KUUAWA ASKARI WENGINE 12 WA IMARATI NCHINI YEMEN, MATOKEO YA KUPENDA KUJITANUA SAUDIA NA ABUDHABI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 7:52 AM
Wizara ya Ulinzi ya Yemen inayofungamana na
Harakati ya Wananchi ya Answarullah, imetangaza habari ya kuangamizwa
askari wengine 12 wa Imarati katika mji wa Taiz ulioko kusini mashariki
mwa nchi hiyo.
Hadi sasa mji wa Taiz umekuwa
ukishuhudia mapigano na vita vya niaba. Kabla ya hapo pia yaani mwezi
Novemba mwaka 2015 na Novemba 2017, mji huo ulishuhudia mapigano makali
kati ya jeshi la Yemen kwa kushirikiana na Harakati ya
Answarullah pamoja na wanamgambo wa Abdrabbuh Mansur Hadi, rais wa
zamani wa Yemen aliyejiuzulu na kutoroka nchi kupitia vita vya muungano
wa Saudia dhidi ya nchi hiyo, na hivi sasa pia ndani ya mwezi huu wa
Februari, Taiz kwa mara nyingine tena unashuhudia vita na mapigano.
Chanzo cha mapigano na vita hivyo kinarejea kwenye nafasi ya kijografia
uliyonayo mji wa Taiz huko kusini mwa mji mkuu wa Yemen Sana'a, mji
ambao uko umbali wa kilometa 256 kutoka mji huo.
Kwa ibara nyingine ni kwamba, Taiz
unahesabiwa kuwa lango la kuingilia mji wa Sana’a na kwa ajili hiyo
kudhibitiwa na wapinzani wa ndani na vibaraka wa Saudia, kunaweza
kuwafanya vibaraka hao kuingia mji mkuu huo wa Yemen ambao kwa sasa uko
mikononi mwa harakati ya Answarullah na jeshi la taifa hilo. Hata kama
nafasi ya Answarullah na jeshi la Yemen bado ni nzuri mjini Taiz, hata
hivyo baadhi ya maeneo ya mkoa huo bado yako mikononi mwa askari
wanaomuunga mkono Mansur Hadi, huku maeneo mengine yakiwa mkononi mwa
magaidi wa kundi la ukufurishaji la al-Qaidah. Katika hali ambayo askari
wa Saudia na Imarati kwa kushirikiana na askari wanaomuunga
mkono Abdrabbuh Mansur Hadi na baadhi ya wapiganaji wa kikabila
wamefanya juhudi kubwa ndani ya kipindi cha miaka mitatu iliyopita kwa
ajili ya kuishinda harakati ya Answarullah na jeshi la Yemen, lakini
juhudi hizo zimekuwa zikigonga mwamba.
Katika matukio ya hivi karibuni zaidi
yanayohusiana na mkoa huo, ni kuangamizwa askari 12 wa Imarati sambamba
na kujeruhiwa wengine kadhaa na hivyo kwa mara nyingine kuifanya Abu
Dhabi inayopenda kujitanua ipate hasara kubwa nchini humo. Moja ya
sababu za hasara hiyo, ni kupenda kujitanua na nafasi haribifu ya
Imarati nchini Yemen. Weledi wa masuala ya Mashariki ya Kati
wanazungumzia nafasi hiyo haribifu ya Imarati nchini Yemen kwa kusema: “Nafasi
hiyo haribifu inatekelezwa kwa kuzua mapigano ya ndani kati ya makundi
tofauti sambamba na kutuma fedha na silaha moja kwa moja kwa makundi
hayo vibaraka na kadhalika kujenga jela za kutisha, kuendesha mauaji ya
kuvizia na kushirikiana na wanachama wa kundi la kigaidi la al-Qaidah
nchini humo. Lengo kuu la njama zote hizo ni kuweza kupora utajiri wa
mafuta na gesi pamoja na vyanzo vingine huko kusini mwa Yemen na
kadhalika kudhibiti baadhi ya maeneo yake ya kistratijia kama vile
kisiwa cha Socotra.” Mwisho wa kunukuu.
Sababu nyingine iliyopelekea Imarati
kupata hasara kubwa nchini Yemen, ni mwendelezo wa siasa chafu za Abu
Dhabi na Riyadh katika nchi hiyo. Hata kama Saudia na Imarati zimeingia
katika tofauti kubwa baina yao kuhusiana na masuala mengi ya Yemen huku
zikipata hasara kubwa za kijeshi, lakini inaonekana kwamba Abu Dhabu na
Riyadh bado zinaendelea kushirikiana mjini Taiz. Katika uwanja huo Hamid
Rizk, mtaalamu wa masuala ya Yemen anasema: “Hivi sasa Masalafi
wa Kiwahabi walio mjini Taiz na wanaoungwa mkono na Imarati,
wanakabiliwa na mashinikizo makubwa. Kushindwa Saudia na Imarati kufikia
malengo yao katika vita dhidi ya Yemen, kumepelekea nchi mbili hizo
kufumbia macho tofauti zao kuhusiana na baadhi ya maeneo ya Yemen
ukiwemo pia mji wa Taiz na hivyo kuwawekea mipaka vibaraka wao hao.” Mwisho
wa kunukuu. Ama nukta muhimu ya kumalizia ni hii kwamba, kuendelea
kujitanua Abu Dhabi na Riyadh katika mgogoro wa Yemen, kunaweza
kuzisababishia nchi hizo hasara kubwa isiyofidika nchini humo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: