KAMATI YA HUDUMA YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YATEMBELA JKCI

Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Deogratis Nkya akiwaonesha wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi  jinsi wanavyofanya upasuaji wa kuzibua tundu la moyo wa mtoto bila ya kufungua kifua wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI Aprili 21, 2024  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Dkt. Nkya  ni makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Jimbo la Kigamboni.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi aina za upasuaji wa moyo zinazofanyika katika Taasisi hiyo wakati kamati hiyo ilipotembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

Afisa Uuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni misimamizi wa wodi ya watoto Theresia Marimo akiwaeleza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi huduma za matibabu ya moyo wanazozipata watoto waliolazwa katika wodi hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwaongoza wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi kwenda kuona ujenzi wa jengo la utawala na vipimo unavyoendelea. Kushoto kwa Mkurugenzi  ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni.

  Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa. Kulia kwa Mhe. Waziri ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  na kushoto ni Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt.Godwin Mollel.

   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akisoma taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa wajumbe wa kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea JKCI  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.
  Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya  bunge ya Afya na masuala ya Ukimwi Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile Mbunge wa Kigamboni  akizungumza na vyombo vya habari wakati kamati hiyo ilipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  kwa ajili ya kuona huduma mbalimbali za matibabu ya moyo zinazotolewa.

(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA).

0 comments: