Na Mwandishi wetu Michuzi TV
Latest Articles
JKT YAREJEA WITO KWA VIJANA WALIOCHELEWA KURIPOTI MAKAMBINI, WARUHUSIWA KURIPOTI HADI JUNI 15, 2026
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:55 AMKIKWETE AKUTANA NA MSHARI WA TRUMP PEMBEZONI MWA MKUTANO WA OSLO FORUM
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 7:03 AMWAGONJWA NANE WENYE MISHIPA YA DAMU ILIYOZIBA KUFANYIWA UPASUAJI WA MOYO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:30 AMWataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao kumfanyia upasuaji wa kupandikiza mshipa wa damu wa moyo bila kusimamisha moyo mgonjwa mwenye matatizo ya mishipa ya damu kuziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
***************************************************************************************************
Wagonjwa nane wenye matatizo ya mishipa ya damu ya moyo iliyoziba (coronary artery disease) kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo (off Pump CABG).
Upasuaji huo unafanyika katika kambi maalumu ya siku nane inayofanywa na watalaamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu ya moyo iliyoziba watumie kambi hiyo kupata matibabu na kupunguza gharama ambazo wangetumia kusafiri nje ya nchi kwaajili ya matibabu.
“Upasuaji huu unafaida kubwa kwa wagonjwa ambao wamekuwa wakitumia dawa kwa muda mrefu kwa kupata matibabu kwani unafanyika bila kusimamisha moyo na unamsaidia mgonjwa kupona kwa muda mfupi na kuendelea na shughuli zake za kawaida”, alisema Dkt. Angela.
Dkt. Angela alibainisha kuwa kupitia kambi hiyo wataalumu wa JKCI watapata fursa ya kujengewa uwezo na kubadilishana uzoefu na wenzao kutoka India jambo mbalo litasaidia kuimarisha zaidi huduma za upasuaji na mishipa ya moyo nchini.
“Tayari tumemfanyia upasuaji mgonjwa mmoja ambaye mishipa mitatu ya moyo ilikuwa imeziba kwa mafanikio makubwa na tunatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa nane katika kambi hii”, alisema Dkt. Angela.
Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo na Mishipa ya Damu kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao alisema upasuaji huo unafanyika kwa ufanisi mkubwa kutokana na uwekezaji mkubwa wa vifaa tiba uliofanywa na Serikali ya Tanzania kupitia JKCI.
“Tumekuwa tukija Tanzania mara kwa mara kutokana na ushirikiano mzuri wa kitabibu uliopo kati ya India na Tanzania na kuwasaidia wagonjwa ambao wanatumia gharama kubwa kufuata matibabu India hivyo uwepo wetu hapa umekuwa ukiwapunguzia adha wagonjwa wenye matatizo ya mishipa yad amu ya moyo iliyoziba”, alisema Bhalerao.
Kambi hiyo maamulu ya upasuaji wa mishipa ya damu ya moyo iliyoziba inatarajiwa kumalizika mapema tarehe 15 mwezi Juni mwaka huu.
RAIS WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MADAKTARI WA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) DR. NIKOLAI SHARKOV ATEMBELEA MABANDA MAONESHO YA PILI YA BIDHAA ZA KINYWA NA MENO ZA KIMATAIFA (DENTAL EXPO)
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:41 PMTDA NA SHIRIKISHO LA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) WAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA MUHAS
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:52 AMChama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) na Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI) wameahidi kuendeleza uhsirikiano na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ahadi ya ushirikiano huo ilifikiwa mwishoni mwa wiki, wakati Mkuu wa Shule Kuu ya Afya ya Kinywa na Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Ferdinand Machibya, alipokuwa akizungumza na Rais wa Shirikisho la kinywa na Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov, ambaye alitembelea MUHAS akiwa na ujumbe wake kutoka FDI kwa lengo la kuongeza ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ziara hiyo iliwakutanisha wataalamu wa tiba ya meno, wahadhiri, pamoja na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Dk. Machibya, alimkaribisha, Prof. Nikolai Sharkov, chuoni hapo. Alieleza kuwa ziara hiyo inaonesha kuongezeka kwa ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Dk. Machibya alisema MUHAS inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi kupitia ufundishaji, utafiti, pamoja na huduma za ushauri wa kitaalamu. Aliongeza kuwa Shule ya Tiba ya Meno imekuwa ikivutia wanafunzi wa shahada za uzamili na wataalamu kutoka nchi mbalimbali wanaojiunga na chuo hicho kwa ajili ya mafunzo maalum na kozi fupi za afya.
Katika ziara hiyo, Prof. Sharkov aliipongeza Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS kwa mchango wake katika sayansi ya afya ya kinywa na meno, na kuisifu shule hiyo kwa kuwa Kituo Bora cha Umahiri katika Sayansi ya Afya ya Kinywa na Meno Afrika Mashariki.
Kwa upande wake, Prof. Sharkov pia aliipongeza MUHAS pamoja na Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.
Aidha, aliwahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.
Tukio hilo lilifanyika katika Shule ya Tiba ya Meno MUHAS na kuhudhuriwa na viongozi wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania, madaktari wa meno wa kanda mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS, pamoja na wanafunzi.
RAIS WA TDA DK. BEREGE ASEMA UJIO WA RAIS WA FDI PROF. SHARKOV UMEWAONGEZEA CHACHU WANATAALUMA, AFYA YA KINYWA NA MENO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:44 PMRais wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) Dk. Gemma Berege, amesema ujio wa Rais wa Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov umewaongezea chachu wao kama wanataaluma na kuwafanya kudumu na kudumu zaidi katika misingi ya majukumu yao ya kila siku.
Amesema, ujio huo unawaongezea chachu kwa kuwa umegusa jukumu lao kubwa ambalo ni kulinda taaluma yao ikiwemo kwa kujiongeza katika elimu. "Tumefurahi kwamba hata katika mazungumzo yake Prof Sharkov, amesisitiza ushirkiano na kujituma, hivyo ametuongezea ari", alisema Dk. Berege.
Dk. Berege alisema pia ujio wa Prof Sharkov umeleta ari kwa vyama vya wanafunzi ambao kwa kuwa wamekuwa wakikutana naye kupitia wawakilishi wao na kupata ya kujifunza mengi kupitia kwake (Prof, Sharkov).
Kwa upande wake Prof, Sharkov ambaye alikuwa nchini na kupata fursa ya kukutana na viongozi wa TDA na Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS, aliwapongeza kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.
Pia amewahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.
Prof. Sharkov, alikutana na viongozi hao Mei 29, 2026, ambapo akiambatana na ujumbe wa TDA alitembelea MUHAS katika juhudi za kuimarisha ushirikiano katika elimu ya tiba ya meno na maendeleo ya taaluma hiyo.
Nyakati za mazungumzo na Prof. Sharkov, walihudhuria viongozi hao wa TDA, madaktari wa meno wa kada mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.
Dk. Berege akimpatia zawadi ya picha Prof Sharkov alipofika ofisi ya TDA.
Dk. Berege akimpatia zawadi ya fulana Prof Sharkov alipofika ofisi ya TDA.
Dk. Berege akimpatia maelezo kwa Prof Sharkov. kuhusu beji ya TDA kabla ya kumkabidhi.
MBUNGE KIGOMA MJINI CLAYTON CHIPANDO ATAKA KITENGO CHA ELIMULISHE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:52 AMMbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.














.jpeg)







