YANGA YAVUNJA REKODI YA MIAKA 30, WASHINDA 1-0 UWANJA WA MAJIMAJI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:32 PM
Uwanja wa
Majimaji Songea taswira ya ndani kabla ya mtanange kuanza kati ya
Majimaji dhidi ya Yanga uliomalizika kwa Yanga kupata ushindi wa goli
1-0.Ripota wa Globu, Songe
MABINGWA
watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara wametoka na ushindi wa goli 1-0 dhidi
ya Majimaji mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Majimaji Songea na
kufikisha alama 43 wakiwa nyuma ya alama moja ya mahasimu wao Simba.
Mtanange
huo ulioanza majira ya saa 10 kamili ilichukua dakika 15 kwa Deus Kaseke
kuwainua mashabiki wa Yanga baada ya kumalizia krosi ya Haruna
Niyonzima iliyopanguliwa na golikipa na kumkuta miguuni na kuachia shuti
kali akiwa nje ya 18.
Yanga
walionekana kutawala sehemu ya kiungo na kuweza kucheza mpira zaidi ya
Majimaji lakini umakini wa safu ya ushambuliaji ilishindwa kuwa makini
na kumalizia mipira ya mwisho iliyokuwa ikitengwa na Juma Abdul pamoja
na Haruna Niyonzima.
Katika
historia ya Majimaji na Yanga katikia Uwanja huo imeweza kuvunjwa leo
baada ya miaka 30 kupita bila wanajangwani hao kuondoka na ushindi huku
msimu uliopita wakiambulia sare.
Kali
Ongala alionekana kutumia zaidi vijana katika mchezo huu dhidi ya Yanga
lakini walishindwa kuonyesha umahiri wao, na ameweka wazi kuwa bado
ataendelea kuwaamini vijana hao kwani ana imani watakuja kuwa wachezaji
wa kutumainiwa hapo baadae.
Huu ni
mchezo wa kwanza wa ligi kuu kwa Kocha Mkuu wa Yanga George Lwandamina
kucheza ugenini na ameweza kuondoka na alama tatu muhimu ambapo zina
faida kwake huku wakiangalia mechi ya kesho baina ya Mtibwa na Simba
utakaopigwa uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Kwenye
mechi hiyo kulitokea vioja vya aina yake kwa Timu ya Yanga kushindwa
kuingia vyumbani na kubadilishia nguo pembeni ya Uwanja.
Kabla ya
kuanza kwa mchezo huo wakati timu ya Yanga wamewasili wakiwa wamekaa
kwenye mabenchi na hawakuingia vyumba vya kubadilishia nguo.
Wakati wa
mapumziko timu ya Yanga wakiwa wanapata maelekezo kutoka kwa benchi la
ufundi wakiwa hawajaingia ndani ya vyumba vya Uwanja.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: