KANAL NDAGALA AKEMEA WATANZANIA WILAYANI KAKONKO- KIGOMA


NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA


UCHELEWESHWAJI  wa Malipo ya posho kwa wakimbizi kutoka Nchi jirani imekuwa ni chachu ya kuongeza kwa matukio ya kihalifu likiwemo la mauwaji kwa nia ya kulipiza kisasi kwa wananchi wa taifa hili wanaowatumia katika shughuli za kilimo.



Hayo yalisemwa juzi  na Mkuu wa Wilaya ya Kakonko Kanal Hosea Ndagala  katika  kikao cha dharura cha Balaza la Madiwani kilichokuwa kikihamasisha shughuli za uhifadhi wa mazingira kutoka shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na mswala uhifadhi wa mazingira katika makambi ya wakimbizi  hasa Kakonko na Kibondo (Redeso).


Kanali Ndaala alisema baadhi ya watanzania huwatumikisha wakimbizi mashambani kwa shughuli za kilimo na  baadhi yao huwacheleweshea na wengine huwanyima  stahiki zao hali inayosababisha baadhi ya wakimbizi kujihusisha na vitendo vya uharifu kwa kulipiza visasi  hatimaye kutumia silaha za moto kuiba mali na hata  mauwaji.


Baadhi ya washirika wa warsha hiyo  ni pamoja na Kasuku Bilago alisema sheria ya mazingira haina meno hali inayochangia uharibifu mkubwa wa mazingira ,ambapo wananchi hulima kwenye vyanzo vya maji na kuchoma moto Misitu bila kuchuliwa hatua za kisheria,ambayo ingewafunza wengine.


Nae Ofisa Mali Asili wa humo Simon Mando  alisema kuwa sheria za mazingira zipo na zina makatazo yake kinachotakiwa ni viongozi wa ngazi zote kuzisimamia ili kuepuka madhara makubwa yanaoweza kujitokeza ikiwa hawawajibiki kuelimisha umuhimu wa utunzaji wa mazingira hali inayokaribisha changamoto ya mabadiliko ya  tabia Nchi.


Baadhi ya Wananchi waliohojiwa na gazeti hili  Filemon Makungu na Masoud Khalfan walizitaka Mamlaka za Serikali wa vijiji watenge mipango ya matumizi bora ya ardhi ,ili kuondoa migongano kwa jamii inayochangiwa  na  viongozi husika ambao wanalima katika vyanzo vya maji,kujenga makazi ndani ya mita 60 kutoka kwenye chanzo cha maji hali inayowashawishi raia kuiga .




Akifunga kikao hicho cha siku mbili Mweneyekiti wa Halmashauri hiyo Juma Maganga aliwaelekeza  Watendaji wa Kata na Madiwani waelimishe wananchi juu  ya uhifadhi wa mazingira na sheria zake  kwa kuwa uhifadhi wa mazingira  ni pamoja na kuchukua hatua za kisheria kwa wakaidi wa uhifadhi wa mazingira.
Mwisho.

0 comments: