NA MAGRETH
MAGOSSO, KIGOMA
DIWANI wa Kata ya
Mwamgongo, kilichopo mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Kigoma, Kasimu Nyamkunga ametishia kuandaa mandamano na kwenda katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Emanuel
Maganga endapo changamoto ya wajawazito kwenye Zahanati ya Mwamgongo kuendelea
kutumia tochi za simu kuzalishwa na ujenzi wa choo kilichoanguka kutopatiwa
ufumbuzi .
Akithibitisha kauli hiyo mbele ya Jamboleo wilayani humo juzi
Nyamkunga alisema wakazi wa vijiji vya mwambao mwa ziwa Tanganyika wanakabiliwa
na changamoto nyingi katika sekta ya afya, elimu, nishati ya umeme na usafiri
duni wa mitumbwi huku zahanati hiyo ikikosa hata nishati ya solar ilihali
inatoa huduma kwa zaidi ya vijiji sita.
“kitendo cha kutumia tochi ni janga kwa wajawazito, lakini
utawala hawaguswi katika hilo na hata bajeti ya mwaka huu haipo ajabu wanasisitiza
usafi lakini wamesahau zahanati hiyo haina choo kimeanguka , diwani nikisema
wanasema siasa ,wakati wataalamu ndio wanasiasa hawajui vipaumbele vya wananchi
kwa kuwa wanapenda kukaa maofisini watajuaje kero zetu”
Alisema ukosefu wa nishati ya umeme katika zahanati hiyo ni kuhatarisha
afya kwa watoa huduma na wapewa huduma na inapotokea mama mjamzito kufanyiwa
upasuaji wa dharura hakuna speed boti ya kumsafirisha katika hospitali ya rufaa
ya mkoa kwa kuwa fedha za mradi wa boti sintofahamu
.
Naye Diwani wa viti maalum Hidaya Kipwi alifafanua kuwa kuwa
changamoto ya zahanati hiyo ni vifo kwa wajawazito na wagonjwa wengine lakini wajawazito
hupata huduma ya kujifungua kwa kutumia tochi ya simu,hakuna glovu za mikono kwa wahudumu ,changamoto hiyo imejitokeza Juni 2016 hadi sasa ni tete.
Alishauri kurudishwa kwa nishati ya umeme wa solar na ujenzi
wa wodi ya upasuaji wa dharura ili kuondoa vifo vitokanavyo na uzazi
unaochangiwa na huduma finyu katika zahanati hiyo inayotoa huduma za afya kwa
vijiji sita vya mwamabo mwa ziwa Tanganyika na kumkumbusha mkurugenzi na idara
ya afya wafanyie matengenezo ya boti la zahanati hiyo ambayo gharama yake
haizidi fedha sh.milioni 4.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya kigoma Enock
Chobhaliko alishauri kutumia vyanzo vya fedha katika soko la kalinzi na
mkongoro ambayo yana uwezo wa kuingiza fedha zaidi ya milioni 3 kwa mwezi ili
kukarabati boti hilo ili kuepusha vifo
kwa wagonjwa wenye hitaji la upasuaji wa dharura.
Akijibia hilo Kaimu Mkurugenzi Shija Leylla alisema haina haja ya kuandamisha wananchi lakini atafika
katika kijiji hicho na kushuhudia uhalisia wa mambo na mwanzoni mwa wiki ya leo
solar itawekwa ili,kuepusha matumizi ya tochi za simu katika utoaji huduma kwa
wajawazito na sula la choo na boti vitashughulikiwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: