RC- KIGOMA AGIZA KIJIJI KIKAGULIWE URAIA WA WANANCHI MKOANI KIGOMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:41 PM
NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA
MKUU wa Mkoa wa Kigoma
Brigedia Jenerari Emanuel Maganga ameviagiza vyombo vya usalama vya hapo,wakague uraia wa
wananchi waishio katika Kijiji Cha Matendo katani humo wilayani Kigoma kutokana
na changamoto ya kugombea ardhi baina ya wakulima na wafugaji,ilihali awali kila kaya walipatiwa hekari 10 ya shughuli hizo.
Akitoa kauli hiyo kijijini humo,katika ziara ya siku moja ya
kukagua miradi ya maendeleo na kuongea na wananchi wa vijiji kadhaa katika
wilaya hiyo,iliyolenga kubaini kero zinazowakabili sambamba na hatua madhubuti
ya kupunguza kero hizo,ambapo katika ziara hiyo ,ilihusisha baadhi ya wakuu wa
idara ya afya,maji,elimu,mkurugenzi Hanji Godigodi na mkuu wa wilaya
hiyo Samson Angana.
Maganga alisema anawasiwasi na uingiaji wa raia kutoka nchi
jirani (BURUNDI) ambao wengi wanajishughulisha na kilimo na ufugaji na kuziagiza
mamlaka husika zichukue hatua za kiutendaji ,kwa kuwa kipindi cha miaka sita
kwa kaya 1505 yenye wakazi 7,400 wafikie hatua ya kutishiana maisha kitendo
kisichokubalika na serikali ya awamu ya tano Rais John Magufuli.
Akifafanua zaidi Maganga alieleza kuwa,kijiji cha matendo
kimegubikwa na ubabe baina ya wananchi na viongozi wa vijiji ,ambapo kila
mkutano wa kijiji lazima kuwe na vurugu ,wananchi kukaidi mikutano ya msingi
hasa ya kupokea tarifa ya mapato na matumizi,ambazo zinaweza zikatatuliwa kwa njia ya mazungumzo
ikiwa wana uchungu wa maendeleo ya kijiji chao.
“isije ikawa kuna raia wa kigeni hapa,tafadhali ukijijua si
raia wa taifa hili,ondoka bwana msituletee vurugu hapa,nagiza vyombo vya usalama na mamlaka
husika waanze mara moja kukagua kaya moja hadi nyingine ,haiwezekani msusie
mikutano ya kijiji kwa kitu cha zaidi ya miaka mitano,mwenyekiti mnamchagua
wenyewe na wote ni chama kimoja sitaki fujo” alisema Mkuu wa mkoa wa kigoma.
Awali Diwani wa Kata ya Matendo Athuman Ntanyagala alifafanua kuwa kuwa ardhi ya matendo imepimwa yote kupitia mpango
wa matumizi bora ya ardhi kuanzia mwaka
1988 hadi 1990 mpango ulikamilika na kipande wanachogombea wakulima na wafugaji
katika ardhi kiliachwa bila matumizi lakini wafugaji walianza kutumia katika
shughuli za ufugaji kiholela na ramani ipo ya kijiji hiki na kushauri itumike
ili kuondoa kero ya uvamizi wa bwawa la Kikombe .
Awali Mwenyekiti wa wafugaji wa hapo Masud Kibenda alidai wafugaji wanahaki ya
kumiliki eneo hilo kwa kuwa walianza shughuli za ufugaji tangu mwaka tangu
mwaka 1990 lakini likaja kundi la wakulima na kuanza shughuli za kilimo katika
bonde la Kikombe hali iliyowafanya wakimbilie katika vyombo vya sheria na
kushinda kesi mara kadhaa na kumuomba mkuu wa mkoa atoe tamko kwa wakulima .
Baadhi ya wananchi wa hapo kusikia tamko la ukaguzi wa uraia
wa kaya moja hadi nyingine wakiomba hifadhi ya majina walisema `kwa hatua
hiyo wananchi wa matendo watabaki
wachache kwa kuwa miongoni mwao wengi ni wakimbizi “.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: