WILLIUM LUKUVI AKIZUNGUMZA NA WADAU KUHUSU MPANGO WA UENDELEZAJI WA MJI MPYA KIGAMBONI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:08 AM
Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Willium Lukuvi akisisitiza jambo wakati wa
mkutano na wadau kuhusu mpango wa uendelezaji wa mji mpya wa Kigamboni,
Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Meck
Sadiki. Sehemu ya wadau hao ni pamoja na viongozi wa taasisi za
Serikali, mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO’s), madhehebu mbalimbali
ya dini na taasisi za elimu na ulinzi na huduma mbalimbali zilizopo
katika eneo hilo la Kigamboni.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Angellah Kairuki akizungumza katika mkutano na
wadau kuhusu mpango wa uendelezaji wa mji mpya wa Kigamboni, Dar es
Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Sellasie Mayunga akizungumza jambo wakati wa mkutano huo.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bibi Sophia Mjema akizungumza wakati wa mkutano huo.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi Mhe. Willium Lukuvi pamoja na Naibu wake Mhe. Angellah Kairuki
wakimsikiliza mmoja wa wadau Bw. Nyaronyo Kicheere nje ya ukumbi wa
mkutano
RAIS DK. SHEIN, KATIKA UFUNGUZI WA GLOBAL HOSPITAL VUGA MJINI UNGUJA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:44 PM
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein akisalimiana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor Turky Salim Hassan
Turky wakati alipofika kufungua Hospitali ya Global Hospital iliyopo Mtaa
wa Vuga Mjini Unguja leo. (Picha zote na Ikulu)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein akifungua pazia kufungua Hospitali ya Global Hospital
iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo. Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Kampuni ya
Vigor Turky Salim Hassan Turky
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein akipeana mkono wa pongezi na Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor Turky
Salim Hassan Turky baada kuifungua Hospitali ya Global Hospital iliyopo
Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein akikata utepekuifungua Hospitali ya Global Hospital iliyopo Mtaa wa
Vuga Mjini Unguja leo (kushoto ni Dkt. K. Ravindranath Daktari Mkuu na Mwenyekiti
wa Kampuni ya Global Hospital (kulia) Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor
Turky Salim Hassan Turky.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein (wa pili kulia) akipata maelezo alipotembelea mashine ya Xray baada ya kuifungua Hospitali ya
Global Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo (wa kwanza kulia)
Dkt. K. Ravindranath Daktari Mkuu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Global Hospital.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein (katikati) akiwa na Daktari Mkuu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Global
Hospital Dkt. K. Ravindranath (wa pili kulia)
na Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor Turky Salim Hassan Turky
wakiangalia mashine ya kufanyia Upasuaji wakati alipotembelea Hospitali ya Global
Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo baada ya kuifungua rasmi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein akifuatana na Daktari Mkuu na Mwenyekiti wa Kampuni ya Global
Hospital Dkt. K. Ravindranath (kulia), wakati alipotembelea
sehemu mbali mbali za kutoa huduma katika Hospitali ya Global
Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo baada ya kuifungua rasmi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mwakilishi wa Mwakilishi wa
Kampuni ya Global Hospital ya India Dkt. Nagesh Rao (kulia), wakati alipotembelea
katika vyumba vya upasuaji vyenye mashine za kisasa baada ya kuifungua Hospitali ya
Global Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo (katikati) Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor Turky Salim
Hassan Turky.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein (wa pili kushoto), akipata maelezo kutoka kwa Daktari Mkuu na Mwenyekiti
wa Kampuni ya Global Hospital ya India Dkt. K. Ravindranath
(katikati) wakati alipotembelea chumba cha wagonjwa
mahututi (Theatre) baada ya kuifungua Hospitali ya Global Hospital
iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo (kulia) Mkurugenzi wa Hospitali ya
Mnazi Mmoja Dk.Jamala A.Taibu.
Baadhi ya Madaktar na waalikwa katika sherehe ya ufunguzi wa Hospitali ya Global
Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
alipokuwa akitoa hutuba yake ya ufunguzi wa Hospitali hiyo leo.
Baadhi ya waalikwa mbali mbali katika sherehe ya ufunguzi wa Hospitali ya Global
Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
alipokuwa akitoa hutuba yake ya ufunguzi wa Hospitali hiyo leo.
Mwenyekiti wa Kampuni ya Vigor Turky Salim Hassan Turky akitoa
salamu zake mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
baada kuifungua Hospitali ya Global Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini
Unguja leo.
Kaimu Waziri wa Fedha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala
Bora Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini akisema machache na kumkaribisha mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) kuzungumza na wananchi
baada ya kuifungua Hospitali ya Global Hospital iliyopo Mtaa
wa Vuga Mjini Unguja leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein (kulia) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za ufunguzi wa Hospitali ya Global
Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo inayomilikiwa na Kampuni ya
Vigor Turky ya hapa Zanzibar ambayo itatoa huduma za Maradhi mbali mbali.
Baadhi ya Viongozi wa Serikali na taasisi mbali mbali
na waalikwa wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za ufunguzi wa Hospitali
ya Global Hospital iliyopo Mtaa wa Vuga Mjini Unguja leo inayomilikiwa na
Kampuni ya Vigor Turky ya hapa Zanzibar ambayo itatoa huduma za Maradhi mbali
mbali.
Na Said Ameir, Zanzibar
28 Machi, 2015
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein
amesisitiza kuwa Zanzibar kama zilivyo nchi nyingine inatambua sekta za
Afya na Elimu kuwa ndizo msingi wa maendeleo na ukuaji wa sekta nyingine
za kiuchumi na kijamii ndio maana wakati wote imekuwa ikichukuwa hatua
mbalimbali za kuziimarisha sekta hizo.
Dk.
Shein amesema hayo leo mara baada ya kuzindua rasmi hospitali mpya na
ya kisasa ya TASAKHTAA iliyopo Vuga mjini Unguja ambayo imejengwa kwa
ushirikiano kati ya kundi la makampuni ya Vigor Turkey Group ya Zanzibar
na Global hospitals ya India.
“Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar inatambua umuhimu wa sekta hizi kwa ustawi wa
wananchi wa Zanzibar, ndio maana, tumeelekeza juhudi kubwa katika
kuziimarisha kwa kuzifanyia mabadiliko, kutunga sera na sheria madhubuti
na kuongeza bajeti ya mwaka kwa sekta hizi kila mwaka” Dk. Shein
alisema.
Aliwaeleza
viongozi na wageni waliohudhuria hafla hiyo kuwa amefurahishwa na
uwekezaji huo wa aina yake katika sekta ya afya na kueleza matumaini
yake kuwa hatua hiyo itazidi kuimarisha utoaji wa huduma bora za afya
nchini.
Dk.
Shein alisisitiza kuwa azma ya serikali ni kuwa na miradi mingi mikubwa
kama hiyo katika sekta zote na kwamba mswada mpya wa sheria
uliopitishwa hivi karibuni kuhusu uanzishaji na uendeshaji ushirikiano
baina ya Sekta ya Umma na Binafsi ni hatua muhimu katika kufikia azma
hiyo.
Alitoa
wito kuwepo ushirikiano wa karibu kati ya sekta binafsi na sekta ya
umma katika afya na kutolea mfano kuwa hospitali hiyo ya TASAKHTAA kuwa
na mashirikiano na hospitali kuu ya Mnazi mmoja.
“hospitali
yenu itahitaji msaada mkubwa kutoka hospitali ya Mnazi Mmoja na kinyume
chake hivyo mnahitaji kushirikiana”alieleza Dk. Shein na kuongeza kuwa
hospitali hizo hazitakuwa washindani.
Katika
hotuba yake hiyo alizidi kubainisha kuwa Serikali inaendelea
kukamilisha mpango wake wa kuifanya hospitali ya Mnazi Mmoja kuwa ya
rufaa ili iweze kutoa huduma nyingi zaidi na bora zaidi kwa wananchi.
Aliongeza
kuwa kuimarika kwa huduma za afya nchini kutasaidia kupunguza idadi
kubwa ya wagonjwa wanaopelekwa nchi za nje kupata matibabu mara kwa
mara.
Dk.
Shein ambaye kabla ya kuizindua hospitali hiyo alitembelea vitengo
mbalimbali vya hospitali hiyo, alieleza kuvutiwa na vifaa na utalaamu
uliopo lakini alisisitiza lugha na mahusiano mazuri kati ya watumishi wa
hospitali na wagonjwa.
“Hospitali
kama hii inatarajiwa kutoa huduma bora na nzuri, kufanya tafiti, na
kuchunguza maradhi pamoja na kuwapa faraja wagonjwa kwa kuwahudumia kwa
lugha nzuri” Dk. Shein alieleza.
Akizungumza
katika hafla hiyo Waziri wa Afya Rashid Seif Suleiman alisema Wizara
imeupokea mradi huo kwa mikono miwili na kuutaka uongozi wa hospitali
kuzingatia sheria na kanuni za uendeshaji wa hospitali zikiwemo za
usajili wa watumishi wake katika bodi husika za kitalaamu pamoja na zile
zinazohusu madawa.
Naye
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dk. Mwinyihaji
Makame Mwadini kwa niaba ya Waziri wa Fedha alisema sekta ya afya imo
katika mpango kabambe wa serikali wa kutoa vivutio maalum vya uwekezaji
ili kuvutia wawekezaji zaidi.
Alibainisha
kuwa hadi sasa sekta hiyo iko nyuma katika kuvutia wawekezaji tofauti
na sekta nyingine kama ya utalii ambapo nchi inahitaji sana huduma
katika sekta ya afya hivyo Serikali itaweka jitihada za
makusudi kuondoa hali hiyo.
“Inawezekana
hatujaitangaza sana lakini pia yawezekana ni kutokana na ukosefu wa
wataalamu na gharama kubwa za uwekezaji”alisema Dk. Mwinyi na kuongeza
kuwa mradi wa TASAKHTAA umeonesha mfano katika uwekezaji katika sekta
hiyo.
Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Vigor Turkey Bwana
Salim Turky aliwahakikishia viongozi na wageni waliohudhuria hafla hiyo
kuwa uongozi wa hospitali hiyo umedhamiria kutoa huduma bora na na kwa
gharama nafuu kwa wananchi wote.
“tutahakikisha
wananchi wote wanapata huduma za matibabu na tayari baadhi ya
wafanyabiashara wameahidi kusaidia gharama za wananchi ambao hawatakuwa
na uwezo kabisa ili wasikose huduma”alibainisha Bwana Turky.
Alisema
nia ya hospitali hiyo ni kushirikiana na watoa huduma wengine katika
sekta hiyo zikiwemo hospitali za umma hivyo wakati wote.
Alizishukuru
mamlaka mbalimbali za serikali kwa ushirikiano wao ambao hatimae
hospitali hiyo imeweza kukamilika na kuzinduliwa tayari kuanza kutoka
huduma kwa wananchi.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger anapanga
kumnunua kiungo wa kati wa Southampton Mkenya Victor Wanyama na
mshambuliaji wa Anderlecht Aleksandr Mitrovic kulingana na gazeti la the
Sun nchini Uingereza.
Wenger amejiandaa kutoa kitita cha pauni
millioni 30 kwa wachezaji hao wawili,huku Wanyama akigharimu kitita cha
pauni millioni 20 naye mshambuliaji huyo wa Anderlecht Mitrovic
akigharimu pauni millioni 10.
Inaaminika kuwa Wanyama ataondoka katika
kilabu ya Southampton iwapo atachukuliwa na kilabu kikubwa huku naye
Mitrovic akiwa amekuwa akifuatiliwa na waajiri wa Arsenal katika kipindi
cha wiki chache zilizopotea.
Mitrovic amekuwa akifananishwa na Didier Drogba kutokana na mchezo wake.
MAKAMU WA PILI WA RAIS, BALOZI SEIF IDDI AKIKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO TIMU 60 ZA MPIRA WA MIGUU JIMBONI MWAKE KITOPE.
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:33 PM
Mbunge
wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi Seti za Jezi na
Mipira Mmoja wa Viongozi wa timu 60 zilizomo ndani ya Jimbo la Kitope
hapo Kijiji cha Kipandoni Upenja Wilaya ya Kaskazini “B”. Katikati yao ni Mke wake Balozi Seif Mama Asha Suleiman Iddi.
Baadhi
ya vijana wa timu za mitaani zilizomo ndani ya Jimbo la Kitope
zilizopata vifaa vya Michezo vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo,
Balozi Seif Ali Iddi, wakiwa katika hafla hiyo.
Kocha
na Kepteni wa Timu ya Soka ya Kipandoni Star Jeilan Omar Jeilan
akipokea mchango wa shilingi 500,000/- kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la
Kitope Balozi Seif Ali Iddi kwa ajili ya kununulia Posi na Nyafu kwa
ajili ya Kwinja chao cha michezo. (Picha zote na – OMPR – ZNZ)
Na Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
28/3/2015.
Mbunge
wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi leo amekabidhi vifaa vya
michezo kwa Timu 60 za Mpira wa soka zilizomo ndani ya Jimbo hilo ili
kusaidia nguvu na chachu ya kuimarisha Michezo katika Jimbo la Kitope.
Vifaa
hivyo ambavyo ni seti za Jezi na Mipira vyenye Thamani ya shilingi
Milioni Nane, Laki Nne na Hamsini Elfu { 8,450,000/- } vimekabidhiwa
kwa timu hizo hapo Kipandoni Wadi ya Upenja Wilaya ya Kaskazini “B”.
Balozi
Seif akiambatana na Mkewe Mama Asha Suleiman Iddi pamoja na baadhi ya
Viongozi wa Wadi ya Upenja na Jimbo la Kitope akikabidhi Seti za Jezi na
Mipira kwa Timu za Jimbo hilo zinazoshiriki Ligi ya Kanda ya
Unguja,Daraja la Pili na daraja la Tatu.
Na
pia akakabidhi mipira kwa 36 ya Mitaani pamoja na timu mbili za watoto
wadogo wa Kijiji cha Kipandoni na kuahidi kuonyesha nia ya kusaidia
kuwatengenezea Kiwanja watakachokichaguwa ili kiwe na hadhi ya michezo
ya Kitaifa ndani ya Wilaya ya Kaskazini “B”.
Akizungumza
na Wanamichezo hao Mbunge huyo wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi
aliwataka Vijana hao kujiepusha na makundi ya baadhi ya watu
wanaojaribu kuwashawishi wajiingize katika mambo yaliyo nje ya Sekta ya
Michezo.
Balozi
Seif alisema ni vyema kwa vijana hao wakaendelea kuwaamini Viongozi
waliokubali kuwatumikia katika mambo na harakati zao za kila siku hasa
zile za michezo ambazo kwa sasa husaidia kutoa ajira.
Aliwataka
wanamichezo hao kupitia Viongozi wao waangalie utaratibu wa kutafuta
kiwanja kitakachowekewa miundo mbinu ambayo baadaye kitakidhi mahitaji
ya kuchezewa Ligi yenye hadhi ya Kitaifa.
Mapema
Mke wa Mbunge huyo wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi alisema
katika kuunga mkono juhudi za wanamichezo hao alisema ni vyema kwa
wanasoka hao wanzishe utaratibu wa kuanza kuchangia hata kwa kiwango
kidogo ili kuwapa nguvu Viongozi na wafadhili wanaoonyesha nia ya
kuwasaidia.
Mama
Asha alisema Viongozi wa Jimbo hilo watashawishika na kuongeza nguvu
zao kwa Timu ambazo tayari zimeshajikubalisha kujisaidia zenyewe
zikisubiri nguvu za ziada.
Mapema
Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar Wilaya ya Kaskazini “
B” Tongoa Moh’d Hassan alisema Wilaya hiyo bado inakabiliwa na
changamoto kubwa ya ukosefu wa Kiwanja cha soka chenye hadhi
inayokubalika kwa michezo mikubwa.
RAIS KIKWETE AFUNGUA MKUTANO WA VIONGOZI WA KAMATI YA AMANI MKOA WA DAR ES SALAAM
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:27 PM
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akifungua mkutano wa Viongozi wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam
uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Julius
Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya
dini mbalimbali wakimsikiliza kwa makini Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
alipokuwa akiwahutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Viongozi wa
Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam leo. (Picha zote na Freddy Maro)
ZITTO KABWE AZINDUA CHAMA CHA ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPARECY(ACT) DAR ES SALAAM LEO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:13 PM
Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for change and Transparecy (ACT) Anaa
Elisha Akiwashukuru wanachama wote walioshiriki walio kiunga Mkono chama hicho nawaliotoka vyama vingine wakiwemo viongozi na Taasisi Mbalimbali.
Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for change and Transparecy (ACT) Anaa
Elisha, akiwasalimia wanachama kwa Salam ya chama hicho
Kiongizi MKuu wa chama hicho na akiliyekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zitto Kabwe. akizungumza na wanachama Mbalimbali toka Nje na Ndani ya Dar es Salaa katika uzinduzi wa chama hicho na kuwaomba wanachama popote walipo waipigie Kura ya Hapana Katiba Pendekezwa.
Kikundi cha Ngoma ya Asili ya Kutoka Kigoma kwa jina maarufu kwa Mkoa huo wa kigoma inaitwa Usambere ikitoa burudani katika uzinduzi huo
Wanachama wa chama hicho kwa makundi mbalimbali wakiingia katika ukumbi kwa nyakati tofauti
Wafuasi wa Chama hicho wakiwa na mabango wakiingia Ukumbini
Wafuasi wa Chama hicho wakiwa na mabango yenye Ujumbe tofauti wakiingia Ukumbini
Wafuasi wa Chama hicho wakiwa na mabango yenye Ujumbe tofauti wakiingia Ukumbini
Wanakikundi wa kasimbo Asili, toka Mkoa wa Kigoma Kijiji cha Nyarubanda Kataa ya Mkigo Wilaya ya Kigoma wakitoa salam ya Chama hicho wakiwa wanajiandaa kuingia kwa Nyimbo za Ali ya Mkoa wao katika Mkutano wa Uzinduzi wa Mkutano wa Alliance for change and Transparecy (ACT)
Baadhi ya Wafuasi wa Chama hicho wakiingia Ukumbini
Msanii Afande Sele akiwa na wanachama wa Alliance for change and Transparecy (ACT) katika Picha ya pamoja kwenye Uzinduzi wa Chama hicho
Baadhi ya wajumbe na Viongozi wa Chama hicho wakimsikiliza Zitto Kabwe alipo kua akizindua Mkutano wa Chama hicho(wa tatu kushoto) ni Baba wa Kiongizi MKuu
wa chama hicho na akiliyekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zitto Kabwe.,
Msanii wa Makomando Said Christopher akisalimia Viongozi alipopanda juukwaani na mwenzake
Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for change and Transparecy (ACT) Anaa Elisha akisalimiana na
Kiongizi MKuu wa chama hicho na akiliyekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zitto Kabwe mara alipo maliza kuzungumza na wafuasi wa chama hicho
Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for change and Transparecy (ACT) Anaa Elisha akisalimiana na Askofu Mstaafu wa Jimbo la Kigoma Angilikana Gerald Mpango baada ya kuzungumza na Wanachama
Afande Sele akiwa Jukwaani akitumbuiza
Wasanii wa Kikundi cha Makomando wakitoa Burudani, kulia ni fred felix na Said Christopher
Wafuasi wa chama hicho wakijiandikisha na kupatakadi ya Uanacha
Wanachama
Mamia wajitokeza Uzinduzi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Zitto Kabwe akisoma Fomu ya Chama hicho inayomtaka kila mwanacha Ngazi ya juu atangaze Mali zake
Kasimbo Asilia ikitoa Burudani katika Mkutano wa chama cha Alliance for change and Transparecy (ACT) katika
Ukumbi wa Diamondi Jubilee Dar es Sallam leo mara baada ya chama hicho kufanya Uzinduzi
Kasimbo Asili ni Kikundi cha Usambere kutoka Mkoa wa Kigoma katika kijiji cha Nyarubanda Kataa ya Mkigo Wilaya ya Kigoma ikitoa burudani, pichani ukiona wakiruka na kupokezana kwa katika kucheza.
Wanachama Mbalimbali wakifatilia kwa makini katika Mkutano wa Uzinduzi wa chama hicho Dar es Salaam leo katika Ukumbi wa Alliance for change and Transparecy (ACT)
Vikundi mbalimbali Vikitoa maigizo katika Uzinduzi wa Chama hicho
Wanachama wakijipanga wakati Viongozi wa Chama hicho Kitaifa wakitarajia kuingia katika Ukumbi wa Diamondi Jubilee
Wanachama wakijipanga mikono wakati Viongozi wa Chama hicho Kitaifa wakitarajia kuingia katika Ukumbi wa Diamondi Jubilee na baadhi ya wanachama wakipunga mikono kwa kuonyesha alama ya chama chao
(kulia) akiwapungia mikono wanachama alipokua akiingia katika
Ukumbi wa Diamondi Jubilee Dar es Sallam leo (kushoto) ni Kiongizi MKuu
wa chama hicho na akiliyekua Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zitto Kabwe.
Ulipoimbwa wimbo wa Mungu Ibariki.
Wanachama wakiimba Wimbo wa Taifa
.Katibu Mkuu ACT Tanzania Samson Mwigamba akizungumza na wanachama alipokua akifafanua jambo (PICHA NA
KHAMISI MUSSA)
Subscribe to:
Posts (Atom)
0 comments: