WAISLAMU WAOMBOLEZA KUFARIKI DUNIA MTUME (S.A.W) NA KUFA SHAHIDI IMAM HASSAN AS
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:08 AM
Iran ya Kiislamu jana usiku ilighariki kwenye
huzuni na majonzi kwa kukumbuka siku aliyoaga dunia Bwana Mtume
Muhammad SAW na aliyokufa shahidi Imam Hassan Al-Mujtaba AS.
Hafla za maombolezo zilifanyika nchini kote katika misikiti,
husaniyyah na maeneo mengine matakatifu ya kidini na zinaendelea pia hii
leo kwa mnasaba wa kukumbuka siku aliyofariki dunia mbora huyo wa
viumbe na mjukuu wake kipenzi.
Hafla za maombolezo kwa mnasaba huo zimefanyika pia katika nchi na maeneo mbalimbali duniani.
Nchini Uingereza mamia ya Waislamu na wapenzi wa Ahlul Bayt (AS) jana
usiku walishiriki kwenye halfa ya maombolezo hayo iliyofanyika katika
kituo cha Kiislamu mjini London.
Hafla hiyo ya maombolezo ilihudhuriwa na Wairan wanaoishi mjini London pamoja na Waislamu wa mataifa mengine.
Katka hafla hiyo Hujjatul Islam Issa Jahangir alizungumzia shakhsia
ya Bwana Mtume Muhammad SAW na kueleza kwamba kutokana na kupambika kwa
akhlaqi njema na mantiki imara, mtukufu huyo alifanikiwa kutekeleza
jukumu la kufikisha ujumbe wa Allah na kuyashinda matatizo na masuala
mbalimbali aliyokabiliana nayo.
Ameongeza kuwa kuamiliana kiadilifu na kwa njia sahihi na watu,
kuchanganyika na watu, kutopenda makuu na kukataa kusifiwa ni miongoni
mwa sifa nyingine muhimu zilizopamba shakhsia yenye nuru, na kushuhudiwa
katika tabia na mwenendo wa Bwana Mtume SAW.
Kwa mnasaba wa kukumbuka kuaga dunia Mtume mtukufu Muhammad
Al-Mustafa SAW pamoja na kufa shahidi Imam Hassan Al-Mujtaba AS na Imam
Ali Ibn Mussa Ridha AS, hafla za maombolezo kwa lugha za Kiarabu,
Kiingereza na Kifarsi zinafanyika kwa muda wa siku tatu katika kituo cha
Kiislamu mjini London, Uingereza.../
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: