DSW lafungua Vituo 33 vya kuwaweza Vijana Kiuchumi na Kijamii
Meneja
Mkazi wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikalilimalojishughulisha na
masuala ya Changamaoto zitokanazo na ongezeko ya Idadi ya Watu Duniani
DSW Bw. Avit Buchwa akizungumza na Afisa Habari kutoka Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Jonas Kamaleki wakati wa Maonyesho ya
Wiki ya Vijana yanayoendelea mkoani Tabora(Picha na Frank Shija, Tabora)
Baadhi
ya Vijana wa DSW wakifuatilia mada wakati wa mdahalo wa vijana kuhusu
Stadi za Maisha ikiwa ni moja ya programu katika kuadhimisha Wiki ya
Vijana ambayo kitaifa inafanyika mkoani Tabora.
Vijana
wa DSW wakiigiza wakati mdahalo wa vijana kuhusu Stadi za Maisha ikiwa
ni moja ya programu katika kuadhimisha Wiki ya Vijana ambayo kitaifa
inafanyika mkoani Tabora.
Vijana wa DSW wakifafanua kuhusu progamu ya Kijana Kwa Kijana inayoendeshwa na Shirika lao kwa kushirikisha vikundi vya vijana.Akizungumza katika Maonyesho ya Wiki ya Vijana yanayoendelea mjini Tabora, Meneja Mkazi wa Miradi wa shirika la DSW nchini Tanzania Bw. Avit Buchwa alisema vituo hivyo vimefunguliwa kwa ajili ya kuwaelimisha vijana kuhusu masuala ya afya ya uzazi ili wabadilike na kuibadilisha jamii. Vituo hivyoni sehemu muhimu kwa vijana kwani wanaweza kutoa mawazo yao kwa uwazi kwa jamii inayowazunguka.
Bw. Buchwa ametaja mikoa ambayo shirika hilo limefungua vituo kuwa ni pamoja na Arusha, Kilimanjaro, Lindi, Mtwara na Manyara. Katika mikoa hiyo vituo hivyo vinawafanya vijana kuwa karibu na jamii husika ambayo inakuwa rahisi kuona na kutambua changamoto zao na kuzishughulikia kikamilifu.
“Vijana wanapata fursa ya kuelimishwa kupitia Vituo vyetu vilivyoko katika maeneo mbalimbali hapa nchini na kwa sasa tumejikita zaidi katika kuelimisha Vijana kujitambua na kutatua changamoto zinazowakabiri kupitia njia ijulikanayo kama kijana kwa Kijana Project”Alisema Buchwa.
Amesema kuwa katika vituo hivyo mtazamo rafiki kuhusu masuala ya afya ya uzazi kwa vijana unatumika katika shughuli zao. Hii imesaidia katika kuvifanya vituo hivyo kuwa na ufanisi mkubwa katika utendaji wa kila siku.
DSW linawawezesha vijana kujitambua na kufanya maamuzi sahihi, kuwajengea uwezo kiuchumi kwa kuwaunganisha na taasisi za fedha kwa ajili ya kupata mikopo ya maendeleo, kuwafundisha vijana stadi za kazi ikiwemo masuala ya uongozi na kuwaandalia ziara za kimafunzo ndani nanje ya nchi ili kuwapatia uzoefu mbalimbali, alisema Bw. Buchwa.
Aidha Buchwa alitoa raia kwa Serikali kupitia Halmashauri zote nchi kuona umuhi wa suala la Afya ya Uzazi kwa Vijana linaingizwa katika mipango yao (CCHP) na kutengea fedha kwa ajili ya utekelezaji ambapo alisema kwa kufanya hivyo kutatimiza haki ya msingi ya Kijana kupata mahitaji ya Kiafya.
Kwa upande mwingine, Katibu wa Kituo cha Vijana Wilaya ya Hai,Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Aziz Salim amesema DSW imewasaidia sana vijana kupata mafunzo mbali mbali kuhusu stadi za maisha pia na kupatiwa pesa mbegu kwa ajili ya miradi ya vijana.
Ameongeza kuwa vijana makini ambao wamepata fursa ya kupata huduma katika Vituo vya Vijana (YEC) vinavyoendeshwa na DSW wamefanikiwa sana kubadilika kimaisha na kuwa na mtazamo chanya wa kimaendeleo.
0 comments: