MAKUMI YA WASICHANA WATOWEKA YOBO BAADA YA SHAMBULIZI LA BOKO HARAM
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:32 AM
Zaidi ya wasichana 90 wa shule wanahofiwa
kutoweka baada ya kundi la kigaidi la Boko Haram kushambulia kijiji
kimoja cha kaskazini mashariki mwa jimbo la Yobo nchini Nigeria.
Kutoweka
kwa wasichana hao litakuwa miongoni mwa matukio makubwa ya aina hiyo
tangu kundi la Boko Haram lilipoteka nyara wasichana 270 wa shule ya
sekondari ya Chibok mwaka 2014. Tukio hilo lilielekeza macho ya
walimwengu kwenye uasi wa karibu miaka 10 wa kundi hilo ambao Umoja wa
Mataifa unautaja kuwa ni miongoni mwa migogoro mibaya zaidi duniani.
Baadhi ya watu wa eneo hilo wanasema waliwaona wasichana katika magari matatu aina ya Tata wakilia na kuomba msaada.
Polisi
ya Nigeria na afisa mkuu wa elimu katika eneo hilo la Dapchi
hawajathibitisha habari hiyo ingawa familia na watu walioshuhudia
wanasema wasichana wengi wametoweka. Baadhi ya familia zimethibitisha
kwamba watoto wao wa kike waliokuwa katika shule hiyo wametoweka.
Watu walioshuhudia wamesema kuwa, wapiganaji wa kundi la kigaidi la
Boko Haram waliingia eneo la Dapchi Jumatatu iliyopita kwenye magari
kadhaa wakiwa na bunduki. Waasi hao walifyatua risasi ovyo na
kuwalazimisha baadhi ya wasichana na walimu wa shule ya eneo hilo
kukimbia.
Zaidi
ya watu elfu 20 wameuawa na mamilioni ya wengine kuwalazimika kuwa
wakimbizi tangu kundi hilo la Boko Haram lilipoanzisha uasi nchini
Nigeria mwaka 2009.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: