MRISHO NGASSA NAYE ATUA KAMBINI STARS, AANZA KUJIWINDA DHIDI YA ALGERIA

 mr1
Na Mwandishi Wetu, Johannesburg
Kwa hisani ya http://www.salehjembe.blogspot.com/
Kiungo Mshambuliaji wa Free State Stars, Mrisho Ngassa naye amejiunga na kikosi cha Taifa Stars kilicho mazoezini jijini Johannesburg.
Ngassa alichelewa kujiunga na kambi hiyo kwa kuwa alikuwa akiichezea timu yake katika mechi ya Ligi Kuu frika Kusini.
Ngassa amejiunga na wenzake na mara moja ameanza mazoezi akiwa na kikosi cha Stars kinachojiandaa kucheza na Algeria
Stars itaivaa Algeria kuwania kucheza Kombe la Dunia katika mechi inayotarajiwa kuwa ngumu.

0 comments: