'' leo nimetembelea vituo na kuona ongezeko kubwa la waomba hifadhi ya ukimbizi,lakini maelekezo mapya yametolewa na serikali kwa kutambua sababu za msingi ili apate hifadhi, hakuna kuingia kwa makundi bali kuchunguzwa tarifa za kila mkimbizi kwa wakati wake ili kuepuka wahalifu wanaotumia fursa ya ukimbizi kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani ushirikiano katika taarifa za wahamiaji kabla ya mambo kubadilika ,ili tuchukue tahadhari kwa faida ya wote" alisema kanali Gaguti.
Akijibia hilo Mkuu wa Wilaya ya Mabanda Mkoa wa Makamba (Musitanteri) Niyonkuru Laetitia alisema kwa sasa nchi ya Burundi ni tulivu na wanaokimbia nchini mwao ni wale wanaokimbia njaa na wengine kukimbia uhalifu aliofanya nchini Burundi na kuomba hifadhi na waliorudishwa Burundi kipindi cha nyuma na wengine wanapenda kupelekwa Nje ya Nchi za Amerika na Ulaya kwa madai ya kuwafuta ndugu na jamaa zao waliopelekwa huko .
Laetitia akiri uongozi wa hapa kabla ya kuwapokea wachunguze vitambulisho vyao,ili kubaini wahalifu wanaokimbia kujibu tuhuma nchini mwao badala yake hutumia kigezo cha machafuko ilihali wanakimbia kujibu kesi za uhalifu na wengine hutumia ukimbizi ili kuongeza nguvu ya kwenda kuipindua serikali iliyopo na kuomba Tanzania iwakabidhi pindi itakapogundua hila hizo.
Nizigimana Silivesta ni Mmoja ya waomba hifadhi kutoka Burundi, alisema kinachowakimbiza Nchini mwao ni usalama mdogo hasa vikundi vya watu wahalifu huwatisha kutokana na baadhi ya ndugu zao walioikimbia nchi hiyo wanaipinga serikali husika.
0 comments: