Latest Articles

MAKAMU WA RAIS DKT. NCHIMBI AMJULIA HALI MJANE WA RAIS WA KWANZA WA ZANZIBAR HAYATI SHEIKH ABEID AMANI KARUME

.  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemjulia hali, Mama Fatma Karume,Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, ambaye anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Lumumba Zanzibar.




 

read more

MAKAMU WA RAIS MHE. BALOZI NCHIMBI AMTEMBELEA SAIS MSTAAFU WA ZANZIBAR MHE. AMANI ABEID KARUME

  •    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali, Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Amani Abeid Karume, katika makazi yake, Mbweni - Unguja Zanzibar.




read more

RAIS SAMIA LEO AHITIMISHA TAMASHA LA KIZIMKAZI 2026

 

Kusini Unguja, Zanzibar 

Leo nimehitimisha Tamasha la Kizimkazi 2026, baada ya siku tatu za shangwe, fursa na shughuli mbalimbali zilizolenga kujenga umoja, kukuza fursa za biashara na uwekezaji, kutangaza utamaduni na utalii wetu, pamoja na kufungua miradi ya maendeleo kwa wananchi. Tunatarajia matokeo ya shughuli hizi kuendelea kuonekana hata baada ya tamasha kumalizika.

Ninawashukuru wote walioshiriki na kufanikisha tamasha hili. Ninawasihi tuendelee kushikamana, tudumishe amani, utulivu na usalama wa nchi yetu, kwa kuwa ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wetu.



read more

RAIS DKT. MWINYI: TAMASHA LA KIZIMKAZI NI JUKWAA LA UTAMADUNI, UTALII NA FURSA ZA UWEKEZAJI

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tamasha la Kizimkazi limeendelea kuwa jukwaa muhimu la kutangaza utamaduni, utalii, biashara na fursa za uwekezaji zilizopo Zanzibar, sambamba na kuchochea maendeleo ya wananchi.


Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 12 Agosti 2026, alipokuwa akizindua rasmi Tamasha la Kizimkazi 2026 lenye kaulimbiu “KIZIMKAZI Kumenoga!” katika Mkoa wa Kusini Unguja.


Amepongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono ya kuasisi Tamasha hilo, ambalo limekuwa likichangia kuhifadhi mila na utamaduni, kukuza utalii na kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi.


Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza umuhimu wa kutumia Tamasha hilo kutangaza fursa za uwekezaji katika utalii, uvuvi, mwani na Uchumi wa Buluu, huku Serikali ikiendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na miundombinu ya uzalishaji.


Amesema Tamasha la Kizimkazi linaunga mkono dhamira ya Serikali ya kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Zanzibar kutoka 800,000 hadi milioni 1.5, kupitia matukio maalum ya utalii na utangazaji wa vivutio, utamaduni, vyakula na ukarimu wa Wazanzibari.


Rais Dkt. Mwinyi amewapongeza waandaaji, wadhamini, taasisi za Serikali, Sekta Binafsi, wajasiriamali, wasanii, wanamichezo na wananchi kwa kufanikisha Tamasha la Kizimkazi 2026, akihimiza kuendelea kulitumia kama jukwaa la kufungua fursa mpya za maendeleo.

Tamasha hilo linaendelea hadi tarehe 14 Agosti 2026, ambapo kilele chake kitafanyika katika Uwanja wa Mwehe, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja.

















read more

MWENYEKITI WA CCM TAIFA NA RAIS DKT. SAMIA AKIZUNGUMZA NA WANACHAMA WA MASKANI KATA YA KISONGE, MICHENZANI ZANZIBAR




Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanachama wa Chama hicho katika Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.

Shamra shamra za Mapokezi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.




read more

JKCI YATAKIWA KUENDELEZA KAMBI ZA MATIBABU YA MOYO NCHINI COMORO

 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imetakiwa kuangalia namna ya kupeleka huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini Comoro kutokana na huduma hizo kutopatikana nchini humo.


Rai hiyo imetolewa leo na Balozi wa Tanzania nchini Comoro Mhe. Dkt. Salim Hamad alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt. Peter Kisenge kuona namna ambavyo huduma zinazotolewa na JKCI zinaweza kuwakomboa wananchi wa Comoro.


Dkt. Hamad alisema baada ya JKCI kuweka kambi maalumu ya matibabu ya moyo katika kisiwa cha Anjouan kilichopo nchini Comoro uongozi wa kisiwa hicho umeitaka JKCI kuingia mkataba nao wa kuendelea kufanya kambi za matibabu jambo ambalo linaonesha umahiri wa huduma zinazotolewa na wataalamu wa JKCI.


“Nilifurahi nilipokutana na uongozi wa kisiwa cha Anjouan na kuniomba niwajulishe kuwa wanataka tuingie nao mkataba wa kufanya kambi za matibabu, hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu katika kutoa huduma bingwa za matibabu ya moyo”, alisema Dkt. Hamad.


Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema uhitaji wa huduma za matibabu ya moyo nchini Comoro ni mkubwa kutokana na mwitikio uliokuwepo wakati wa kambi ya matibabu iliyofanyika mwezi Oktoba mwaka jana katika kisiwa cha Anjouan.


“Tunaandaa mkakati wa kuitangaza JKCI nchini Comoro ili tuweze kuwasaidia wananchi wa Comoro kufahamu zaidi huduma tunazozitoa na kuwapunguzia adha ya kuzifuata huduma hizi mbali na nchi ya Comoro”, alisema Dkt. Kisenge.



read more

IAEA KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUSAFIRISHA MABAKI YA VYANZO VYA MIONZI ORCI

  

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo, akiongoza kikao na wawakilishi wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kupitia Institute of Isotopes Co. Ltd. ya Hungary pamoja na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) cha kujadili taratibu za usafirishaji wa mabaki ya vyanzo vya mionzi vilivyotumika katika matibabu ya saratani.
Gábor Kaszás kutoka Institute of Isotopes Co. Ltd. ya nchini Hungary akichangia mada katika kikao cha majadiliano kuhusu taratibu za usafirishaji salama wa mabaki ya vyanzo vya mionzi vilivyotumika katika Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCi kwa ajili ya matibabu ya saratani.
Wataalamu kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) wakifuatilia kwa makini majadiliano wakati wa kikao cha kujadili  taratibu za usafirishaji salama wa mabaki ya vyanzo vya mionzi vilivyotumika katika matibabu ya saratani.



12/08/2026 Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), kwa kushirikiana na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC), limekubaliana na Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) kuanza mchakato wa kusafirisha mabaki ya vyanzo vya mionzi vilivyomaliza matumizi yake katika mashine za matibabu ya mionzi kwa wagonjwa wa saratani.



Makubaliano hayo yamefikiwa leo jana katika kikao kilichowakutanisha Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dkt. Diwani Msemo, ujumbe wa IAEA kupitia kampuni ya Institute of Isotopes Co. Ltd kutoka nchini Hungary, ukiongozwa na Mr. Gábor Kaszás, pamoja na wajumbe kutoka TAEC.



Kwa mujibu wa makubaliano hayo, mabaki ya vyanzo hivyo vya mionzi yatasafirishwa kwenda nchini Hungary kwa ajili ya kuhifadhiwa na kufanyiwa mchakato wa kuyahuisha kwa matumizi mengine.


Vyanzo hivyo aina ya Cobalt vilitumika katika mashine za tiba ya mionzi kwa vipindi mbalimbali kuanzia mwaka 2008, huku vingine vikitumika katika vipindi vya mwaka 2014 hadi 2020 na mwaka 2025. Baada ya nguvu ya vyanzo hivyo kupungua na kutofikia kiwango kinachohitajika kwa ajili ya matibabu, ORCI ilinunua vyanzo vipya ili kuhakikisha huduma za matibabu ya saratani zinaendelea kutolewa kwa kuzingatia viwango vya ubora.



Mchakato wa kuondoa na kusafirisha mabaki ya vyanzo vya mionzi ni utaratibu wa kawaida unaotekelezwa kwa kushirikisha mamlaka husika za ndani, TAEC na IAEA kwa kuzingatia taratibu za usalama katika usimamizi wa vyanzo vya mionzi.



Hatua hiyo inalenga kuhakikisha mabaki ya vyanzo vya mionzi vilivyomaliza matumizi yake yanadhibitiwa na kusimamiwa kwa usalama huku vyanzo vipya vikiendelea kutumika katika kutoa huduma za matibabu ya mionzi kwa wagonjwa wa saratani.
read more