Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
AZAM FC ‘WAICHANJA CHANJA‘ MTIBWA SUGAR, WAIGONGA 5-2 CHAMAZI, WAISHUSHA YANGA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:21 AM
Wachezaji wa Azam FC wakishangilia bao lao la tano leo Chamazi
Na Bin zubery
MABINGWA watetezi, Azam FC wamerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara baada ya ushindi mnono wa mabao 5-2 dhidi ya mabingwa wa
zamani, Mtibwa Sugar ya Morogoro Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es
Salaam jioni ya leo.
Ushindi huo, unaifanya Azam FC ifikishe pointi 25 baada ya kucheza
mechi 13, sawa na Yanga SC wanaoangukia nafasi ya pili kwa kuzidiwa
wastani wa mabao.
Hadi mapumziko, tayari Azam FC walikuwa mbele kwa mabao 3-1
yaliyofungwa na mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Kipere Tchetche, kiungo
mzawa Frank Domayo na mpachika mabao wa Burundi, Didier Kavumbangu.
Tchetche, mfungaji bora wa Ligi Kuu msimu miwili iliyopita, alifunga
bao lake dakika ya 19 baada ya kuwahi mpira uliogonga mwamba kufuatia
kipa Said Mohammed kushindwa kuokoa shuti la winga Mganda, Brian
Majegwa.
Domayo akaifungia bao la pili Azam FC dakika ya 26 akimalizia pasi fupi ya Brian Majegwa ndani ya 18.
Mtibwa Sugar ikazinduka dakika ya 34 baada ya kupata bao la kwanza,
lililofungwa na Mussa Nampaka kwa shuti la kushitukiza kufuatia pasi ya
Ally Shomary.
Kavumbangu akaifungia bao la tatu Azam FC akimalizia pasi nzuri ya kiungo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Azam FC ilirudi na moto wake kipindi cha pili na kufanikiwa bao la
pili mapema tu dakika ya 58, Frank Domayo tena akiwainua vitini
mashabiki Uwanja wa Azam Complex, baada ya kuwahi mpira uliotemwa na
kipa Said Mohammed.
Frank Domayo katikati ya wachezaji wa Mtibwa Sugar
Ame Ally ‘Zungu’ akaifungia Mtibwa Sugar bao la pili dakika ya 70
baada ya kupokea pasi ya Abdallah Juma ambaye aliingia muda huo huo
kuchukua nafasi ya Mussa Mgosi.
Kipre Herman Tchetche akaifungia bao la tano Azam FC dakika ya 86 akiunganisha krosi ya beki Shomary Kapombe.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto
Nyoni/John Bocco dk65, Said Mourad, Serge Wawa, Kipre Bolou/Mudathir
Yahya dk55, Kipre Tchetche, Frank Domayo, Didier Kavumbagu/Khamis Mcha
‘Vialli’ dk80, Salum Abubakar na Brian Majwega.
Mtibwa Sugar; Said Mohammed, Andrew Vincent, Majaliwa Mbaga, Ally
Lundenga, Salim Mbonde, Shaaban Nditi, Ramadhani Kichuya, Mussa Nampaka,
Ame Ally, Henry Joseph/Ally Shomary dk33 na Mussa Mgosi/Abdallah Juma.
ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI AMOS MAKALLA WILAYANI HANANG
Naibu Maziri Maji, Amos Makalla (wa pili kulia) na Waziri Ofisi ya Rais
Mahusiano na Mbunge wa Hanang, Dk. Mary Nagu (kulia) wakiwasikiliza
viongozi wa Kijiji cha Ishponga-Hanang mkoani Manyara.
Naibu Waziri Maji, Amos Makalla akipewa matatizo ya mradi wa maji wa
Kijiji cha Ishponga kutoka kwa mbunge wa jimbo la Hanang Dr Mary Nagu
Posted by Richard Mwaikenda at Wednesday, February 11, 2015
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest
Post a Comment
Newer Post Older Post Home
Wanaotembelea Blogu hii
Sparkline 2251359
MATOKEO YA KIDATO CHA PILI
MATOKEO YA KIDATO CHA PILI
BOFYA HAPA KUTAZAMA
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE HAYA HAPA
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2013 HAYA HAPA
Tanzania National Flag
Tanzania National Flag
Time
Dar es Salaam
The Digital Company
The Digital Company
Mtayarishaji:
Mtayarishaji:
Richard Mwaikenda
BONGO HITS
Find more music like this on GongaMx
Blog Archive
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: