OPERESHENI YA KULIPIZA KISIASA YA YEMEN YAUA ASKARI 7 WA SAUDIA

Operesheni ya kulipiza kisiasa ya Yemen yaua askari 7 wa Saudia
Walenga shabaha stadi wa jeshi la Yemen wameua kwa kuwafyatulia risasi wanajeshi saba wa Saudi Arabia katika maeneo ya Najran na Jizan, ikiwa ni radiamali kwa mashambulizi ya anga ya Riyadh dhidi ya nchi hiyo.
Duru za kijeshi nchini Yemen zimesema walenga shabaha hao wa jeshi la Yemen wakishirikiana na vikosi vya kujitolea vya wananchi walifanya operesheni hiyo jana Ijumaa, ambao askari watano wa Saudia waliuawa katika kijiji cha Hamezah katika eneo la Jizan, yapata kilomita 967 kusini magharibi mwa mji mkuu wa Saudia, Riyadh.
Wanajeshi wengine wawili wa Saudia waliuawa jana alasiri kwa kumiminiwa risasi katika kambi ya jeshi ya Raqabat al-Zour, iliyoko katika eneo la Najran, umbali wa kilomita 844 kusini mwa Riyadh.
Sehemu ndogo ya hujuma za Saudia dhidi ya jirani yake Yemen
Mapema jana ndege za kivita za Saudia zilifanya mashambulizi matatu ya anga katika wilaya ya Razih, kaskazini mashariki mwa eneo la Sa'ada. 
Saudi Arabia na washirika wake waliivamia Yemen tangu mwezi Machi mwaka 2015 na hadi sasa nchi hizo zinaendelea kuizingira nchi hiyo kutokea nchi kavu, majini na angani na zimeua raia wasio na hatia zaidi ya 13,000 na kuwalazimisha mamilioni ya wengine kuwa wakimbizi. 

0 comments: