JKCI

Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Deogratis Nkya akiwaonesha wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi  jinsi wanavyofanya upasuaji wa kuzibua tundu la moyo wa mtoto bila ya kufungua kifua wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI Aprili 21, 2024  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Dkt. Nkya  ni makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Jimbo la Kigamboni.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi aina za upasuaji wa moyo zinazofanyika katika Taasisi hiyo wakati kamati hiyo ilipotembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni misimamizi wa wodi ya watoto Theresia Marimo akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi huduma za matibabu ya moyo wanazozipata watoto waliolazwa katika wodi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaongoza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi kwenda kuona ujenzi wa jengo la utawala na vipimo unavyoendelea. Kushoto kwa Mkurugenzi  ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni.

  Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Mhe. Waziri ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  na kushoto ni Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt.Godwin Mollel.

   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisoma taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.
  Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  akizungumza na vyombo vya habari wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA).

read more