WAFANYABIASHARA SOKO LA ILALA MCHIKICHINI JIJINI DAR ES SALAAM WAPEWA ELIMU YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:02 PM
Mwezeshaji
wa kisheria kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG), Amina Mussa
akitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia kwa
wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo.
Mfanyabiashara Shikei Ngosi, akielezea changamoto zinazotokana na ukatili wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji Khadija Mohamed akitoa elimu ya upingaji wa ukatili wa kijinsia.
Mfanyabiashara, Mussa Ibrahim, akichangia jambo.
Juma Mohamed akichangia jambo.
Mfanyabiashara wa nguo katika soko hilo, Godrey Milonge akielezea changamoto za ukati wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji wa Sheria kutoka Soko la Temeke Stereo, Batuli Mkumbukwa akichangia jambo.
Mwezeshaji Sheria,wa Soko la Kigogo Kisambusa, Mariam Rashid akitoa mafunzo
Mwezeshaji wa Sheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Consolata Cleophas akitoa elimu hiyo.
Mfanyabiashara, Johnson Stephano akisoma moja ya kijarida kinachoelezea ukatili huo.
Mafunzo yakiendelea.
Ofisa
Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Suzan Sitha, akiwaeleza jambo
wafanyabiashara wa soko hilo kuhusu kukomesha ukatili wa jinsia.
Na Dotto Mwaibale
WAFANYABIASHARA katika Soko la Ilala Mchikichini wamepatiwa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia masokoni .
Katika
hatua nyingine wafanyabiashara wanaume wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia
na wanawake wametakiwa kwenda kushitaki ofisi za masoko husika ili
sheria ichukue mkondo wake kwa wahusika waweze kujirekebisha.
Mwito
huo umetolewa na Mwezeshaji wa Sheria masokoni, Khadija Mohamed kutoka
Shirika la Equality for Growth (EfG) wakati wanasheria wa shirika hilo
wakitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa
wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo hii.
"Wakina
baba mnapofanyiwa vitendo vya kijinsia na wanawake katika masoko msione
haya nendeni kushitaki kwa viongozi wa masoko ili watuhumiwa waweze
kukamatwa na kujirekebisha" alisema Mohamed.
Mohamed
alisema vitendo vya ukatili wa jinsia hawafanyiwi wanawake pekee bali
hata wanaume wamekuwa wakifanyiwa lakini wanaona aibu kwenda kushitaki.Mwezeshaji
wa Sheria Batuli Mkumbukwa alisema vitendo vya ukatili wa kijinsia
katika soko hilo vimeshamiri hivyo alitoa mwito kwa wafanyabiashara wa
soko hilo kuviacha.
Mkumbukwa
alisema ili kumaliza vitendo hivyo kwa makosa madogo madogo kama kutoa
lugha ya matusi, kumshika mtu maunoni bila ya ridhaa yake mtuhumiwa
amekuwa akipewa adhabu pamoja na kupigwa faini lakini kwa kosa la
ubakaji adhabu yake ni kifungo cha maisha au miaka 30.
Mariam
Rashid, ambaye ni mwezeshaji wa kisheria kutoka EfG alitaja ukatili wa
kijinsia unaofanyika katika masoko ni ukatili wa kingono, uchumi,
kisaikolojia na kimwili.Baadhi
ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vinafanyika katika soko hilo
ni pamoja na wafanyabiashara kuwashika sehemu za siri wateja wao wa
kike maarufu kama kunawa, kukojoa kwenye chupa za maji na kwenda
kuziweka kwenye meza za
wafanyabiashara, lugha za matusi, kujambisha na kutolipa fedha baada ya kuuziwa chakula na mama lishe.Wafanyabiashara
katika soko hilo walisema kuwa kukithiri kwa vitendo hivyo vya ukatili
wa kijinsia katika soko hilo kwa namna moja au nyingine vinachangiwa na
wanawake wenyewe kutokana na tamaa zao kwa kuvaa nguo fupi na
kujilengesha kwa wanaume ili wapate bure bidhaa wanazozitaka.
"Wanawake wanabakwa na kushikwa maungoni kwa kupenda wenyewe wala hawalazimishwi" alisema Juma Mohamed mfanyabiashara.
Ofisa
Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Susan Sitta alisema lengo la
kutoa mafunzo hayo ni kuwaongezea uelewa wafanyabiashara ili waweze
kuacha kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia katika masoko ili kutoa
fursa kwao kufanya biashara zao bila ya kuwa na bugudha.
Alisema
mradi huo umefadhiliwa na Shirika la United Nations Trust Fund na kuwa
unafanyika katika masoko ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na Temeke.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: