Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.
Latest Articles
MBUNGE KIGOMA MJINI CLAYTON CHIPANDO ATAKA KITENGO CHA ELIMULISHE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:52 AM Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 leo jijini Dodoma
**************************************************************************************************************************
Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.
Mhe. Chipando ameyasema hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27
"Mhe. Mwenyekiti mimi nimekula Ugali kwa miaka 35, lakini Leo kila ukiingia mtandaoni utakutana na matangazo mbalimbali yanayotumika kuelimisha watu juu ya utaratibu wa matumizi ya chakula" amesema Mhe. Chipando
Mhe. Chipando amesema katìka siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la watoa huduma, ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakitoa elimu kuhusu lishe na kuwaweka wananchi kwenye mtanziko wa nini wale na kiwango gani.
Kwa upande wake Mhe. Khamis Ali Vuai Mbunge wa Jimbo la Mkwajuni (CCM) mkoani Kaskazini UngujaMbunge aliyeomba kutoa taarifa wakati wa Mchango huo, aliliambia Bunge kuwa taifa la India ni moja ya Taifa lililoweka Utaratibu wa nani atatoa elimu ya Afya, hivyo kama Taifa tuone kama kitu muhimu, jambo lililokubaliwa na Mchangiaji.
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea na Uchangiaji wa Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52, kwa mwaka wa fedha 2026/27 iliyowasilishwa Mei 11, 2026 Bungeni na Waziri wa Afya Mhe Mohamed Mchengerwa na kuomba kuidhinishiwa kiasi cha shilingi Trilioni 1.8 kwa ajili yakutekeleza vipaumbele 11.M
read more
Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.
JKCI YAWAGUSA WANANCHI NJOMBE KUPITIA KAMPENI YA "JUWA NAMBA ZAKO"
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 7:43 AM

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Modesta Nyagawa akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mkazi wa Njombe aliyefika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinayotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
Mtaalamu wa vipimo vya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sven Kamugisha akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Njombe aliyefika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinazotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
**********************************************************************************************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imewahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara kupitia kampeni ya “Jua Namba Zako” ili kubaini mapema vihatarishi vya magonjwa ya moyo na kupata matibabu kwa wakati.
Rai hiyo imetolewa leo na Daktari wa Taasisi hiyo Samweli Mbilinyi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma za upimaji wa moyo zinazotolewa na JKCI kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kinachofanyika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe.
Dkt. Mbilinyi alisema wananchi wengi bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu magonjwa ya moyo jambo linalosababisha baadhi yao kuishi na matatizo hayo bila kujitambua hadi wanapofika hospitalini wakiwa na matatizo mengine.
Alitoa mfano wa mgonjwa aliyefika katika upimaji huo ambao huduma za upimaji wa magonjwa mbalimbali zinatolewa kwajili ya matatizo ya miguu lakini baada ya kupimwa alibainika kuwa na shinikizo kubwa la damu lililozidi kiwango cha kawaida hali iliyowalazimu wataalamu wa JKCI kumfanyia vipimo vya moyo na kuanza matibabu mara moja.
“Tumegundua wananchi wengi hawajawahi kupima afya ya moyo wala kufahamu viwango vyao vya afya. Kupitia kampeni ya Jua Namba Zako tunawahamasisha wananchi wajitokeze kupima ili kujua hali zao mapema na kupata tiba stahiki”, alisema Dkt. Mbilinyi.
Dkt. Mbilinyi alisema katika upimaji unaoendelea wamebaini watu wengi wenye shinikizo la juu la damu na matatizo ya moyo ambao hawakuwahi kufanyiwa vipimo vya moyo wala kujua hali zao za afya.
Aliishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuwezesha upatikanaji wa dawa bure kwa wananchi wanaobainika kuwa na matatizo mbalimbali ya afya ikiwemo magonjwa ya moyo katika upimaji huo.
“Ninawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kupima afya zao. Watakaobainika kuwa na changamoto watapatiwa ushauri wa kitaalamu, tiba, dawa bila malipo na rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI”, alisisitiza.
Kwa upande wao wananchi waliopata huduma hizo walieleza kufurahishwa na ujio wa wataalamu wa JKCI mkoani Njombe huku wakisema umewasaidia kupata huduma karibu na maeneo yao na kupunguza gharama za kusafiri kwenda Dar es Salaam.
Mmoja wa wananchi hao Farida Fredrick kutoka kijiji cha Ihalula, alisema alifika kupata huduma baada ya kusikia madaktari wa JKCI wanatoa huduma Njombe.
“Mimi ni mgonjwa wa moyo na huwa nahudhuria kliniki ya JKCI Dar es Salaam. Niliposikia madaktari wako hapa Njombe nikaona nitumie nafasi hii kupata huduma karibu na nyumbani, huduma ni nzuri sana na wananchi wengi wajitokeze kupima”, alisema Farida.
Joseph Mwakalonge mkazi wa Njombe mjini alisema alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya kichwa pamoja na uchovu wa mara kwa mara bila kufahamu chanzo chake lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi alibainika kuwa na shinikizo la juu la damu na kupewa matibabu.
“Naishukuru sana JKCI kwa kuleta huduma hizi karibu yetu. Sikuwahi kujua kama nina tatizo la presha kubwa kiasi hiki lakini leo nimepata elimu, vipimo na dawa kitu ambacho kitanisaidia kuutunza moyo wangu mapema ili usipate madhara zaidi”,alisema Mwakalobe.
Naye Rehema Mlowe mkazi wa Makambako alisema alikuwa hajawahi kupima afya ya moyo tangu alipogundulika kuwa na changamoto ya presha miaka miwili iliyopita lakini ujio wa madaktari wa JKCI umempa nafasi ya kufanyiwa uchunguzi wa kina na kupata ushauri wa namna ya kuishi kwa kufuata mtindo bora wa maisha.
“Nimepata huduma nzuri na wataalamu wanatoa elimu kwa upendo mkubwa. Ninawaomba wananchi wenzangu watumie fursa hii kuja kupima afya zao mapema kabla hali haijawa mbaya”, alisema Rehema.
Katika upimaji huo JKCI inatoa huduma za uchunguzi wa awali wa magonjwa ya moyo, uchunguzi wa shinikizo la damu, kipimo cha kuangalia uwingi wa sukari kwenye damu, kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi, elimu ya lishe bora na mtindo sahihi wa maisha, elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa madaktari bingwa wa moyo.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli Mbilinyi akimpa vipeperushi vya elimu ya magonjwa ya moyo Dorah Kachele ambaye ni Mkurugenzi wa vipindi na maudhui wa Kings FM ya mjini Njombe alipofika katika Hoteli ya Agreement kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinayotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli Mbilinyi akimpa vipeperushi vya elimu ya magonjwa ya moyo Dorah Kachele ambaye ni Mkurugenzi wa vipindi na maudhui wa Kings FM ya mjini Njombe alipofika katika Hoteli ya Agreement kwaajili ya kupata huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinayotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
read more
MAAFISA UTAWALA NA RASILIMALIWATU 316 NCHINI WAPIMWA MAGONJWA YA MOYO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:27 AM Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nadia Zuberi akimpima shinikizo la damu (BP) Afisa Rasirimali Watu aliyefika katika kliniki ya JKCI wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.
Daktari wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adda Justine akimpa ushauri Afisa Rasirimali Watu aliyefika katika kliniki ya JKCI wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.
Baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
.............................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................
Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 nchini wamefanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kuwawezesha kufahamu namba zao na kuwapa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo.
Uchunguzi huo umefanyika kwa siku tatu wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.
Akielezea kuhusu mwitikio wa maafisa hao kufanya uchunguzi wa afya Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete alisema mwitikio umekuwa mkubwa na wenye tija kwa maafisa Utawala na Rasirimali Watu nchini.
“Baada ya kuwafanyia uchunguzi wa afya baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu tumewapa rufaa kufika katika Hospitali zetu kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na kuona viashiria ambavyo vinahitaji uchunguzi zaidi”, alisema Dkt. Salehe
Dkt. Salehe alisema inapotokea fursa kama hiyo ya kupima afya eneo la kazi ni vizuri watumishi wakaitumia vizuri kwani wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi wanakosa muda wa kufika hospitali kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.
“JKCI tumekuwa mstari wa mbele kuwafikishia watumishi wa umma na sekta binafsi huduma za uchunguzi wa afya wakati wa mikutano mbalimbali lakini pia hata kuwafuata katika maeneo yao ya kazi, jitihada zote hizi tunazofanya tunataka kuhakikisha kuwa tunailinda jamii na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo”, alisema Dkt. Salehe
Nao maafisa Utawala na Rasirimali Watu walioshiriki katika mkutano huo wameiomba JKCI kuendela kutoa elimu ya magonjwa ya moyo ili kuliokoa taifa la Tanzania na changamoto ya magonjwa hayo.
Maafisa hao walisema Serikali ya Tanzania ina mchango mkubwa katika kuhakikisha watu wake wanakuwa salama ndio maana imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya na kuhakikisha elimu kuhusu kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali inawafikia wananchi.
read more
Uchunguzi huo umefanyika kwa siku tatu wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.
Akielezea kuhusu mwitikio wa maafisa hao kufanya uchunguzi wa afya Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete alisema mwitikio umekuwa mkubwa na wenye tija kwa maafisa Utawala na Rasirimali Watu nchini.
“Baada ya kuwafanyia uchunguzi wa afya baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu tumewapa rufaa kufika katika Hospitali zetu kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na kuona viashiria ambavyo vinahitaji uchunguzi zaidi”, alisema Dkt. Salehe
Dkt. Salehe alisema inapotokea fursa kama hiyo ya kupima afya eneo la kazi ni vizuri watumishi wakaitumia vizuri kwani wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi wanakosa muda wa kufika hospitali kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.
“JKCI tumekuwa mstari wa mbele kuwafikishia watumishi wa umma na sekta binafsi huduma za uchunguzi wa afya wakati wa mikutano mbalimbali lakini pia hata kuwafuata katika maeneo yao ya kazi, jitihada zote hizi tunazofanya tunataka kuhakikisha kuwa tunailinda jamii na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo”, alisema Dkt. Salehe
Nao maafisa Utawala na Rasirimali Watu walioshiriki katika mkutano huo wameiomba JKCI kuendela kutoa elimu ya magonjwa ya moyo ili kuliokoa taifa la Tanzania na changamoto ya magonjwa hayo.
Maafisa hao walisema Serikali ya Tanzania ina mchango mkubwa katika kuhakikisha watu wake wanakuwa salama ndio maana imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya na kuhakikisha elimu kuhusu kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali inawafikia wananchi.
RAIS SAMIA AAGIZA MPANGO MAALUM WA KUWAINUA WAFUNGWA WENYE UJUZI WANAPOREJEA URAIANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:48 PMNa Mwandishi wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Magereza kufanya tafiti za kina zitakazowezesha kuanzishwa kwa mfuko maalumu wa kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanaporejea uraiani, ili waweze kujitegemea kiuchumi na kuepuka kurejea katika makosa ya uhalifu.
Rais Samia amesema hatua hiyo ni sehemu ya kuimarisha mfumo wa urekebishaji nchini kwa kuhakikisha wafungwa wanaopata mafunzo ya ufundi na stadi mbalimbali wakiwa magerezani wanapata mazingira rafiki ya kuanza maisha mapya baada ya kutumikia vifungo vyao.
Ametoa maelekezo hayo leo Mei 9, 2026, wakati akihutubia hafla ya kuhitimisha Mafunzo ya Uongozi Ngazi ya Juu Kozi Na. 28 pamoja na Uongozi Daraja la Pili Kozi Na. 48 iliyofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA), Ukonga jijini Dar es Salaam.
Katika hotuba yake, Rais Samia alisema wafungwa wengi wamekuwa wakipata ujuzi muhimu wakiwa magerezani kupitia mafunzo mbalimbali ya ufundi stadi, ushonaji, kilimo, useremala na shughuli nyingine za uzalishaji, lakini changamoto kubwa imekuwa ni ukosefu wa mtaji au mifumo ya kuwawezesha kuanza maisha mapya wanapotoka gerezani.
Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kutasaidia kuwapa nguvu ya kuanza upya kwa kutumia maarifa na taaluma walizozipata, jambo litakalosaidia kupunguza matukio ya kurudia makosa pamoja na kuongeza mchango wao katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.
“Tunapaswa kuwapa nafasi ya pili ya maisha. Kama wamejifunza kazi na stadi mbalimbali wakiwa magerezani, basi wanapotoka wanahitaji kuungwa mkono ili waweze kujitegemea na kuwa sehemu ya maendeleo ya nchi,” alisisitiza Rais Samia.
Aidha, amemuelekeza Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, Jeremiah Katungu kushirikiana na wadau mbalimbali kufanya tafiti za sera na mifumo bora itakayowezesha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi.
Rais Samia pia alipongeza Jeshi la Magereza kwa kuendelea kuboresha mfumo wa urekebishaji wa wafungwa kwa kuwapatia elimu, maadili na stadi za maisha zinazowaandaa kuwa raia wema baada ya kumaliza vifungo vyao.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, maafisa wa Jeshi la Magereza pamoja na washiriki wa mafunzo waliohitimu kozi hizo za uongozi.
read more
Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge tuzo ya mdhamini mkuu wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Afisa Utawala Adila Lugamara wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge tuzo ya mtoa mada wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
wakifuatilia mada zinazoendelea katika Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Baadhi ya Maafisa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Utawala na RasilimaliWatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Picha na JKCI
read more
Picha na JKCI
WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA JUMUIYA YA WAFANYA BIASHARA KARIAKOO 2026
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:42 AMWaziri wa Viwada na Biashara Judith Kapinga akizungumza wakati
wa Mkutano Mkuu 2026 wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo leo Aprili
25,2026.
Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza wakati
wa Mkutano Mkuu 2026 wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo leo Aprili
25,2026 na kuwapongeza wafanya biashara kwa ulipaji mzuri wa kodi
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo (JWK) Severini
Mushi akimkabidi Tuzo Waziri wa Viwada na Biashara Judith Kapinga leo Aprili
25,2026. Wakati wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya 2026 uliofanyika Jijini Dar es
Salaam.
Subscribe to:
Posts (Atom)













































