SYRIA YAITAKA UN KUCHUKUA HATUA YA WAUNGAJI MKONO UGAIDI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:59 AM
Serikali ya Syria imeuandikia barua Umoja wa
Mataifa ikizungumzia ongezeko la mauaji ya kigaidi yanayofanywa dhidi ya
raia wa Damascus na vitongoji vyake na kuutaka umoja huo kuchukua hatua
dhidi ya nchi zinazoyasaidia na kuyafadhili makundi ya kigaidi.
Wizara
ya Mambo ya Nje ya Syria imetuma barua mbili kwa Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa na Mwenyekiti wa Baraza Kuu la umoja huo masaa kadhaa baada
ya makundi ya waasi yaliyoko eneo la Ghouta Mashariki kulenga mji mkuu
wa nchi hiyo na vitongoji vyake kwa maroketi ambayo yameua makumi ya
watu na kujeruhi wengine wengi.
Barua
hiyo imelaani mashambulizi hayo iliyoyataja kuwa ni jinai zinazofanywa
kila siku na magaidi hao dhidi ya raia na kusisitiza kuwa, zaidi ya
maroketi 1500 yamevurumishwa dhidi ya mji wa Damascus na viunga vyake
katika kipindi cha wiki saba zilizopita.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria imewatuhumu maafisa wa baadhi ya nchi
za Ulaya kuwa wanaunga mkono na kuwasaidia magaidi bila ya kuchukuliwa
hatua yoyote.
Mji
mkuu wa Syria umeshuhudia mashambulizi mengi katika wiki za hivi
karibuni kutoka maeneo ya karibu yanayodhibitiwa makundi vya wanamgambo
wanaoungwa mkono na kusaidiwa na baadhi ya nchi za Magharibi kama
Marekani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: