




Latest Articles
KATIBU MKUU CCM AONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI KISIWANDUI, ZANZIBAR
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:36 AM Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, akiongoza Kikao cha Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kilichofanyika katika Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui, Zanzibar, leo Jumanne, tarehe 28 Julai 2026
RAIS SAMIA AONGOZA SEMINA ALEKEZI KWA MAWAZIRI, NAIBU MAWAZIRI NA MAKATIBU WAKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUMGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA ZANZIBAR
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:36 AMLeo nimekutana na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Mhe. Nicole Providoli, ambapo tumebadilishana mawazo kuhusu namna ya kuendeleza ushirikiano katika kuimarisha sekta ya afya kwa manufaa ya wananchi wa Zanzibar.
Nimemueleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuwekeza katika kujenga mifumo imara ya afya, kuboresha ugharamiaji wa huduma za afya na kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote ili kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora, salama na kwa usawa.
Pia nimetoa shukrani kwa Serikali ya Uswisi kwa ushirikiano wake wa muda mrefu katika sekta ya afya, hususan katika utafiti, mapambano dhidi ya malaria na kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya.
Ninaamini ushirikiano huu utaendelea kuleta matokeo chanya katika kuboresha afya na ustawi wa wananchi wetu, sambamba na kuijenga Zanzibar yenye jamii yenye afya na maendeleo endelevu.
Ninaipongeza Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania (Twiga Stars), kwa kuanza vyema michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026 nchini Morocco kwa ushindi dhidi ya Timu ya Taifa ya Wanawake ya Afrika Kusini, (Banyana Banyana).
Ninaungana na Watanzania wote kuitakia kila la kheri Twiga Stars inapoendelea kupeperusha bendera ya Taifa letu katika michezo inayofuata.
Endeleeni kupambana kwa moyo huo huo, mkionesha uzalendo, nidhamu na ari ya ushindani inayolitangaza vyema Taifa letu.
read more
WANANCHI WAHIMIZWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUPIMA SARATANI MARA KWA MARA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:57 PMMkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo akizungumza na waandishi wa habari jana kuhusu huduma mbalimbali za uchunguzi na matibabu ya saratani zinazotolewa na taasisi hiyo pamoja na uwekezaji uliofanywa na Serikali.
23/7/2027 Wananchi wametakiwa kujenga utamaduni wa kupima saratani mara kwa mara ili kama watagundulika kuwa na ugonjwa huo waweze kupata matibabu mapema kwani saratani ikigundulika mapema inatibika.
Wito huo umetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) Dkt. Diwani Msemo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma mbalimbali za uchunguzi na matibabu ya saratani zinazotolewa na taasisi hiyo pamoja na uwekezaji uliofanywa na Serikali.
Dkt. Msemo ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya saratani alisema ugonjwa huo kama yalivyo magonjwa mengine unatibika iwapo utabainika katika hatua za awali na mgonjwa kupata matibabu sahihi kwa wakati.
“Matibabu ya Saratani ni tofauti na matibabu ya magonjwa mengine yasiyo ya kuambukiza, iwapo mgonjwa atabainika mapema kuwa na tatizo atatibiwa na kupona na kuendelea na maisha yake ya kawaida bila ya kutumia dawa”, alisema Dkt. Msemo.
Alisema zipo aina mbalimbali za Saratani, ikiwemo Saratani ya tezi dume na kuwataka wanaume wenye umri wa miaka 45 na kuendelea kujitokeza kupima ugonjwa huo.
Kwa mujibu wa Dkt. Msemo baadhi ya wanaume huogopa kupima Saratani ya tezi dume kutokana na imani potofu kuwa uchunguzi wake hufanywa kwa njia isiyo rafiki.
Alisema uchunguzi wa awali unaweza kufanyika kwa urahisi kama vile kupima maralia na iwapo kutabainika kuwa na viashiria vya ugonjwa huo, mgonjwa atafanyiwa vipimo vingine vikiwemo vya ultrasound au CT scan kulingana na ushauri wa daktari.
“Kila mwanaume ana tezi dume ambayo ipo karibu na njia ya mkojo. Dalili kama kukojoa kwa shida zinaweza kuashiria uwepo wa uvimbe unaozuia mkojo kupita. Hata hivyo uvimbe huo si lazima uwe wa saratani ndiyo maana uchunguzi wa mapema ni muhimu kufanyika”, alisema Dkt. Msemo.
Daktari huyo bingwa wa magonjwa ya saratani alisema baadhi ya wagonjwa huchelewa kufika hospitalini kupata matibabu kwa kutegemea tiba mbadala hii ni kutokana na imani potofu waliyonayo kuhusu matibabu ya Saratani.
Alisema kuchelewa huko kunawafanya baadhi ya wagonjwa kufika hospitalini wakiwa katika hatua za tatu au nne za ugonjwa hali inayoweza kufanya matibabu kuwa magumu zaidi.
Dkt. Msemo alisema ORCI inaendelea kutoa elimu kwa wananchi pamoja na huduma za uchunguzi wa Saratani kwa kufanya kambi mbalimbali za uchunguzi wa ugonjwa huo.
Aliwashukuru waandishi wa habari kwa ushirikiano wao katika kuhakikisha jamii inapata elimu sahihi kuhusu ugonjwa huo.
WATUHUMIWA WA MAKOSA YA MAUAJI WATAFUTWA NA POLISI SONGWE.
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 12:24 PMRAIS SAMIA AZINDUA UJENZI WA RELI YA SGR YA TABORA - KIGOMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 11:59 AMRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) mkoani Kigoma leo, tarehe 20 Julai 2026.
Mradi huo unatarajiwa kuboresha usafiri na usafirishaji wa abiria pamoja na mizigo, kuimarisha biashara, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Kigoma na maeneo ya ukanda wa Magharibi.
read more
HABARI ZILIZOPEWA UZITO WA JUU KATIKA MAGAZETI YA JULAI 20,2026
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:44 PM
Subscribe to:
Posts (Atom)




























