KIPLAGAT, KIRUI WASHINDA MBIO ZA MARATHON BOSTON


Edna Kiplagat na Geoffrey Kirui baada ya ushindi wao huko Boston.
Mkimbiaji maarufu Edna Kiplagat kutoka Kenya ametwaa ushindi (mbio za wanawake) kwa kuongoza mashindano ya marathon ya 121 huko Boston, Marekani. Kwa upande wake Geoffrey Kirui ambaye pia ni Mkenya ameshinda mbio za upande wa wanaume.
Kwa mujibu wa mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili VOA Kiplagat ambaye ni afisa wa jeshi la polisi la Kenya alianza mbio hizo kwa kuwaacha wapinzani wake nyuma sana.

Hata hivyo wakati anaelekea katika milima ya Newton akaongeza kasi kufikia ushindi katika muda (usio rasmi) wa masaa 2, dakika 21, sekunde 53 katika mbio hizo za 121, siku ya Jumatatu April 17, 2017.

Ni mara ya kwanza Kiplagat, ambaye ni mshindi wa kimataifa kwa mara mbili ameshiriki katika mbio hizo za Boston.
Mshindi huyu amewahi kushinda London, New York City na Los Angeles.

Kwa upande wa mbio za wanaume, Mkenya Geoffrey Kirui ameshinda mbio za Marathon katika mashindano haya kwa mara ya kwanza.

Kirui alimshinda mpinzani wake Galen Rupp wa Marekani na kunyakua ubingwa huo wa mbio hizo za 121 katika muda usio rasmi wa masaa 2, dakika 9 na sekunde 36. Hata hivyo alikuwa mshindi mwaka jana katika mbio za marathon za Amsterdam na watatu katika mbio za Rotterdam. Rupp alimaliza mbio hizo kwa muda usio rasmi wa masaa 2, dakika 9 na sekunde 58.

Katika mbio hizo za wanawake Chelimo wa Bahrain alichukua nafasi ya pili, akiwa nyuma kwa dakika 59 na Jordan Hasay wa Marekani ametwaa nafasi ya tatu katika uzinduzi wa mashindano hayo ya Marathon.

Desi Linden, ambaye alitwaa ushindi wa pili huko Boston kwa tofauti ya dakika mbili mwaka 2011, alimaliza akiwa mshindi wanne—kwa mara ya kwanza tangu 1991ambapo wanawake wawili wa Kimarekani kumaliza katika wanne bora.

0 comments: