Kaimu Mkurugenzi Mkuu CPA Anthony
Kasore akizungumza na waandishi katika moja ya banda katika Maonesho ya
47 ya Biashara Kimataifa Dar es Salaam yanayoendelea katika viwanja vya
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Sabasaba Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Picha ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA katika Mabanda ya VETA.
*Serikali imewekeza nguvu ya kutosha katika kuwafikia watanzania
Na Mwandishi wetu TV
MAMLAKA
ya Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA) imesema vijana wa kitanzania
itumie fursa ya mafunzo ya ufundi stadi kutokana na kuwepo kwa ajira
katika mapinduzi ya viwanda nchini.
Hayo
ameyasema Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore wakati
akizungumza na waandishi wa habari katika Banda la VETA kwenye maonesho
47 ya Biashara Kimataifa Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika
viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Sabasaba Jijini Dar es
Salaam.
Kasore
amesema kuwa serikali imewekeza nguvu katika ujenzi wa vyuo mafunzo ya
ufundi stadi katika kuhakikisha vijana wanapata ujuzi wa kuweza
kuajiriwa na kujiajiri pasipo kuwepo kwa changamoto.
Amesema VETA inatarajia kujenga vyuo 64 ikiwemo kimoja cha Mkoa wa Songwe na vingine vyote vya wilaya.
Aidha
amesema Serikali ya awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan iko bega
kwa bega na VETA katika kuwapatia vijana ujuzi waweze kutengeneza ajira
na maendeleo kwa ujumla.
Kasore
amesema kuwa katika utoaji wa mafunzo kumekuwa na ubunifu ambapo
wabunifu walimu na wanafunzi kazi ya VETA ni kuwashika mkono kwa kuwa
na miliki ili watu wengine wasije wakazifanyia biashara.
Kasore
amesema kuwa wenye viwanda na wawekezaji wasipate changamoto ya nguvu
kazi kutokana na nguvu kazi hiyo imeshazalishwa na VETA.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu amesesma VETA inashirikiana na Costech katika
kuhakikisha wabunifu wanakuwa wanatambuliwa na kuweza bunifu hizo kwenda
mbali zaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)





0 comments: