SERIKALI HAINA BUDI KUWEKA SERA NZURI NA KUDUMISHA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Kamati Maalum kuhusu Kutathmini hali ya Utendaji na Uchumi kwenye Vyombo vya Habari Tanzania Bara kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwandishi Mbobevu Tido Mhando wakati wa Kongamano la Pili la Maendeleo ya Sekta ya Habari katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam tarehe 18 Juni, 2024.
Samia Suluhu Hassan amesema vyombo vya habari si adui wa serikali bali ni mdau muhimu, hivyo Serikali haina budi kuweka sera nzuri na kudumisha uhuru wa vyombo vya habari.

Samia amesema vyombo vya habari vikiwa huru vinagusa kila pembe ya jamii kwa kuelemisha , kufichua maovu , kuchangia maendeleo ya kijamii na kukuza demokrasia.

Amesema hayo leo Juni 18,2024 jijini Dar es salaam kwenye kongamano la sekta ya habari na kusema kuwa habari za kiuchambuzi kwenye vyombo vya habari ni chache, hivyo waandishi watilie mkazo kwenye uchambuzi na wajielekeze kwenye habari zinazokubalika

Amesema zama zinabadilika waandishi lazima waendane na mabadiliko yaliyopo ya kiteknolojia na watumie uwezo wao wa taaluma vizuri.

Naye Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, amesema Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mageuzi makubwa kwenye sekta ya habari na Tanzania imekuwa kinara Afrika Mashariki kwa uhuru wa vyombo vya habari.   

0 comments: