LIGI YA MABINGWA ULAYA JUVENTUS WAICHAPA MONACO BAO 2

Historia wakati mwingine huwa ina umuhimu sana katika maisha ya soka, usiku wa Mei 3, 2017 katika uwanja wa unaotumiwa na AS Monaco kama uwanja wa nyumbani Monaco waliikaribisha Juventus kucheza mchezo wao wa kwanza wa nusu fainali ya pili ya UEFA Champions League msimu wa 2016/2017.
Mchezo wa nusu fainali ya pili ya kati ya Juventus dhidi ya Monaco kivutio kilikuwa ni golikipa wa Juventus Buffon na mshambuliaji wa Monaco Mbappe ambaye ameonesha umahiri mkubwa katika michuano hiyo kwa siku za karibuni, Mbappe amezaliwa mwaka 1998 alikuwa anajitahidi kumfunga Buffon ambaye mwaka anaozaliwa Buffon alikuwa anacheza World Cup yake ya kwanza.
Buffon amefanikiwa kumdhibiti Mbappe ambaye ameonesha makali lakini Buffon pia hajawahi kufungwa goli na Lionel Messi ambaye ni moja kati ya wachezaji bora wa muda wote wa kizazi cha sasa, hata hivyo Juventus wamefanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0 katika mchezo huo wa kwanza, magoli yamefungwa na Gonzalo Higuan dakika ya 29 na 59.

0 comments: