WAISLAMU WACHANGIA CHUPA 44 ZA DAMU, MADHIMISHO YA MTUME MUHAMAD (S.W.A)


WAISLAMUNA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA
WAISLAMU  wa  Halmashauri ya Mnispaa ya Kigoma Ujiji Mkoa wa Kigoma wamechangia chupa 44 za damu ikiwa ni sehemu ya Madhimisho ya Kuzaliwa kwa  Mtume Muhamad ( S.W.A) kila ifikapo mfungo sita wa mwishoni mwa Mwaka.

Mbali na hilo wamehamasishwa kufanya matukio  chanya yatakayoathiri jamii kwa ujumla ambapo awali walifanya usafi katika makaburi ya yaliyopo kata ya Kipampa kigoma ujiji kwa nia ya kuimarisha imani,upendo na kulinda amani kwa kuongeza ibada kwa mwenyezi mungu yatakayosaidia umati wa mtume muhamad iondokane na tamaduni zisizofaa duniani na akhera siku ya kiyama.

Akifafanua  hilo kijiji cha kidahwe baada ya sherehe hiyo iliyohitimishwa na Mjumbe wa Mashekhe BAKWATA  Shekhe Haruna Kibonajoro ,Katibu wa Baraza la waislamu mkoani hapa( BAKWATA),Alhaji Shabani Guoguo alisema madhimisho hayo ni fursa kwa waislamu kubuni mbinu mbalimbali za kutoa sadaka ikiwemo sadaka kubwa ya damu,ambayo inaokoa mamia ya wahitaji wa damu hiyo akitolea mfano majeruhi wa ajali na wanawake wanaokabiliwa na uzazi pingamizi.

Alhaji Guoguo alisema ili kuimarisha imani kwa waumini wa dini hiyo,mashekhe hawana budi kutembea kaya hadi kaya kutoa mawaidha ambayo yataimarisha imani ya walengwa ili waepukane na janga la ulevi ,uzinifu na uhalifu wa kutumia silaha za moto sambamba na makundi yanayotumia dini kudhulumu uhai na mali za watu na kusihi waepuke na migogoro ya kugombea misikiti.

Jamboleo lilizungumza na Mkuu wa kitengo cha Damu salama mkoani humo Juma Kiangi juu ya tukio hilo,akiri kupokea makundi ya waislamu waliojitolea damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wahitaji na walifanikiwa kupata chupa 44 za damu,ambapo hitaji la mkoa kwa siku ni chupa 1,500 na kutoa wmwito kwa wadau wengine wakumbuke kutoa sadaka  kwa wahitaji ili wapate fadhila kwa mola wao.

Baadhi ya waumini wa dini hiyo Johari Yusuph na Zituni Kabeke kwa nyakati tofauti wakiri madhimisho ya mazazi ya mtume muhamad (SWA) ni fursa kwa waislamu kuitumia siku hiyo kwa toba ya dhati kwa kuwa kila aombaye na kutubu siku hiyo hufutiwa madhambi na hupatiwa kila ahitajilo kwa kuwa ni siku iliyotakasika kwa mujibu ya kitabu kitukufu cha Q’ruani ambacho kimechakata utume wake na dhima kwa umati wake.
Mwisho.

0 comments: