BIDHAA YA NAFAKA SOKO LA MWANGA ,,, YAPANDA BEI KIGOMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:42 PM
NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA
WAFANYABIASHARA wa Bidhaa ya Mahindi,Unga na
Mchele Soko la Mwanga Manispaa ya Kigoma Mjini Mkoa wa Kigoma inazidi kupanda bei mwezi hadi mwezi mkoani
Kigoma, hali inayochangiwa na ukosefu wa ghala la Chakula sanajari na uboreshaji
wa miundombinu ya barabara hasa
Kigoma -Mpanda iwekewe lami ili
kuondoa gharama za kupanda kwa bidhaa
hizo.
Akizungumza na mwandishi wetu, mmiliki wa mashine za kusaga nafaka
Jiti Rubibi alisema mwanzoni mwa mwezi Septemba debe moja la mahindi ni
sh.11,000 sawa na sh.66 kwa gunia moja kwa mahindi yanayotoka
wilayani kasulu na uvinza lakini
mwanzoni mwa mwezi huu debe moja kwa bei
ya jumla hulangua kwa sh.13 sawa na sh.78
kwa gunia moja .
Alisema sababu kubwa ni
kukosekana kwa ghala la chakula mkoani humo, ambapo serikali ingedhibiti uzwaji
wa nafaka hizo na kipindi hiki cha kuadimika kwa nafaka hizo ghala ingepunguza
ukali wa bei ya bidhaa hiyo sambamba na kuboreshwa kwa barabara ya kigoma
kwenda mpanda ambako wafanyabishara huagiza katika ghala la chakula mkoani
humo.
Kwa upande wa muuza mahindi
Matilda Salehe na muuza unga Khadija Lucas kwa nyakatio tofauti wakiri mahindi
kupanda bei kwa kuwa awali walikuwa wakinunua gunia kwa sh.65 na debe
wakilangua kwa sh.12,000 kwa kipindi cha mwezi uliopita,lakini sasa wanalangua
debe moja kwa sh.78,000 mahindi ya kutoka mpanda.
Khadija alisema kutokana na hilo
huwauzia wateja wanaofika katika mashine za kusaga nafaka kilo moja kwa sh.1,000
na wanaokwenda kuuza maduka ya mitaani
huwauzia wateja kilo moja kwa sh.1200 na wengine 1100 kulingana na gharama za
usafiri wa kufikisha eneo husika na kuiomba serikali iboreshe miundombinu ya
barabara ili kupunguza gharama za uingizaji wa nafaka hizo.
Naye muuzaji wa bidhaa ya mchele
Soko la Mwanga Manispaa ya kigoma Ujiji Fedirick Emanuel alisema awali walikuwa
wakiuza kilo moja ya mchele kwa sh.1000 hadi sh.1,200 na gunia moja walikuwa wakilangua mkwa
sh.120,000 lakini kuanzia mwanzoni mwa mwezi huu gunia moja la mchele
wanalangua kwa sh.130,000 ambapo huwauzia wateja kilo moja kwa sh.1400 hadi
1500 kwa mchele msafi.
Emanuel alisema kwa mchele
unaolimwa mkoani kigoma kata ya kalya
wilaya ya Uvinza wakulima wanapeleka bidhaa hiyo nchini DRC-Congo na hulazimika
kulangua mkoani mpanda hali mbaya ya
barabara inachangia kuongezeka kwa gharama za usafirishaji hivyo hawana budi kufidia hilo kwa mlaji.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: