WAZAYUNI WAKIVAMIA TENA KIBLA CHA KWANZA CHA WAISLAMU

Karibu walowezi 50 wa Kizayuni leo Alkhamisi wamekivamia tena Kibla cha Kwanza cha Waislamu yaani Masjidul Aqswa na kuuvujia heshima msikiti huo mtakatifu kwa ulinzi kamili wa polisi wa Israel.
Kituo cha Upashaji Habari cha Palestina kimeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, walowezi Wazayuni wameuvamia Msikiti wa al Aqsa kwa mara kadhaa katika kipindi cha wiki moja iliyopita na kuwashambulia walinzi wa eneo hilo takatifu.
Kwa mujibu wa kituo hicho cha habari, vitendo vya walowezi wa Kizayuni vya kuvamia Kibla cha Kwanza cha Waislamu vinazidi kuongezeka.
Mwezi Machi mwaka huu. walowezi 1,782 wa Kizayuni waliuvamia Msikiti wa al Aqsa na kuuvunjia heshima msikiti huo mtakatifu ikiwa ni ongezeko la takriban mara mbili ikilinganishwa na mwezi Machi mwaka jana ambapo walowezi 960 walilivamia eneo hilo tukufu.
Masjidul Aqswa, Kibla cha Kwanza cha Waislamu

Mwezi Machi mwaka huu pia, taasisi zenye misimamo mikali za Kiyahudi zilitoa mwito mara kadhaa wa kuvamiwa na Wazayuni, Kibla cha Kwanza cha Waislamu.
Masjidul Aqswa imegeuzwa kuwa eneo la kuonesha jeuri za wanajeshi wa Israel na walowezi wa Kizayuni wenye nia ya kuupokonya msikiti huo sura na utambulisho wake wa Kiislamu.
Kuwepo msikiti huo mtakatifu na maeneo mengine matukufu kwa Waislamu na Wakristo, kunaufanya mji wa Baytul Muqaddas huko Palestina kuwa eneo takatifu kwa wafuasi wa dini hizo mbili.
Hata hivyo utawala wa Kizayuni wa Israel unafanya njama za kila namna za kuuyahudisha mji huo na kuupokonya kabisa sura yake ya Kiislamu na pia ya Kikristo.

0 comments: