CCM YAWAFUKUZA UANACHAMA SOPHIA SIMBA NA WENZAKE KADHAA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:11 PM
Sophia Simba
NA K-VIS BLOG,DODOMA
VIGOGO kadhaa wa Chama Cha
Mapinduzi wamefukuzwa uanachama kuanzia leo Machi 11, 2017 na wengine kupewa
onyo kali kufuatia vikao viwili nyeti vya chama hicho, Kamati Kuu ya CCM, (CC)
na Halmashauri Kuu ya chama hicho, (NEC).
Kwa mujibu wa taarifa ya
maamuzi ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM iliyopatikana kwa vyombo vya habari
jioni hii, sababu za kufukuzwa uanachama
kwa wanachama hao zimeelezwa kuwa ni “makosa ya maadili kinyume na katiba na
kanuni za uongozi na maadili za CCM.
Waluofukuzwa (kuvuliwa)
uanachama ni pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM, (UWT), ambaye
pia ni Mbunge wa Viti Maalum katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sophia
Simba, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Rashid Madabida, Mwenyekiti
wa CCM, Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu, Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Mara, Christopher
Sanya, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, na Erasto Izengo Kwilasa.
Aidha taarifa hiyo imetaja
orodha ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, waliofukuzwa uanachama kuwa ni
pamoja na Ally kheri Sumaye, kutoka wilaya ya Babati Mjini, na Mathias Erasto
Manga, kutoka wilaya ya Arumeru.
Taarifa hiyo imesema, Wana
CCM wengine waliopewa onyo kali ni pamoja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM,
Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye pamoja na kupewa onyo kali anatakiwa kuomba
radhi, Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Kigoma, Josephine Genzabuke wakati Mwenyekiti
wa CCM, Mkoa wa Dodoma, Alhaji Adam Kimbisa, yeye amesamehewa.
Wajumbe wengine wa NEC
waliopewa onyo kali ni pamoja na Ali Mchumo, kutoka wilaya ya Kilwa, huku Ajili
Mchumo, mjumbe wa NEC kutoka wilaya ya Tunduru, yeye amevuliwa uongozi, Hassan
Mazala mjumbe wa nec kutoka wilaya ya Singida mjini yeye amevuliwa uongozi pia
na ndugu Valerian Allen Buretta kutoka wilaya ya Kibaha vijijini naye pia
ameachishwa uongozi.
Jesca Msambatavangu.
Christopher Sanya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: