JESHI LA YEMEN LAENDELEA KUPATA MAFANIKIO DHIDI YA VIBARAKAWA SAUDIA

Askari wa serikali ya Yemen kwa kushirikiana na Harakati ya Wananchi ya Answarullah limeendelea kupata mafanikio katika operesheni kadhaa lilizozifanya katika mikoa ya Lahij, Dhale na Taiz na kufanikiwa kuwaangamiza askari wengi vibaraka wa Saudia sambamba na kuwatia hasara kubwa.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la Yemen imesema kuwa, askari wa serikali na harakati hiyo ya Answarullah, wameweza kuwazuia askari vamizi wa Saudia na waungaji mkono wao kuelekea mji wa Kirsh mkoa wa Lahij, kusini mwa Yemen ambapo kumejiri mapigano makali yaliyowafanya askari wa Saudia kurudi nyuma na kukimbia.
Baadhi ya askari wa Saudia walioangamizwa na jeshi la Yemen
Hii ni katika hali ambayo kikosi cha mizinga cha jeshi na harakati ya Answarullah kilichopewa jina la 'al-Swaderain' kimelilenga eneo la 'Maris' la mkoa wa Dhale, kusini mwa nchi ambapo kumewekwa kambi ya jeshi la askari wa Saudia na kufanikiwa kuangamiza baadhi yao. Kadhalika magari kadhaa ya kijeshi ya Saudia yaliyokuwa yamewabeba askari wa nchi hiyo vamizi wameangamizwa huko magharibi mwa mkoa wa Taiz. Makumi ya askari wa Saudia na vibaraka wake wameangamizwa katika siku za hivi karibuni katika maeneo tofauti ndani na nje ya Yemen na hivyo kuitia hasara kubwa Saudi Arabia na washirika wake.
Baadhi ya magari na vifaru vya jeshi la Saudia vilivyoharibiwa na jeshi la Yemen
Wakati huo huo duru za kuaminika zimeripoti kuibuka mapigano makali baina ya askari wanaomuunga mkono Abdrabbuh Mansur Hadi, rais wa zamani wa Yemen aliyejiuzulu na kutoroka nchi. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mapigano hayo yametokea huko mkoa wa Aden, baada ya kundi moja kati ya askari hao kutaka kudhibiti kituo cha upekuzi mkoani hapo.

0 comments: