MAWAZIRI WA JPM "WASHAMBULIA" KAMA NYUKI, NCHEMBA, SIMBACHAWENE, DKT. KIGWANGALA "WAVAMIA" MACHINJIO YAVINGUNGUTI, MKUU WA MNADA WA PUGU AFUTWA KAZI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:12 AM
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
Mwigulu Nchemba, (kushoto), Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Tamisemi, na
Utawala Bora), Bw. George Simbachawene, (katikati), na Naibu Waziri wa
Afya, Dkt. Khamisi Kigwangala, wakijadiliana jambo wakati 'walipovamia'
machinjio ya Vingunguti jijini Dar es Salaam leo asubuhi Januari 2,
2016. ambapo pamoja na mambo mengine, Mkuu wa Mnada wa mifugo, Pugu
jijini Dar es Salaam, amefutwa kazi na maafisa wengine kadhaa kwa
"kutafuna" fedha za ushuru wa mifugo
NA
K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
Mwigulu Nchemba, amemfuta kazi Mkuu wa
mnada wa pugu na Watumishi waliokuwa zamu tar.24.12.2015 na tar.01.01.2016 na kuagiza wafike kwa Katibu Mkuu wa Wizara
hiyo Jumatatu Januari 4. 2015 kwa maelezo zaidi.
Mbali na
kuwafuta kazi watumishi hao Nchemba pia amesitisha kuanzia leo uchukuaji wa Ushuru eneo la mnada
wa pugu,badala yake makusanyo yote ya fedha za serikali hizo yatafanyika
Machinjio ya Vingunguti kwa kutumia mashine za Elektroniki za EFD,Kwa maana
hiyo mnada wa pugu utakuwa unatumika kutoa vibali tu vya mifugo ilikudhibiti
ubora wa mifugo inayopaswa kuchinjwa.
Uamuzi mwingine aliouchukua Waziri
Nchemba ni
eneo la kuhifadhia nyama lililokuwa
limejengwa kwa fedha za Wananchi kushirikiana na serikali lifunguliwe kwaajili
ya Wananchi kulitumia kuhifadhia nyama hiyo, awali eneo hilo lilifungwa bila
sababu za msingi.Vilevile umeme uliokuwa umekatwa eneo hilo urudishwe hii leo
kwaajili ya kuwarahisishia wananchi shughuli zao.
Hatua za kuboresha miundombinu ya
Machinjio hayo zimeelekezwa kwa Halmashauri ya Ilala zifanyiwe kazi haraka na
kwa ubora.
Hatua hiyo ameichukua leo Jumamosi
Januari 2, 2015 ikiwa ni saa chache baada ya “kuvamia” machinjio ya Vingunguti
jijini Dar es Salaam usiku wa manane kuamkia Januari 2.
Baada ya kukuta taarifa za utafunwaji wa
fedha za ushuru wa mifugo na malalamiko mengine kibao, Waziri Nchemba aliahidi
kuwa asubuhi atarejea tena na kweli alirejea tena kwenye eneo hilo safari hii
akifuatana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi, na Utawala Bora, George
Simbachawene, na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Khamisi Kigwangalla.
Mwigulu alisema, ziara yake ya kushtukiza usiku wa kuamkia leo
Januari 2, 2016, iligundua ufisadi wa kukwepa kulipa ushuru wa mifugo ambapo
kati ya Ng’ombe 1,450, waliopelekwa kwenye machinjio hayo wakitokea mnada wa
Pugu jijini Dar es Salaam, ni 343 tu ndio waliolipiwa na
mifugo 1,107 haikulipiwa ushuru, kwa maana hiyo “Wajanja” wametafuna fedha.
Hata
hivyo kero za machinjio ya Vingunguti ni nyingi sio kukwepa ushuru tu, bali pia
mazingira machafu ya machinjio na ndio maana Mwigulu aliona peke yake
changamoto za hapo zitamshinda na kuahidi kurejea tena leo asubuhi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)








0 comments: