WAZIRI WA AFYA JENISTA MHAGAMA AFANYA ZIARA LEO TAASISI YA MOYO (JKCI)

 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete akimkaribisha Mhe. Waziri wa Afya . Jenista Mhagama mara alipowasili katika Taasisihiyo wakati wa ziara yake iliyofanyika leo 11, Septemba 2024.

  Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA na TAKWIMU Taasisi ya Moyo JKCI. Lazaro Swai (wa pili kulia) akimpatia maelezo Mhe. Jenista Mhagama juu ya mfumo wa Kiongozi foleni ambao upande mmoja una lengo la kuongoza foleni ya watu wanaokuja kusalimia wagonjwa wao upande wa pili ni kuongoza foleni ya wagonjwa wanaokuja kupatiwa matibabu 
  Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama akimsikiliza Mtoto Ally Mwandu aliefanyiwa upasuaji Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete wakati akikabidhiwa UA mara alipofanya ziara katika Taasisi hiyo leo 11,Septemba 2024.
Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama  akizungumza na baadhi ya ndugu wa wagonjwa mara alipofanya ziara ya kutembelea Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete leo Septemba 11, 2024 

Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama akisaini kitabu cha wageni mara alipofanya ziara ya kuitembelea Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete leo Septemba 11, 2024 Jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi Mtendaji akimkabidhi zawadi Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama leo wakati alipofanya ziara katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

  Mhe. Waziri wa Afya Jenista Mhagama akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete leo Jijini Dar es Salaam.

0 comments: