Na Magreth Magosso,Kigoma
WALIMU wanajifunza mafunzo ya uimarishwaji wa stadi
za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) Mkoa wa
Kigoma wameiomba serikali kuweka mazingira rafiki kwa walimu na
wanafunzi ili kuleta tija katika matokeo ya wahitimu wa darasa la saba.
Maombi hayo waliyatoa juzi katika
hafla ya uzinduzi wa mafunzo hayo ambayo kimkoa yanafanyika katika chuo cha
ualimu cha kasulu na kuongeza kuwa licha ya mtaala wa sasa kuwa na mbinu
shirikishi za kumuwezesha mwalimu kumuandaa vizuri mwanafunzi serikali haina
budi kuongeza kasi katika utatuzi wa baadhi ya changamoto zinazoikabili
sekta ya elimu.
Wakizungumza baada ya ufunguzi wa
Mafunzo hayo baadhi ya Walimu hao akiwemo Mwalimu, Geogre Jelome alisema
mafunzo hayo yenye lengo la kuwawezesha Walimu kuwaandaa wanafunzi katika stadi
za KKK kwa kumuwezesha Mwanafunzi kumaliza shule akiwa na uwezo wa kujiajili.
" mafunzo haya tumeyafurahia ,kabla
hatujapata mafunzo haya ilitupa shida sana kutumia mtaala wa zamani na
wanafunzi walikuwa hawashirikishwi kwa namna yoyote kwa sasa tunauhakika wa
kuwafundisha wanafunzi na kuelewa kwa makini sana nakumaliza shule wakiwa
nauwezo wa kujua kusoma na kuandika", alisema Jelome.
Jelome alisema Ilikufanikisha Mtaala
huo unafanikiwa ni kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa kuboresha nyenzo za
ufundishaji, posho za walimu na Madarasa ya kutosha ilikuhakikisha wanafunzi
wanashilikishwa katika mbinu za ufundishaji.
Kwa upande wake Mratibu wa mafunzo
hayo kitaifa Mwalimu Richard Ibraimu alisema wanawajengea uwezo walimu wa
shule za msingi hasa darasa la tatu na la nne ,kuwa na mbinu za kufundisha
wanafunzi ili,wafahamu haraka kusoma kuandika na kuhesabu (KKK ).ili kuongeza ufanisi kwa wahitimu
darasa la saba.
Alisema mafunzo hayo ni muendelezo
wa mafunzo ya uimalishaji wa stadi za KKK yaliyofanyika awali kwa mikoa19 ya
Tanzania bara ambapo Mikoa saba iliyokuwa chini ya program ya Equipt ukiwemo
Mkoa wa Kigoma haikupata mafunzo hayo, Serikali kupitia WyEST pamoja na
OR-TAMISEMI imeona ni muhimu sasa kwa mikoa hii kupewa mafunzo hayo
ilikuhakikisha kuwa kunakuwa na mfanano wa kitaifa.
Akizungumza katika ufunguzi wa
mafunzo hayo katibu tawala mkoa wa kigoma Charles Palangyo aliwataka walimu hao
kutumia ujuzi huo ili kuongeza kiwango cha ufaulu na ufanisi wa wanafunzi
katika mkoa wa kigoma.
Alisema ,Kigoma ni miongoni mwa
mikoa ambayo inafanya vizuri katika matokeo ya Darasa la saba , kidato cha nne
na cha sita endapo walimu hao watatumia ipasavyo mafunzo hayo waliyo yapata
itasaidia kufanya vizuri zaidi kutokana na wanafunzi wengi wanavipaji .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: