MASHAMBULIO YA NDEGE ZA KIVITA ZA SAUDIA YAENDELEA KUUA RAIA WA YEMEN

Watu 19 wameuawa katika mashambulio mapya ya anga yaliyofanywa na ndege za kivita za Saudi Arabia dhidi ya maeneo ya makaazi ya raia nchini Yemen.
Watu 16 wameuawa na wengine 11 wamejeruhiwa wakati ndege za kivita za Saudia ziliposhambulia mji wa Murawa'ah mkoani Al Hudaydah magharibi mwa Yemen.
Ndege za kivita za jeshi la utawala wa Aal Saud zimeshambulia pia mji wa Ad-Durayhami na kuua raia watatu.
Wakati huohuo jeshi la Yemen likishirikiana na vikosi vya kujitolea vya wananchi vimejibu jinai na mashambulio hayo ya wavamizi kwa kushambulia kwa makombora ngome za jeshi la Saudia katika maeneo ya Jizan, Najran na Usair na kufanikiwa kuwaangamiza askari kadhaa wa jeshi hilo.
Maelfu ya raia wameuawa Yemen kutokana na mashambulio ya anga ya Saudia
Kikosi cha makombora cha jeshi la Yemen na wapiganaji wa kujitolea kimeshambulia pia boti za kivita za muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudia  katika pwani ya mji wa Dhabab mkoani Taiz kusini magharibi mwa Yemen na kusababisha hasara kubwa kwa boti hizo.
Aidha ndege moja isiyo na rubani (drone) ya vikosi vamizi vya Saudia ilianguka jana usiku karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Aden kusini mwa Yemen.../

0 comments: