JESHI LA POLISI MOROGORO LATOWA SABABU KWA KUKAMATWA NAY WA MITEGO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:53 PM
Kamishna
Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro, Kamanda Ulrich
Matei amethibitisha kukamatwa kwa msanii Nay wa Mitego usiku wa kuamkia jana mkoani Morogoro.
Kamanda
Ulrich Matei ametoa sababu kubwa ya kukamatwa kwa msanii huyo ni
kutokana na kutoa wimbo unaofahamika kwa jina la 'Wapo' ambao anadai
unaikashfu Serikali iliyopo maradakani.
Kamanda
Matei amesema shauri la Nay wa Mitego lipo jijini Dar es Salaam hivyo
msanii huyo atasafirishwa na kupelekwa Dar es Salaam kuhojiwa kwa Mkuu
wa Upelelezi wa mkoa.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: