Afisa Tawala wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Joachim Asenga akiwaelekeza jinsi ya kujaza fomu watumishi wapya 57 wa Taasisi hiyo ambao wameajiriwa hivi karibuni.(PICHA NA JKCI) |
WAFANYAKAZI WAPYA WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WAPIGWA MSASA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:17 AM
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya
Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza leo na wafanyakazi wapya 57 walioajiriwa
katika Taasisi hiyo kuhusu umuhimu kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya
utumishi wa Umma.
Na
Mwandishi Maalum
WAFANYAKAZI
wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wametakiwa kufanya kazi zao kwa kufuata
maadili ya utumishi wa umma na kuepuka vitendo vya rushwa.
Rai
hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Prof. Mohamed Janabi,
wakati alipokuwa akuzungumza na
wafanyakazi wapya 57 wa kada
mbalimbali walioajiriwa hivi karibuni.
Alisema
miongoni mwa wafanyakazi hao, wapo madaktari, maafisa uuguzi, wahasibu,
maafisa Tehama, wahudumu wa afya,
wataalam wa maabara na maafisa ustawi wa jamii.
“Mtumishi
wa umma lazima ufanye kazi kwa kuzingatia maadili na sheria za kazi ikiwa ni pamoja
na kufanya kazi kwa ufanisi, weledi na kuzingatia
maadili ya taaluma yako.
“Humu
ndani ya taasisi kazi yetu inahitaji nidhamu ya hali ya juu kwa sababu
tukikosea hata kidogo maana yake tunapoteza maisha ya mtu.
“Ukipangiwa
zamu zingatia, msipokee rushwa,
kwani ni kitu hatari sana ukimuona mwenzio anajihusisha na vitendo hivyo hatua
ya kwanza ni kumkemea na kumshauri kuacha mara moja,” amesisitiza
Amewataka wafanyakazi hao kuzingatia kuvaa mavazi
yenye staha wakati wote hususan wale ambao watakuwa hawavai sare maalum za
kazi.
“Hakikisheni mnawahi kazini, kama unaishi mbali
jitahidi kuwahi mapema kutekeleza majukumu yenu,” amewasihi.
Prof
Janabi hakusita kuwaeleza wafanyakazi hao baadhi ya changamoto zinazoikabili
taasisi hiyo ikiwamo ufinyu wa nafasi.
“Ofisi
tulizonazo ni chache, kwa kuanzia tutashirikiana hivyo hivyo hasa wale ambao si
wataalamu wa afya,” amesema.
Kwa
upande wake Mkuu wa Idara ya Rasilimali Watu wa Taasisi hiyo, Ghati Chacha alisema
kati ya wafanyakazi walioajiriwa 23 ni wanaume na 29 ni wanawake.
“Wameajiriwa
JKCI baada ya kupatiwa kibali na Serikali kulikuwa na nafasi 57 zilizojazwa ni
56 na hadi sasa walioripoti kazini ni 52, wanne wameomba udhuru kwani wana
dharura na hadi kufikia wiki ijayo tunatarajia nao watakuwa wameripoti kazini,”
amesema.
Baadhi
ya Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na vitengo vya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)
wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi (hayupi
pichani) wakati akinzungumza na wafanyakazi wapya 57 walioajiriwa katika
Taasisi hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: