WAASI WA KIKRISTO WAUA WAISLAMU 25 JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Magaidi wa Anti Balaka wakiwatishia kuwakata vichwa Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati Magaidi wa Anti Balaka wakiwatishia kuwakata vichwa Waislamu Jamhuri ya Afrika ya Kati
Waasi wa Kikristo wenye mfungamano na genge la kigaidi la anti-Balaka wameua Waislamu 25 ndani ya msikiti katika mji wa Kembe wa kusini mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Abdourahman Bronou, mkuu wa baraza la wazee katika mji wa Kembe amethibitisha habari hiyo na kusema kuwa, waasi hao waliuzingira na kuushambulia msikiti huo mapema Jumatano asubuhi.
Akizungumza Ijumaa, Bornou ameongeza kuwa, katika hujuma hiyo ya kigaidi Imamu wa msikiti na naibu wake walikuwa miongoni mwa waliouawa. Wakuu wa mji huo wametangaza siku tatu za maombolezo.
Machafuko huko Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) yalizuka mwaka 2013, baada ya waasi wa Seleka kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo, François Bozizé. Baada ya rais Mwislamu, Michel Djotodia kuchukua mamlaka, waasi na magaidi wa Kikristo wenye misimamo ya kufurutu ada wa Anti-Balaka walianzisha mauaji ya kimbari dhidi ya jamii ya Waislamu, ambapo maelfu ya Waislamu waliuawa na wengine wengi kuwa wakimbizi.
Askari wa kulinda amani wa UN wameshindwa kuzuia mauaji ya Waislamu CAR
Djotodia alilazimishwa na nchi za eneohilo kujiuzulu mwezi Januari mwaka 2014 na hapo mauaji ya Waislamu yakashika kasi zaidi. Kabla ya kuanza mgogoro huo, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui, ulikuwa na Waislamu 130,000 lakini hivi sasa taarifa zinasema idadi hiyo ni chini ya 1,000.
Aidha watu zaidi ya 400,000, wengi wao wakiwa ni Waislamu wamelazimika kukimbia makazi yao huku wengine milioni 2.7, au nusu ya watu wote CAR wanahitaji msaada. Mauaji ya Waislamu CAR yanajiri licha ya kuweko askari wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo.

0 comments: