KOREA KASKAZINI: TRUMP NI MFANYABIASHARA WA VITA NA MNYONYAJI WA AMANI DUNIANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:38 PM
Serikali ya Korea Kaskazini imejibu matamshi
ya uhasama ya Rais Donald Trump wa Marekani kupitia mtandao wa kijamii
wa Twitter na kusema kuwa, Trump ni mfanyabiashara wa vita na mnyongaji
wa amani duaniani.
Gazeti la serikali ya Korea
Kaskazini la Rodong Sinmun limeandika kuwa, Pyongyang itaendelea
kusimama imara kwa nguvu zake zote dhidi ya vitisho vya Washington.
Taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari vya Korea Kaskazini imesema
kuwa, serikali ya Marekani chini ya uongozi wa Rais Donald Trump
inashadidisha mgogoro katika Peninsula ya Korea kwa lengo la kuimarisha
soko la mauzo ya silaha zake kwa Korea Kusini na Japan.
Hii ni katika hali ambayo, hadi sasa
tayari serikali za Seoul na Tokyo zimetangaza mpango wao wa kununua
silaza za kisasa za Marekani, ukiwemo mpango wa kununua ndege za kivita
aina ya F-35 za Marekani. Kabla ya hapo pia, Trump alitangaza kupitia
ujumbe aliouandika kwenye mtandao wa Twitter akitoa idhini ya kuziuzia
nchi hizo mbili (yaani Korea Kusini na Japan) silaha za kisasa kwa kile
alichokisema kuwa ni kukabiliana na Korea Kaskazini. Mgogoro wa
Peninsula ya Korea umeendelea kuongezeka kutokana na siasa za uhasama za
Marekani kwa kushirikiana na washirika wake katika eneo hilo. Kwa mara
kadhaa Pyongyang imekuwa ikisisitiza kujizatiti kwa silaha za nyuklia na
makombora ya balestiki madamu Marekani itaendeleza mkondo wake wa
vitisho na uhasama dhidi yake.
Katika hatua nyingine, Waziri wa Mambo
ya Nje wa Korea Kusini amesema kuwa, Korea Kaskazini inalipa gharama
kutokana na majaribio ya silaha zake za nyuklia na kurusha makombora ya
balestiki. Kang Kyung-wha amesema kuwa, Pyongyang itaendelea kukabiliwa
na matatizo makubwa ya kiuchumi kutokana na vikwazo ilivyowekewa na
kwamba hatua hiyo inatokana na kulipa gharama ya kile alichokisema kuwa
ni kuchafua usalama wa eneo la Korea.
Ameongeza kwa kusema kuwa, baadhi ya
nchi za Magharibi zimekusudia kushadidisha zaidi vikwazo vyao kwa Korea
Kaskazini na kwamba suala la nchi hiyo limekuwa ni changamoto kubwa
katika siasa na usalama za Korea Kusini. Aidha amesisitiza kuwa huwenda
vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini vikaendelea kuwepo kwa miaka mingi
zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: