MKURUGENZI MTENDAJI AFUNGA SEMINA YA UJASILIAMALI KWA WANACHAMA WA TUGHE MOI

  Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface (kushoto) akizungumza na wanachama wa Tughe Tawi la Taasisi hiyo wakati alipokuwa akifunga semina ya ujasiliamali iliyoandaliwa na Chama Cha Wafanyakazi Tawi la Taasisi hiyo, Dkt.  Boniface aliwashukuru waandaaji na watoa mada wote kwa kuwapatia elimu hiyo na kuwaomba washiriki kuyashika yale waliyofundishwa na kuyaendeleza .(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 Katibu wa Tughe Mkoa wa Iringa, Shadrack Mkodo (kulia) akizungumza Wakatialipokuwa akitowa mada ya ujasiliamali kabla ya kufungwa na Mkurugenzi wa taasisi ya (MOI) iliyofanyika Dar es Salaam jana
 Washiriki wakisikiliza kwa umakini
   Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface (wa tatu kulia) akiandika jambo wakati Katibu wa Tughe Mkoa wa Iringa, Shadrack Mkodo (pichani hayupo) alipokuwa akitowa mada katika Ukumbi wa Taasisi hiyo.
 Washiriki
 Mwenyekiti wa Tawi la Tughe (MOI), Privatus Masula (kushoto) akizungumza jambo kabla ya kufungwa semina hiyo na    Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Dkt. Respicious Boniface (wa tatu kushoto waliyokaa)
 Mwenyekiti wa Tawi la Tughe (MOI), Privatus Masula, akizungumza na wandishi wa habari alisema, anapenda kumshukuru Mungu na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo kwa kukubali kuwa Mgeni rami na kuwashukuru viongozo wote waliyowezesha kufanikisha kufanyika kwa semina hiyo ya ujasilia mali kwa wanachama wa Tawi la Tughe (MOI), Masula alisema.

Lengo lake nikuona wafanyakazi wanafanya kazi kwa kujituma kwa moyo mmoja ili kupelekea Taasisi kupata mapato na kuwezesha kupata maslahi kwa wakati nakuwahi mahala pa kazi na pia aliwaomba kwa wafanyakazi wote kujituma ili kuzalisha kiasi cha kutosha ili hata ikitokea kumwambia mwajiri aweze kuwa na kitu cha kutulipa.

Masula anawaomba washiriki hao kuweza kujitegemea katika kujiajiri kwa kufuga kuku ambapo mtu huyo anaweza kuchukuwa dakika 45 ambazo zinamtosha kuiendeleza miradi yake tofauti ya kwenda katika hospitali nyingine na kwenda kuumia kwa masaa mengine, pia Masula alisema.

Kuzingati mafunzo hayo waliyoyapata na kuwa ufugaji wa nyuki na kilimo cha kisasa kutoka kwa mtoa mada kuzingatia sana ili mfanyakazi aweze kujikwamua na isiwe kutegemea mshahara .

Masula alisema,  kulingana na mafunzo hayo mtu anaweza kujiajiri na kuajiri watu wengine kwakujipatia kipato nje ya mshahara na kutowa wito kwa Serikali katika sehemu zao za kazi, Serikali iweze kuwashawishi wafanyakazi sehemu zao za kazi wajiunge na vyama vyao vya wafanyakazi na vilevile Serikali ijaribu kuviwezesha vyama vya wafanyakazi pale wanapodai madai yao waweze kutimiziwa, aliendelea kwa kusema.

Mfano wapo wafanyakazi ambao hawajapata mafao yao na mtuhuyo kisha staafu kwa mujibu wa sheria na anaendelea kuambiwa asubiri kwa muda mrefu, hivyo naiomba serikali kulifanyia kazi kwa wafanyakazi wanao dai walipwe kwa wakati pia.

Naishukuru Taasisi ya MOI kwa mtu anaye staafu hupewa mkono wa kwaheri ambapo unamuwezesha kumsaidia huko anakokwenda.

Masula ajijibu swali aliloulizwa na mwandishi, hapa MOI kunadhana ya wananchi wanasema, wafanyakazi wanafanya kazi wanavyo taka je, unalizungumziaje? Masula alisema.

Naweza kusema hiyo ni dhana potofu na ninayoweza kusema ni potofu kaulihiyo na niyakupuuzwa na ni kwamba sikweli na kwa muda nilioingia madarakani sijasikia swala hilo kwa wafanyakazi wa Taasisi hii swala hilo halipo na tunajitahidi kupita katika kila Idara na pia MOI tunafanya kwa masaa kumi na mbili na wanafanyakazi kwa kujituma sana na hata ukipita na utawakuta kila mmoja mgonjwa yupo katika sehemu yake anayo tibiwa kulingana ugonjwa.



 Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt. Respicious Boniface akizungumza na wandishi mara baada ya kufunga semina ya
ujasilia mali kwa wanachama wa Tawi la Tughe (MOI).

 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI Dkt. Respicius (wa tatu kushoto) waliyokaa katika picha ya pamoja na  washiriki 





Katibu Tughe Mkoa, Gaudensi Kadyango (kulia) akizungumza na wanachama wa Tughe Tawi la Taasisi ya  (MOI) na kumshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo,chachu ya semina hii ni mwendelezo wa semina iliyofanywa Morogoro ilichukua makatibu wa mabaraza ya wafanyakazi, ikachukua wenyeviti wa chama cha wafanyakazi na ikachukua afisa utumishi  mmoja kila tawi kwa aliyeweza kushiriki
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI Dkt. Respicius (wa tatu kushoto) waliyokaa katika picha ya pamoja na  washiriki 

0 comments:

WATANZANIA WAMETAKIWA KUENZI UTAMADUNI WETU KUKUZA FURSA ZA UTALII WA KIUTAMADUNI

Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu

Watanzania wametakiwa kuenzi mila na desturi ambazo ni chanya wazitunze na kuzitumia ili kujenga jamii yenye maadili mema nchini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadaye.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom wilaya Mbulu mkoani Manyara ambapo amejionea utajiri wa kiutamaduni wenye fursa za utalii wa kiutamaduni.

“Nimetembelea nyumba za asili zilizopo hapa katika kituo hiki nimefurahishwa sana na utajiri wa kiutamaduni uliopo hapa, wazee walizingatia maadili katika kuwalea watoto wao kulingana na mila na desturi zao, ni vema tuenzi utamaduni wetu, huo ni msingi wa maadili mema ya jamii” alisema Naibu Waziri Wambura

Akitolea mfano wa maadili mema yanayopaswa kurithishwa aliyojionea katika kituo cha 4CCP na namna ambavyo watoto waliheshimu nyumba za wazazi wao, Naibu Waziri Wambura amesema kuwa kwa mujibu wa mila na desturi za Kitanzani suala la ulevi na utumiaji wa tumbaku kwa vijana ilikuwa ni mwiko hadi kijana afikie umri wa utu uzima ambapo anaweza kuwa na maamuzi sahihi katika maisha yake yenye kuwa na tija kwa familia.

“Kabla ya kuoa kijana alikuwa haruhusiwi kutumia tumbaku na kunywa pombe, bali kijana akioa na kuwa na watoto wawili kwa mujibu wa mila za makabila ya yaliyopo Mbulu aliruhusiwa kuingia katika kundi la watu wazima na kuruhusiwa kutumia vitu mbalimbali ikiwemo tumbaku na kinywaji cha pombe. Hapa kuna jambo la Watanzania kujifunza na kutunza ili kuondokana na mmomonyoko wa maadili” alisema Naibu Waziri Wambura.

Mila za jamii zilizo njema zinapaswa kutunzwa na kuendelezwa ili ziweze kusaidia vijana na jamii kwa ujumla kuweka mawazo yao katika shughuli za maendeleo pamoja na kupatia familia zao mahitaji ya kila siku.

Naibu Waziri Wambura alisisitiza kuwa mila hizo hazitakiwi kuachwa bali zainatakiwa kuenziwa, kutunzwa, kuendelezwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya sasa ziweze kuchangia katika kukuza utalii wa kiutamaduni ambao ni moja ya vyanzo vya mapato kwa wanajamii na taifa kwa ujumla.

Aidha, Naibu Waziri Wambura alisema kuwa wilaya ya Mbulu ni tajiri katika masuala ya utamaduni na kuongeza kuwa wilaya hiyo ni mdau muhimu katika sekta ya michezo na utamaduni ambazo zinapaswa kuendelezwa kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wake Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay amesema kuwa wilaya hiyo imekuwa na utamaduni wa kufanya tamasha la utamaduni kila mwaka ambapo mwaka huu lilifanyika tarehe 21 hadi 23 mwezi Septemba na inaedelea kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hatua inayopelekea makabila yote kuwa mstari wa mbele katika kudumisha amani ya nchi.

Mbunge huyo aliyataja makabila yanayotokana na makundi makuu manne yanayopatikana wilaya ya Mbulu kuwa ni pamoja na Wairaqw ambao ni jamii ya Wakushi, Wahadzabe jamii ya Khoisan, Wanyiramba na Wanyisanzu jamii ya wabantu na Wadatooga jamii ya Kiniloti.

Naye Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga amemhakikishia Naibu Waziri Wambura kuwa wilaya hiyo itaendelea kuenzi sekta ya utamaduni kwa kuwa na tamasha la utamaduni linalokutanisha makabila yote wilyani humo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uanuwai wa Utamaduni duniani ambayo hufanyika mwezi Mei tarehe 21 kila mwaka.

Hatua hiyo inatokana na Tanzania kusaini mkataba wa azimio la Umoja wa Mataifa (UN) kuenzi utamaduni na kuheshimu tamaduni za watu wengine chini unaosimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mwaka 2002 Umoja wa Mataifa uliamua kuanzisha maadhimisho ya siku ya Utamaduni Duniani kutokana na kuongezeka kwa migogoro, mapigano na kupotea kwa maisha ya watu na mali zao iliyokuwa inatokea sehemu mbalimbali duniani mwishoni mwa miaka ya 1990.

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kushoto) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Ulinzi na Usalama mara baada ya kuwasili Wilayani Mbulu kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.
Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga akimkaribisha Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura kuongea na wananchi waliokuwa katika tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom mara baada ya kuwasili Wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.
Baadhi ya Washiriki wa tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom, wilaya ya Mbullu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (hayupo pichani) alipotembelea kituo hicho.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akitoka ndani kujionea moja ya nyumba za asili ya Wabantu Wanyiramba na Wanyisanzu iliyopo Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akicheza ngoma na washiriki wa tamasha la utamaduni alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kulia) akipata maelezo ya utamaduni wa kabila la Wadatoga katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wasichana wa kabila la Datoga na kusisitiza Watanzania kuenzi utamaduni wetu kwa kuurithisha kwa vijana wetu. Wa nne kushoto ni Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay.(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu)

0 comments:

MAKAMISHNA WA UPELELEZI WA KODI AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA DAR

Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala akisalimiana na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala kabla ya kuanza kwa mkutano wa watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs) 
Washiriki wa mkutano huo wakianza kwa kumtanguliza Mungu kwanza. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa akisoma hotuba ya Kamishna Mkuu wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa makamshina na watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya watendaji waandamizi wa mamlaka hiyo wakati wa mapumziko ya Mkutano wa Mamlaka za mapato za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofunguliwa jijini Dar es Salaam leo Septemba 27 2017. Kutokea (kushoto) ni Kaimu Naibu Kamishna wa Upelelezi wa Kodi, Salim Kessi, Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo. 
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo. 
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo.

0 comments:

WAFANYABIASHARA SOKO LA ILALA MCHIKICHINI JIJINI DAR ES SALAAM WAPEWA ELIMU YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

Mwezeshaji wa kisheria kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG), Amina Mussa akitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia kwa wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo. 
Mfanyabiashara Shikei Ngosi, akielezea changamoto zinazotokana na ukatili wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji Khadija Mohamed akitoa elimu ya upingaji wa ukatili wa kijinsia.
Mfanyabiashara, Mussa Ibrahim, akichangia jambo.
Juma Mohamed akichangia jambo.
Mfanyabiashara wa nguo katika soko hilo, Godrey Milonge akielezea changamoto za ukati wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji wa Sheria kutoka Soko la Temeke Stereo, Batuli Mkumbukwa akichangia jambo.
Mwezeshaji Sheria,wa Soko la Kigogo Kisambusa, Mariam Rashid akitoa mafunzo
Mwezeshaji wa Sheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Consolata Cleophas akitoa elimu hiyo.
Mfanyabiashara, Johnson Stephano akisoma moja ya kijarida kinachoelezea ukatili huo.
Mafunzo yakiendelea.
Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Suzan Sitha, akiwaeleza jambo wafanyabiashara wa soko hilo kuhusu kukomesha ukatili wa jinsia.



Na Dotto Mwaibale

WAFANYABIASHARA katika Soko la Ilala Mchikichini wamepatiwa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia masokoni .

Katika hatua nyingine wafanyabiashara wanaume wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia na wanawake wametakiwa kwenda kushitaki ofisi za masoko husika ili sheria ichukue mkondo wake kwa wahusika waweze kujirekebisha.

Mwito huo umetolewa na Mwezeshaji wa Sheria masokoni, Khadija Mohamed kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG) wakati wanasheria wa shirika hilo wakitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo hii.

"Wakina baba mnapofanyiwa vitendo vya kijinsia na wanawake katika masoko msione haya nendeni kushitaki kwa viongozi wa masoko ili watuhumiwa waweze kukamatwa na kujirekebisha" alisema Mohamed.

Mohamed alisema vitendo vya ukatili wa jinsia hawafanyiwi wanawake pekee bali hata wanaume wamekuwa wakifanyiwa lakini wanaona aibu kwenda kushitaki.Mwezeshaji wa Sheria Batuli Mkumbukwa alisema vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo vimeshamiri hivyo alitoa mwito kwa wafanyabiashara wa soko hilo kuviacha. 

Mkumbukwa alisema ili kumaliza vitendo hivyo kwa makosa madogo madogo kama kutoa lugha ya matusi, kumshika mtu maunoni bila ya ridhaa yake mtuhumiwa amekuwa akipewa adhabu pamoja na kupigwa faini lakini kwa kosa la ubakaji adhabu yake ni kifungo cha maisha au miaka 30.

Mariam Rashid, ambaye ni mwezeshaji wa kisheria kutoka EfG alitaja ukatili wa kijinsia unaofanyika katika masoko ni ukatili wa kingono, uchumi, kisaikolojia na kimwili.Baadhi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vinafanyika katika soko hilo ni pamoja na wafanyabiashara kuwashika sehemu za siri wateja wao wa kike maarufu kama kunawa, kukojoa kwenye chupa za maji na kwenda kuziweka kwenye meza za 

wafanyabiashara, lugha za matusi, kujambisha na kutolipa fedha baada ya kuuziwa chakula na mama lishe.Wafanyabiashara katika soko hilo walisema kuwa kukithiri kwa vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo kwa namna moja au nyingine vinachangiwa na wanawake wenyewe kutokana na tamaa zao kwa kuvaa nguo fupi na kujilengesha kwa wanaume ili wapate bure bidhaa wanazozitaka.

"Wanawake wanabakwa na kushikwa maungoni kwa kupenda wenyewe wala hawalazimishwi" alisema Juma Mohamed mfanyabiashara.

Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Susan Sitta alisema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwaongezea uelewa wafanyabiashara ili waweze kuacha kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia katika masoko ili kutoa fursa kwao kufanya biashara zao bila ya kuwa na bugudha.

Alisema mradi huo umefadhiliwa na Shirika la United Nations Trust Fund na kuwa unafanyika katika masoko ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na Temeke.

0 comments:

MKUU WA MKOA WA SHINYANGA AZINDUA KAMPENI YA UPANDAJI MITI 'SHINYANGA MPYA,MTI KWANZA'


Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akizindua kampeni ya upandaji miti ya ‘Shinyanga Mpya, Mti Kwanza’ leo Septemba 23,2017-Picha na Kadama Malunde - Malunde1 blog




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack amezindua kampeni ya upandaji miti katika wilaya ya Shinyanga yenye kauli mbiu ya ‘Shinyanga Mpya,Mti Kwanza’ ili kuboresha mazingira Shinyanga na kupambana na mabadiliko ya tabia nchi yanayosababisha jangwa. 


Kampeni hiyo inayoratibiwa na ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, imezinduliwa leo Jumamosi Septemba 23,2017 katika manispaa ya Shinyanga ,kwa lengo la kuboresha mazingira ya mji wa Shinyanga,maeneo ya taasisi,maeneo ya wazi,maeneo yanayozunguka kaya,kandokando ya barabara na sehemu zingine ambazo hazina miti. 


Akizungumza wakati wa kuzindua kampeni hiyo,Telack alisema kutokana na mvua haba katika mkoa wa Shinyanga, kumekuwepo na mabadiliko ya tabia nchi hali inayosababisha kuwepo na hali ya jangwa. Telack aliwataka wananchi na wadau wote kuhakikisha wanatunza miti hiyo na kuzuia mifugo kuzurura ovyo mitaani. 


“Tutakuwa wakali,kuanzia sasa ni marufuku kwa mifugo kuzurura mitaani, ikikamatwa kwa kila mfugo faini ni kati ya shilingi 50,000/= na 100,000/=,iwe ng’ombe,mbuzi,kondoo au punda, tukikuta mti umekauka faini ni shilingi 50,000/=”,alieleza mkuu huyo wa mkoa. 


Naye Mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro alisema uzinduzi wa kampeni hiyo umeanza na barabara 25 za mji wa Shinyanga ambapo jumla ya miti 3000 imepandwa na ofisi zote kata 17 za manispaa ya Shinyanga zitaendelea kutekeleza zoezi hilo. 


“Kampeni hii ni kwa wilaya ya Shinyanga,leo tumeanza katika manispaa ya Shinyanga,tunataka wilaya yetu iwe na mandhari nzuri ya kuvutia,ardhi iboreke,tuzuie upepo mkali katika majengo,tuhifadhi vyanzo vya maji,kuongeza vivuli katika maeneo ya kupumzikia,kujinasua na athari za mabadiliko ya tabia nchi lakini pia jamii itanufaika na miti ya matunda itakayopandwa”,alifafanua Matiro. Alibainisha kuwa ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi,sasa wilaya hiyo imekuja na teknolojia rahisi ya kumwagilia miti kwa njia ya matone,teknolojia ambayo inatumia maji kidogo lakini inaweza kumwagilia miti mingi na kwa muda wote. 


“Tumekuwa tukipanda miti kila mwaka lakini miti hii ilikumbwa na changamoto nyingi wakati wa usimamizi na kusababisha miti mingi kufa,kwa sasa tumekuja na mpango huu mpya wa kupanda miti itayosimamiwa na wananchi na wadau wote”,alieleza Matiro. Alisema kauli mbiu hiyo ya Upandaji miti ya ‘Shinyanga Mpya,Mti Kwanza’ ina maana ya kuwaasa watu wote wa Shinyanga kuachana na tabia ya kuharibu miti na hivyo wahifadhi miti. 


“Tutatekeleza kampeni hii katika halmashauri zote,kila halmashauri itaanzisha kitalu na kuzalisha miche isiyopungua 25,000,kila kata ipande miti isiyopungua 1000 na iwe na kitalu cha kudumu,ofisi za mitaa na vijiji miti 100,vitongoji miti 50,kila mwananchi miti isiyopungua mitatu na taasisi zote zipande miti”,alifafanua Matiro.


Aliongeza kuwa ili kufanikisha kampeni hiyo,taasisi mbalimbali zitachangia mbegu,miche na kupanda miti ili kufikia lengo la kupanda miti isiyopungua milioni 1,500,000 kwa mwaka.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akizungumza wakati wa kuzindua kampeni ya upandaji miti ‘Shinyanga Mpya,Mti Kwanza’ leo katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga.Kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga,Geofrey Mwangulumbi.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akiteta jambo na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro wakati wa uzinduzi huo. 

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ya upandaji miti ambapo alisema miongoni mwa malengo yake ni kuhifadhi ardhi na kuiongezea thamani,kuzuia mmomonyoko wa adhi na kuboresha mazingira

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.Alieleza kuwa kila kiongozi akialikwa kwenye tukio lolote,kabla ya shughuli ni vyema kwanza apande mti.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akisisitiza kuwa kampeni hiyo inalenga kujinasua na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Wananchi wakiwa wameshikilia vijiti vinavyotumika katika zoezi la upandaji miti.

Uzinduzi unaendelea

Mdau wa Mazingira Ezra Manjerenga akieleza namna ya kupanda miti hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akipanda mti nje ya ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga.

Wananchi wakishuhudia mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akipanda mti.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akichomeka vijiti kwenye mti aliopanda.

Meneja wa Benki ya CRDB,Said Pamui akipanda mti nje ya ofisi ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya upandaji miti 'Shinyanga mpya,mti kwanza'.

Wafanyakazi wa benki ya CRDB na wananchi wakishuhudia Meneja wa Benki ya CRDB,Said Pamui akipanda mti.

Meneja wa Benki ya CRDB,Said Pamui akishindilia udongo kwenye mti alioupanda.
Wananchi wakitoka katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Shinyanga wakielekea kwenye barabara mbalimbali mjini Shinyanga kwa ajili ya kupanda miti.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akiweka udongo kwenye mti alioupanda nje ya ofisi ya CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akiwa katika ofisi ya CCM wilaya ya Shinyanga mjini.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akichimba shimo kwa ajili ya kupanda mti katika barabara ya Hospitali ya mkoa wa Shinyanga.

Mwananchi akifurahia baada ya kumaliza kupanda mti katika Barabara ya Shinyanga - Mwanza.

0 comments: