Latest Articles

TAASISI YA MOYO (JKCI) YAIBUKA KIDEDEA MFANYAKAZI BORA 2024

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akimkabidhi cheti cha pongezi Afisa Muuguzi Mkuu Msaidizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Robert Yeyeye kwa kuwa mfanyakazi bora  wa  mwaka 2024.
 

read more

KUNDI LINGINE LENYE WANANCHI 564 LAHAMA HIFADHI YA NGORONGORO.

 Na Mwandishi wetu, Ngorongoro.


Zoezi la wananchi wanaoishi ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kujiandikisha na kuhama kwa hiari limepamba moto ambapo leo tarehe 28 Aprili, 2024 jumla ya Kaya 105 zenye wananchi 564 na mifugo 1,540 zimehama katika hifadhi ya Ngorongoro kwenda Kijiji cha Msomera, Simanjiro, Meatu na Monduli.

Kwa mujibu wa Meneja mradi wa kuhamisha wananchi wanaojiandikisha kuhama kwa hiari, Afisa Uhifadhi Mkuu Florah Assey, kati ya kaya hizo 105 zenye wananchi 564 wanaohama, kaya 96 zenye watu 520 na mifugo 1,424 zinahamia Kijiji cha Msomera huku kaya 9 zenye watu 44 na mifugo 116 zikihamia wilaya za Simanjiro mkoani Manyara, Meatu Mkoani Simiyu, Monduli mkoani Arusha na Dakawa Mkoani Morogoro.

Assey amebainisha kuwa zoezi la kuelimisha, kuandikisha na kuthaminisha mali za wananchi linaendelea ndani ya hifadhi hiyob ambapo kila kaya inayojiandikisha mkuu wa kaya na wategemezi wake hukabidhiwa nyumba yenye vyumba vitatu katika kiwanja chenye ukubwa wa ekari 2.5, shamba la ekari tano kwa ajili ya kilimo huku maeneo waliyohamia yakiwa na miundomnibu yote muhimu ya kijamii.

Akiaga kundi hilo kwa niaba ya Serikali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro Bw. Murtallah sadiki mbillu amewasihi wananchi hao wanapofika Msomera kutoruhusu ndugu waliowaacha Ngorongoro kuhamia Msomera bila kufuata utaratibu wa kiserikali unaohusisha kupata stahiki zao zote kwa mujibu wa sheria.

“Naomba nisisitize kuwa mwananchi hapaswi kuhamia msomera bila utaratibu na kwenda kuishi kwa ndugu kwa nguvu wakati akifuata utaratibu Serikali inampa stahiki zake zote kwa mujibu wa sheria, tumepokea changamoto ya mwananchi aliyehamia Msomera bila utaratibu na alipoona mazingira ni mazuri akavamia kwenye Nyumba iliyojengwa ambayo hajakabidhiwa kwa utaratibu, hivyo ni vizuri kufuata sheria na utaratibu” aliongeza Mbillu.

Amewaasa wananchi hao kuwa inapotokea Changamoto yoyote wanapokuwa Msomera au maeneo mengine wanayohamia kuwasiliana na Viongozi wa Serikali katika maeneo hayo badala ya kukimbilia kwenye mitandao ya kijamii au baadhi ya Vyombo vya habari.

Mkurugenzi huyo amewahakikishia wananchi wanaohama kuwa Serikali inafanya zoezi hilo kwa lengo na kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwajengea miundombinu wezeshi nje ya hifadhi na kwamba zoezi hilo litaendelea kutekelezwa kwa kuzingatia misingi ya Sheria kanuni, taratibu na haki za binadamu.

Kwa upande wake kaimu Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Victoria Shayo ameeleza kuwa kwa sasa vijiji vyote ndani ya hifadhi vimefikiwa na timu za uandikishaji na kufafanua kuwa vitendea kazi ikiwemo Vishkwambi vya kuandikishia zaidi ya 50 na magari vimeongezwa ili kuongeza kasi ya uandikishaji kutokana na wananchi wanaotaka kuhama kuwa mkubwa.

“Nawahakikishia kuwa zoezi hili litaendea kufanyika kwa kasi na kuzingatia ufanisi kwa kuwa timu zetu za uhamasishaji, uandikishaji, tathmini na kuhamisha zina ari na utayari mkubwa na zinajitoa kufanya kazi ili kuisaidia Serikali kuboresha Maisha ya wananchi” alisisitiza kaimu kamishna.



read more

RAIS WA JAMHURI YA SOMALIA MHE. HASSAN MOHAHADAIPONGEZA TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE (JKCI)

 

Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akisaini kitabu cha wageni Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud tibabu  ya moyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge.

    Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud  akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge. mara alipoitembelea Taasisi hiyo kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo. Wa katikati anae shuhudia ni Waziri wa Afya Nchini Tanzania Mhe. Ummy Mwalimu wakimo viongozi wengine wa Taasisi hiyo.
  Waziri wa Afya  Nchini Tanzania Ummy Mwalimu akizungumza katika chumba cha Cathlab katika Taasisi ya Moyo (JKCI) na Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud 
  Rais wa Jamuhuri ya Somali akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jalaya Kikwete mara baada ya kuitembele na kujionea Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Hassan Suluhu.

  Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akiwapungia mkono Viongozi na Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete mara baada ya kujionea mtambo wa Cathlab ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu  ya moyo. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
 

Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud aipongeza JKCI


Na Mwandishi Maalumu -  Dar es Salaam


27/4/2024 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud amewapongeza wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa huduma nzuri wanayoitoa ya kuokoa maisha ya watu wenye matatizo ya moyo.


Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud  alizitoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea Taasisi hiyo  (JKCI) kwaajili ya kuona  huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.


Akiwa katika Taasisi hiyo Mhe. Rais Mahamud alitembelea maeneo mbalimbali  ya JKCI ikiwa ni pamoja na mtambo wa Cathlab ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu  ya moyo.


Akizungumzia kuhusu ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema JKCI ni moja ya Taasisi inayoongoza katika nchi za Afrika Mashariki na kati katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.


Dkt. Kisenge alisema Rais Mohamud alitembelea Taasisi hiyo kwaajili ya  kuona namna ambavyo nchi ya Somalia itawapeleka wagonjwa wa moyo JKCI kupata  tiba ya matibabu ya moyo.


“Nchi ya Somalia inawapeleka wagonjwa wengi  wa moyo kwenda kutibiwa katika nchi za India, Ulaya na Marekani  wakati huduma hii inapatikana nchini Tanzania, na ukiangalia nchi hizi ziko karibu hivyo basi itakuwa ni rahisi kwao kuwaleta wagonjwa kuja kutibiwa hapa kwetu”.


“Kuja kwa wagonjwa hawa kutaisaidia nchi yetu kukua kiuchumi kwani pesa zitakazopatikana zitawafikia watu wengi ikiwemo wamiliki wa hoteli ambako wagonjwa watalala pamoja na wafanyabiashara watakaowauzia vyakula na mahitaji mengine”, alisema Dkt. Kisenge.


 Dkt. Kisenge alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzidi kuimarisha mahusiano na nchi za nje ndiyo maana watu wengi wanakuja kuwekeza hapa nchi hata Taasisi hiyo imekuwa ikiwapokea  wageni mbalimbali kutoka nchi za nje.


Akiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud pamoja na ujumbe wake aliambata na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.

read more

BENKI YA CRDB YAKABIDHI MADARASA YA SEKONDARI KILOLO

 
Benki ya CRDB kupitia sera yake ya uwekezaji kwa jamii, Aprili 24 - 25, 2024 ilikabidhi madarasa mawili katika Shule ya Sekondari Kikilo na madarasa mengine mawili katika Shule ya Msingi Isabe zote za wilayani Kondoa, mkoa wa Dodoma yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki hiyo.

Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.

Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.

Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay wakiwa pamoja na viongozi wengine pamoja na Wanafunzi katika moja ya madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 katika Shule ya Msingi Isabe, iliyopo katika kijiji cha Bukuru, Wilayani Kondoa, katika hafla  iliyofanyika Aprili 25, 202.
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi (wanne kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay (katikati) akiwa pamoja na viongozi wengine wa Benki ya CRDB pamoja na wa Halmashauri ya Kondoa wakiwa katika picha ya paamoja na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kikilo, muda mfupi baada ya kukaidhi madarasa mawili katika shule hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt, Ally Laay akizungumza wakati wa hafla kukaidhi madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya CRDB yenye thamani ya shilingi Milioni 40 kwa uongozi wa Halmashauri ya Kondoa.












read more

AGENDA YA KUTOKOMEZA MALARIA IWE YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYA MAAMUZI

 Na WAF, TABORA


Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameziasa Kamati za Ulinzi na Usalama nchini kuona umuhimu wakuifanya ajenda yakutokomeza Malaria iwe yakudumu kwenye vikao vya maamuzi.

Dkt. Mollel ameyasema hayo leo, Aprili 25, 2024 akiwa amemwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwenye kilele cha Siku ya Malaria Duniani iliyofanyika mkoani Tabora na kusema kuwa kama nchi imeendelea kupiga hatua katika vita hivyo ikilinganishwa na miaka zaidi ya ishini iliyopita ambapo maambuki na vifo vya Malaria vilikuwa kati ya asilimia 45 hadi 50.

Aidha Dkt. Mollel amesema azma ya Serikali ni kufikia asilimia 3.5 ifikapo 2025 na kuwa na ziro Malaria 2030 huku akisisitiza kwa kusema itafikiwa endapo juhudi za Makusudi zitafanywa kwa ushirikiano baina ya Serikali na wadau

"Leo tunazungumza asilimia 8.1 kama nchi lakini miaka ya 1998, tulikuwa na kiwango cha juu sana, hivyo ili tuweze kufikia adhma yakumaliza kabisa malaria ifikapo 2030 kila mmoja wetu anawajibu wakufanya" amesema Mollel.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI Samsoni Maella, amesema Utumiaji wa Mifumo ya GoTHOMIS na FFARS imekuwa chachu ya kukusanya takwimu sahihi kwa ajili ya ngazi ya maamuzi, hali iliyochangia kufanya maamuzi sahihi kutokana na kuwa na takwimu sahihi.

"Kama Ofisi ya Rais TAMISEMI, tumefanikiwa kuimarisha miundo mbinu ya Afya na Rasilimali watu mathalani miaka mitatu nyuma tulikuwa na Hospitali za Wilaya 77 leo hii tunazo 177 hizi zimechochea sana uimarishaji wa huduma” amesema Mahela.

Naye Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI Dkt. Hamis Kigwangala ametoa wito kwa serikali na wadau kuongeza afua za kutibu watoto Shuleni, pia wafike maeneo ya Migodi, Mashamba Makubwa na maeneo ya Wafugaji.

Awali Msimamizi wa Miradi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Catherine Joachim, akiwa amemwakilisha Katibu Mkuu, amesema kuchaguliwa kwa mkoa wa Tabora kuwa mwenyeji wa Maadhimisho ya Wiki ya Malaria, ni pamoja na kuongeza nguvu ya afua za kupambana na Malaria kutokana na Mkoa huo kuwa na Maambukizi ya juu ya Ugonjwa huo ya asilimia 23.4 kwa sasa kutoka asilimia 11.7 kwa mwaka 2011.

read more

AIS SAMIA AKIWA KWENYE SHEREHE ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa wa Tanzania na ule wa Afrika Mashariki ukiimbwa katika Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kushuka kwenye gari Maalum la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakati wa Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sherehe hizo zimefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.
read more

MKUTANO MKUU WA ALAT 2024; WAZIRI MCHENGERWA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF

 ZANZIBAR

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma umeshiriki kwenye Mkutano Mkuu wa 38 wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Zanzibar na kupata fursa ya kuelimisha kupitia maonesho na uwasilishaji wa mada kwa wajumbe wa mkutano Mkuu.

Mkutano huo muhimu hujumuisha Wenyeviti wa Mikoa na Halmashauri zote nchini, Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa zote nchini, Mameya, na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya ALAT.

Meneja wa Ofisi ya Zanzibar wa PSSSF, Bi. Amina Kassim aliwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuhusu maboresho ya kidijitali yaliyofanywa na PSSSF ili kuboresha huduma kwa wateja ikiwemo kuhusu mfumo mpya wa kupokea madai ya mafao mtandaoni na usajili wa wanachama mtandaoni.

Aidha aliwaomba waendelee kutoa ushirkiano ili kutatua changamoto za kiutendaji kwa wakati.

Mkutano huo ulifunguliwa rasmi na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa na kufungwa na Waziri wa Nchi Ofisi yanRais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud Ali Mohamed.

Mkutano Mkuu umehudhuriwa na wajumbe na taasisi wadhamini takribani 450.




read more