ZITTO KABWE: MUNGU ALIAMUA NIINGIE MAHABUSU ILI NIJIONEE MATESO WANAYOPATA WANANCHI WENZANGU TANZANIA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:16 PM
Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini, magharibi
mwa Tanzania kupitia chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe
amesema kuwa, inawezekana Mungu aliamua yeye akamatwe jana na polisi na
kisha apelekwe mahabusu ili aweze kushuhudia mateso wanayoyapata watu
wanaozuiliwa korokoroni kinyume cha sheria.
Akizungumza
baada ya kuachiliwa na polisi mkoani Morogoro alikokuwa amezuiliwa
Zitto ameelezea kile alichokikuta katika mahabusu hizo na kusema, kuna
watuhumiwa waliowekwa mahabusu kwa muda mrefu bila ya kupelekwa
mahakamani, suala ambalo mbali na kukiuka sheria, pia linawafanya watu
hao kutojua mustakbali wao.
"Huko mahabusu nimekuta watuhumiwa wengi
ambao wengi wao wamekaa mahabusu bila ya kufunguliwa mashataka yoyote.
Inawezekana Mungu ameamua niingie huko ili nijionee mateso wanayopata.”
Amesema Zitto.
Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Ulrich
Matei amekanusha madai ya mbunge huyo wa Kigoma Mjini magharibi mwa
Tanzania juu ya kuwepo watuhumiwa wa muda mrefu katika kituo hicho
akisema kuwa watuhumiwa wote hufikishwa mahakamani kwa wakati.
Matei ameyasema hayo ikiwa ni saa chache
baada ya Zitto Kabwe kuachiliwa huru kwa dhamana na kuongeza kwamba,
polisi ilimkamata na kumuweka mahabusu kwa kuwa alifanya mkutano wa
hadhara bila ya kibali. Ameongeza kuwa, mbunge huyo anashtakiwa kwa
vifungu 74 na 75 vya kanuni ya adhabu kwa kufanya mkutano bila ya
kibali. Kamanda huyo amesema awali Zitto alikuwa akifanya mkutano wa
ndani, lakini baadaye wananchi walijaa nje na ndipo alipotoka na
kuwahutubia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: