
"SEGERA" LA CUF LAENDELEA, BARAZA KUU SASA LAMFUKUZA UANACHAMA PROFESA IBRAHIM LIPUMBA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:13 AM
CHAMA Cha Wananchi, CUF, kimetangaza kumvua
uanachama wa Chama hicho, Mwenyekiti wake Profesa Ibrahim Haruna Lipumba ikiwa
ni takribani siku tatu tu baada ya Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini
kumrejeshea uenyekiti wake ambao Baraza kuu la uongozi la chama hicho
liliridhia barua yake ya kujiuzulu.
Kwa mujibu wa maafisa wa chama hicho, Baraza
Kuu la Uongozi la CUF lililokutana visiwani Zanzibar juzi na Septemba, 27,
2016, limeamua kumvua uanachama Profesa Lipumba, kwa maelezo kuwa hatua hiyo ni
muhimu katika kukinusuru chama hicho kisisambaratike
Kwa mujibu wa maafisa hao uamuzi wa Baraza Kuu
la Uongozi la Taifa la CUF unatokana na uwezo wake kwa mujibu wa Katiba ya
Chama, Ibara ya 10 (1)(c) limemfukuza uanachama Prof. Ibrahim Lipumba.
Hata
hivyo Profesa Lipumba alikaririwa akisema, kikao cha Baraza Kuu la
Uongozi kilichofanyiak Zanzibar hakikuwa halali kwa vile mwenye mamlaka
ya kuitisha kikao hicho ni Katibu Mkuu wa chama ambaye ni Maalim Seif
Shariff Hamad, ambaye kwa sasa yuko ng'ambo kwenye matibabu. "Kwa vile
Maalim hayupo, mwenye mamlaka ya kuitisha kwa sasa ni Naibu Katibu Mkuu
wa chama (Tanzania Bara), ambaye ni Magdalena Sakaya, lakini mama Sakaya
hakuitisha kikao hicho, hivyo ni kikao batili kwa mjibu wa katiba ya
chama." Alikaririwa Profesa Lipumba Septemba 26, 2016 akisema
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: