“Alitufunga kamba miguuni na mikononi na kuanza kututesa kwa kutupiga na baada ya kuona hatusemi ndipo alipochukua makaratasi ya naironi na kutufunga miguuni kisha kuchukua kiberiti ,mafuta ya taa na kuwasha moto katika miguu yetu huku akiendelea kutupiga na moto ukiwaka miguuni….wakati huo mama alikuwa amekaa mlangoni akishangilia kuwa wapige sana mimi nimewachoka hawa watoto heri wafe tu” walisema watoto hao
UKATILI!! Baba awachoma moto watoto wake wawili huku Mama Akishangilia..!!
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:27 AM
WAKATI wanaharakati mbali mbali
wakiwemo wanaharakati wa mtandao wa kijinsia Tanzania
(TGNP) ,wanaharakati wa haki za binadam,WAMA kuendelea kukemea na
kuendelea kupinga vikali vitendo vya ukatili wa kijinsia na uyanyasaji
wa wanawake na watoto hata kulifanya jeshi la jeshi
la polisi kuanzisha dawati maalum linaloshughulikia vitendo vya
unyanyasaji wa kijinsia ,baba wa kambo Mussa Mdetela aamua kuwatesa
kinyama watoto wake kwa kuwachoma moto miguu wakituhumiwa kuiba Tsh
10,000
Wakizungumza kwa shida na
mtandao huu watoto hao Baraka Rajab Mohamed anayesoma darasa la kwanza
na Mood Rajab Mohamed anayesoma darasa la sita walisema
kuwa ilikuwa ni siku ya tarehe 3 ambapo walichukua pesa hiyo kiasi cha
Tsh 10,000 na kwenda kununua chakula baada ya mama yao kushindwa
kuwaandalia chakula.
Hata hivyo Mood anayesoma darasa la
sita msingi Lugalo alisema kuwa siku ya tukio mdogo wake alikwenda
ndani na kuchukua kiasi hicho cha fedha na baada ya
muda walishirikiana katika matumizi .
Watoto hao ambao wanadai kuwa
baba yao mzazi Rajab Mohamed aliwaacha na sasa anaishi jijini Dar es
Salaam na wao wamekuwa wakiishi na baba yao mdogo huyo ambae mara kwa
mara amekuwa akiwaadhibu vikali.
Kwani walisema kuwa kutokana na
mara kwa mara kushinda bila kula ndipo siku hiyo walipoamua kuchukua
pesa hiyo ili kununua bagia na vitumbua ili kujikimu kwa njaa .
Hivi ndivyo watoto hao walivyougunzwa kinyama na baba wa kambo
Mrakibu mwandamizi wa polisi na
mkuu wa dawati la jinsia na watoto mkoa wa Iringa ,Atupele Mwambunda
akiwatazama watoto hao nje ya ofisi ya dawati la jinsia mkoa wa
Iringa
Mama wa watoto hao Watende Sanga akiendelea kupika chakula baada ya watoto kuchukuliwa na polisi
Askari wa dawati la jinsia Iringa
akiingia kumsimamia mama wa watoto hao kufunga duka lake kabla ya
kuchukuliwa kwenda polisi
Hata hivyo walisema baada ya baba
yao kurudi kutoka katika shughuli zake na kubaini kuwa fedha hiyo
imechukuliwa ndipo alipowakamata na kuwafunga kamba na kuanza kuwatesa
kwa kichapo ili waweze kusema mtu aliyechukua pesa hiyo.
Atupele Mwambunda mkuu wa dawati la
jinsia mkoa wa Iringa ameuthibitishia mtandao huu juu ya tukio hilo
na kuwa kitendo hicho ni cha kinyama na kamwe hakitavumilika.
Alisema kuwa kuanzishwa kwa dawati
hilo ni kutaka kukomesha vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia
kama hivyo na kuwataka wazazi na jamii kuepuka kuchukua sheria mkononi
kwa kuwatesa watoto kama hao ambao mwisho wa siku wanapoteza
mwelekeo wa maisha.
Mwambunda alisema kuwa hadi sasa
wamefanikiwa kumkamata mama wa watoto hao Watende Sanga
huku mzazi mwenzake Mussa Mdetele bado anatafutwa na jeshi la polisi
ili kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kuwatesa watoto hao.
Huku mama wa watoto
hao akidai kuwa wakati baba yao mdogo akiwapiga watoto hao yeye
hakujua kinachotokea japo alikuwa na taarifa ya kupotea kwa pesa
katika duka na kuwa baada ya tukio hilo aliwanunulia dawa ili
kuwatibu kinyemela pamoja na kuwaombea ruhusa shuleni .
Pia mwanamke huyo aliomba kusamehewa kwa madai kuwa hakujua kama kushangilia wakati baba yao akiwatesa watoto hao ni kosa
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: