MUFTI MKUU WA TANZANIA WA TANZANIA BAADA YA MUFTI SIMBA KUFARIKI DUNIA JULAI MWAKA 2015
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:57 PM
Mkutano mkuu wa baraza kuu la waislamu Tanzania Bakwata umempitisha
Sheikh Abubakary Zubeir kuwa mufti mkuu wa awamu ya tatu wa Tanzania
baada ya kukosa mpinzani katika kinyang’anyiro cha uchaguzi huku
akiwataka waumini wa dini hiyo kuliombea taifa amani katika kipindi hiki
cha kampeni mpaka kufanyika kwa uchaguzi mkuu na kutangazwa kwa matokeo
yake.
Sheikh Abubakary Zubeiry amechaguliwa kuwa mufti wa Tanzania baada ya
mpinzani wake Sheikh Ali Mkoyogole kujitoa dakika za mwisho kabla ya
kufanyika kwa uchaguzi kwa madai kuwa anaridhika na utendaji wa Sheikh
Zubeir ambaye awali alikuwa kaimu mufti kufuatia kufariki kwa aliyekuwa
mufti mkuu wa tanzania wa awamu ya pili Sheikh Shaaban Issa Bin Simba
Jully mwaka huu.
Muda mfupi baada ya uteuzi huyo mufti Zubeiry alipata fursa ya
kuzungumza na wajumbe wa Bakwata ambapo pamoja na mambo mengine
amewataka waumini wa dini ya kiislamu kuliombea taifa amani wakati
linakabiliwa na changamoto ya uchaguzi mkuu ujao huku akitoa wito kwa
watanzania kushiriki mchakato huo kwa utulivu ili kuilinda tunu ya amani
na upendo ambayo tanzania imekuwa ikijivunia kwa muda mrefu.
Akitoa salamu katika baraza hilo mkuu wa mkoa wa Dodoma Luteni Mstaafu
Chiku Galawa wamewataka viongozi wa dini ya kiislamu kuendelea kuhubiri
na kufundisha waumini mafunzo ya kiroho ili kudumisha amani ya nchi
lakini pia wasisahahu kusisitiza elimu dunia ili taifa na watu wake
kuondokana na utegemezi.
Kwa upande wao baadhi ya Masheikh ambao ni wajumbe wa baraza kuu la
bakwata wametoa maoni yao kuhusu mufti huyo huku pia wakizungumzia
nafasi ya waislamu katika uchaguzi mkuu ujao.
Uchaguzi wa mufti mkuu wa Tanzania awali ulikuwa na wagombea wanne ambao
ni mufti aliyechaguliwa na aliyejitoa pamoja na masheikh wengine wawili
ambao waliyeenguliwa katika kinyang’anyiro hicho na baraza la maulamaa
nchini ambao ni Sheikh Hamis Abass Mtupa na Hasan Ibrahim Kiburwa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: