Rais Rouhani alipoonana na balozi wa Tanzania, Bw. Mbarouk Nassor Mbarouk
Mheshimiwa Rais pia amesema, kuna nyuga nyingi za kustawisha uhusiano wa Iran na Tanzania kama vile sekta ya madini na nishati na kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuipatia Tanzania uzeofu wake katika masuala mbalimbali.
Kwa upande wake, Balozi Mbarouk ameashiria namna Tanzania inavyolipa umuhimu mkubwa suala la kuimarisha uhusiano wake wa Iran katika sekta tofauti na kusema: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imepiga hatua nzuri katika nyuga nyingi na tofauti; za kisayansi, kiufundi na kiteknolojia hususan sekta na nishati na kwamba anaamini kuwa, Tanzania inaweza kufaidika na uzoefu wa Iran katika mambo tofauti.





0 comments: