DOLA MILIONI 68 KUGHARAMIA MAPOKEZI YA TRUMP

Kufuatia kuvuja barua ya siri ambayo Mfalme Salman wa Saudi Arabia ameiandikia Wizara ya Fedha ya nchi hiyo, imebainika kuwa utawala huo wa kifalme utatumia dola milioni 68 kwa ajili ya kugharamia mapokezi ya Rais Donald Trump wa Marekani anayetazamiwa kuitembelea nchi hiyo mwishoni mwa mwezi huu.
Sambamba na kukaribia safari ya Trump nchini Saudia, waraka wa siri unaotoka Baraza la Ufalme wa nchi hiyo na unaosisitiza kuchukuliwa hatua za haraka umesambazwa katika mitandao ya kijamii ukionyesha gharama za fedha zitakazotumika kwa ajili ya kumlaki rais huyo wa Marekani.
Rais wa Marekani, Trump (kushoto) na Mfalme Salman wa Saudia
Kwa mujibu wa waraka huo, ofisi ya Mfalme Salman bin Abdulaziz Aal Saud imeiandikia barua Wizara ya Fedha kuitaka ifanye maandalizi yanayohitajika kwa ajili ya kumlaki rais wa Marekani na pia kuitaka iafiki kuidhinisha bajeti ya mapokezi ya dola milioni 68 kwa ajili kugharamia kikao cha pamoja baina ya Waarabu na Marekani.
Rais wa Marekani, Trump akimlaki Waziri wa Ulinzi wa Saudia Muhammad Salman, Ikulu ya White House
Trump anatazamiwa kufanya safari nchini Saudi Arabia mwishoni mwa mwezi huu wa Mei. Duru za kuamimika zimeripoti kuwa lengo kuu la safari hiyo ya rais wa Marekani ni kufunga mikataba ya kuiuzia Saudia silaha zenye thamani ya makumi ya mabilioni ya dola.
Hii ni katika hali ambayo kutokana na kushuka bei ya mafuta, gharama za vita dhidi ya Yemen na kuyasaidia kifedha makundi ya kigaidi katika eneo uchumi wa Saudia umezorota ambapo idadi ya watu wasio na ajira nchini humo imefika watu milioni 27 ikiwa ni zaidi ya asilimia 11.
Idadi ya raia masikini nchini Saudia imekuwa ikiongezeka
Aidha kutokana na kuanzisha vita dhidi ya Yemen na kukoleza moto wa vita katika nchi nyengine za eneo la Mashariki ya Kati, Saudi Arabia ni nchi ya tatu inayonunua silaha kwa wingi duniani huku asilimia 99 ya silaha za nchi hiyo ikiwa inaagizwa kutoka nje.../

0 comments: