Waziri Mkuu Majaliwa (katikati), akiwa na Waziri wa nchi (TAMISEMI) na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky SADICK.
WAZIRI MKUU MAJALIWA AKATAA VIWANGO VYA NAULI ZA MABASI YA MWENDO KASI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:06 AM
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na waandishi wa habari
kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar
es salaam, alipowasili kutoka mkoani Ruvuma alikokuwa kwenye ziara ya
kikazi. Kubwa alilosema, Majaliwa ni kuzikataa nauli zilizopendekezwa
za mabasi yaendayo kasi, Majaliwa aliwaambia waandishi wa habari
kuwa, viwango hivyo vya shilingi 1,200 na 1,400 huku wanafunzi wakilipa
nusu ya viwango hivyo, ni vikubwa mno kwa Mwananchi wa kawaida na
haikuwa lengo la mradi huko Ameitaka Tamisemi na wizara ya uchukuzi kwa
kushirikiana na waendeshaji wa mradi huko wakajipange upya na
wakishindwa serikali itauendesha mradi huko.
Waziri Mkuu Majaliwa (katikati), akiwa na Waziri wa nchi (TAMISEMI) na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky SADICK.
Waziri Mkuu Majaliwa (katikati), akiwa na Waziri wa nchi (TAMISEMI) na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky SADICK.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: