
kukopa Wizarani shilingi 500/- (kuzilipa baada ya kuanza kazi). Wanafunzi wengi walikuwa wakikosa kuingia madarasani shauri ya “pesa kibindoni” au kwa msemo wa siku hizo “bumu” (boom)! Wanafunzi wa kiume waliweka hata vimada wa kike hadi “bumu” ilipokauka!
Mwanzo wa mwaka ulikuwa pia ni “bumu” kwa watu wengi wasio wanafunzi. Waliibia kuja kula hadi hapo vitambulisho vilipotolewa na njia nyinginezo za kudhibiti kula mara mbili au tatu zilipotekelezwa kwa wanafunzi!
Najua wakati wa Juma la Kwanza la Kuzoezeshwa (Orientation Week), tulifundwa namna ya kuishi katika mazingira hayo ya ki-elimu na yale ya maudhui ya kufahamiana na kuelewana (social growth), ikiwa ni pamoja na ustaarabu (etiquettes) wa chumba cha mlo: jinsi ya kutumia uma, vijiko na visu na chakula gani kinaanza!
Nakumbuka mwaka wangu wa kwanza na wa pili, kila baada ya miezi kama mitatu hivi, jioni moja tulikuwa tunaandaliwa Hall of Residence Dinner Evening – kana kwamba tuliishi katika hoteli ya Nyota Nne au Tano – na dansi la kukata shoka! Mwishowe, wenye msimamo mkali wakakataa hayo ya Dinner; tulikuwa na chakula cha jioni ambacho kilikidhi mahitaji ya siha na kutujenga akili.
Wanafunzi wengine waliokuwa na akili za huruma (compassion) kwa maskini na ma-kabwela walishauri, pembeni, hizo pesa za “dinner” zitumike kwa ajili ya maslahi yao. Lakini wanafunzi wenye kupenda ulevi (unywi) walishauri kuwa hizo pesa zitumie kuongezea vinywaji; wakashinda! Baadhi ya wanafunzi “wanywi” wakaanza kukusanya hata makesi ya bia. Hatimaye, ikaamuliwa kuwa kila mmoja apewe vocha tatu kwa ajili ya kupata chupa tatu za bia.
(Tuyaache hayo ya unywi!) ... Wengi wetu hatutamsahau Daktari m-Ulaya wa dispensary yetu! Jina lake limenitoka kidogo...tulimwita “Dr. Nyurosisi” (Neurosis) kwa sababu kwake kila tatizo la kuumwa kwa mwanafunzi lilisababishwa na “neurosis”!
Sisemi kuwa kila m-Tanzania mwenye asili ya ki-Asia alikuwa mbaguzi. La hasha! Vijana wengine, kama akina Issa Shivji, Hirji, Sumra na Meghji walijumuika nasi wa-Matumbi bila ubaguzi wowote. Lakini kulikuwa na fununu kuwa baadhi yao walikuwa wakipata wakati mgumu kutoka kwa “dugu zao” waliowashitaki mbele ya jamii yao huko mjini!
0 comments: