Msemaji wa jeshi la polisi katika jimbo la North Rhine Westphalia, Gunnar Wortmann, aliliambia shirika la habari la Associated Press, "Basi lilianza safari kutoka hoteli ya timu ya Dortmund wakati milipuko mitatu ilipotokea. Milipuko mitatu ilitokea karibu na basi hilo lilipokuwa njiani kuelekea uwanjani na kwamba mchezaji mmoja amejeruhiwa na dirisha moja kuharibiwa."
Beki wa Dortmund ajeruhiwa
Gazeti la Ujerumani la Bild limeripoti kwamba beki wa Borussia Doetmund Marc Bartra amejeruhiwa na kupelekwa hospitali. Klabu ya Dortmund imetuma taarifa katika mtandao wa kijamii wa Twitter ikisema mchezaji huyo yuko salama na hakuna kitisho chochote ndani na nje ya uwanja wa Signal Iduna Park.
Mkurugenzi wa klabu ya Dortmund, Hans-Joachim Watzke, alithibitisha kujeruhiwa kwa Bartra, akisema ameumia mkononi na kuwa majeruhi si hatari kwa maisha yake.
Msemaji wa polisi ya Dortmund, Nina Vogt, alisema wachunguzi bado hawafahamu chanzo cha milipuko iliyotokea wakati timu ya Borussia Dortmund ilipokuwa ikijiandaa kuondoka hotelini kuelekea uwanjani kuchuana na Monaco. Polisi imesema inalichukulia tukio hilo kuwa shambulizi. Hata hivyo hakuna dalili kuonyesha ni shambulizi la kigaidi.
0 comments: