Waziri wa habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe akimsikiliza kulia Msanii wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa aka Roma Mkatoliki akifafanua jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jioni hii wakati akizungumzia sakata la kutekwa kwake paoja na wasanii wenzake katika studio ya Tongwe iliyopo Masaki jijini Dar es salaam |
TULIFUNGWA VITAMBAA USONI NA PINGU MIKONONI: ROMA MKATOLIKI AZUNGUMZIA MACHUNGU WALIYOWAKUTA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:06 PM
MSANII wa muziki wa kizazi kipya,
Ibrahim Mussa, maarufu kama Roma Mkatoliki, amewaambia waandishi wa
habari waliofurika kwenye ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dar
es Saam leo Aprili 10, 2017 kuwa yeye na wenzake walitekwa na kufungwa
vitambaa usoni na kufungwa pingu kula vipigo, kabla ya kutupwa ufukweni
mwa bahari jijini Jumamosi "Tulipokuwepo si pazuri, tuliteswa na
kupigwa tulipiga alama ya msalaba na wenzetu wenye imani nyingine
waliomba kwa dini zao." Alisema Roma, ambaye alikuwa na mkewe na Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, wenzake
watatu aliotekwa nao pamoja na uongozi wa studio za Tongwe Records. Kwa
upande wake, waziri Mwakyembe amewahakikishia watanzania kuwa watulifu
na kwamba."
Lazima
upelelezi kamilifu ufanyike tujue nini kimefanyika vinginevyo vitendo hivi
vitaemdelea.” Alisema Dkt. Harrison Mwakyembe
Roma Mkatoliki akifafanua zaidi kwa waandishi wa Habari
Roma
akiwaonesha wana habari namna alivyojeruhiwa aliokuwa akiteswa na hao
watekaji ambao mpaka sasa hawajajulikana ni akina nani,kufuatia
Uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
Waziri
wa habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe
akimsikiliza kulia Msanii wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa
aka Roma Mkatoliki akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa
Idara ya Habari Maelezo jioni hii wakati akizungumzia sakata la kutekwa
kwake paoja na wasanii wenzake katika studio ya Tongwe iliyopo Masaki
jijini Dar es salaam, Roma ameiomba serikali kuwahakikishia ulinzi
wasanii pamoja na watanzania kwa ujula kwakuwa inaoyesha hawana usalama
kabisa kutokana na tukio lenyewe lilivyowatokea. Kushoto ni Mke wa wa
Msanii huyo, Bi Nancy.
Baadhi
ya Wana Habari wakimsubiri msanii wa Muziki wa Kizazi kipya ajulikanae
kwa jina la Roma Mkatoliki kuja kuzungumza nao na kuwaeleza
kilichowatokea
Baadhi ya Wana habari wakifuatilia tukio hilo
Waziri
wa habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe
akimsikiliza kulia Msanii wa bongo Fleva kutoka Tanzania Ibrahim Musa
aka Roma Mkatoliki akifafanua jambo wakati akizungumza na waandishi wa
habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jioni hii wakati
akizungumzia sakata la kutekwa kwake paoja na wasanii wenzake katika
studio ya Tongwe iliyopo Masaki jijini Dar es salaam
Mke
wa Roma Mkatoliki Nancy (mwenye kilemba cha bluu) pamoja na baadhi ya
wasanii wakisubiri kuanza kwa mkutano huo wakati Msanii huyo akijiandaa
kuzungumza na waandishi wa habari kuhusu sakata la kutekwa kwake kulia
ni Waziri wa Habari , Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson
Mwakyembe.
Waziri
wa habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dk. Harisson Mwakyembe
akiongozana na wasanii Roma Mkatoliki na wenzake ili kuzungumzia sakata
la Roma Mkatoliki lililotokea hivi karibuni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: