Latest Articles
RAIS WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MADAKTARI WA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) DR. NIKOLAI SHARKOV ATEMBELEA MABANDA MAONESHO YA PILI YA BIDHAA ZA KINYWA NA MENO ZA KIMATAIFA (DENTAL EXPO)
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:41 PMTDA NA SHIRIKISHO LA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) WAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA MUHAS
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:52 AMChama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) na Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI) wameahidi kuendeleza uhsirikiano na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ahadi ya ushirikiano huo ilifikiwa mwishoni mwa wiki, wakati Mkuu wa Shule Kuu ya Afya ya Kinywa na Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Ferdinand Machibya, alipokuwa akizungumza na Rais wa Shirikisho la kinywa na Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov, ambaye alitembelea MUHAS akiwa na ujumbe wake kutoka FDI kwa lengo la kuongeza ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ziara hiyo iliwakutanisha wataalamu wa tiba ya meno, wahadhiri, pamoja na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Dk. Machibya, alimkaribisha, Prof. Nikolai Sharkov, chuoni hapo. Alieleza kuwa ziara hiyo inaonesha kuongezeka kwa ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Dk. Machibya alisema MUHAS inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi kupitia ufundishaji, utafiti, pamoja na huduma za ushauri wa kitaalamu. Aliongeza kuwa Shule ya Tiba ya Meno imekuwa ikivutia wanafunzi wa shahada za uzamili na wataalamu kutoka nchi mbalimbali wanaojiunga na chuo hicho kwa ajili ya mafunzo maalum na kozi fupi za afya.
Katika ziara hiyo, Prof. Sharkov aliipongeza Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS kwa mchango wake katika sayansi ya afya ya kinywa na meno, na kuisifu shule hiyo kwa kuwa Kituo Bora cha Umahiri katika Sayansi ya Afya ya Kinywa na Meno Afrika Mashariki.
Kwa upande wake, Prof. Sharkov pia aliipongeza MUHAS pamoja na Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.
Aidha, aliwahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.
Tukio hilo lilifanyika katika Shule ya Tiba ya Meno MUHAS na kuhudhuriwa na viongozi wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania, madaktari wa meno wa kanda mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS, pamoja na wanafunzi.
RAIS WA TDA DK. BEREGE ASEMA UJIO WA RAIS WA FDI PROF. SHARKOV UMEWAONGEZEA CHACHU WANATAALUMA, AFYA YA KINYWA NA MENO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 3:44 PMRais wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) Dk. Gemma Berege, amesema ujio wa Rais wa Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov umewaongezea chachu wao kama wanataaluma na kuwafanya kudumu na kudumu zaidi katika misingi ya majukumu yao ya kila siku.
Amesema, ujio huo unawaongezea chachu kwa kuwa umegusa jukumu lao kubwa ambalo ni kulinda taaluma yao ikiwemo kwa kujiongeza katika elimu. "Tumefurahi kwamba hata katika mazungumzo yake Prof Sharkov, amesisitiza ushirkiano na kujituma, hivyo ametuongezea ari", alisema Dk. Berege.
Dk. Berege alisema pia ujio wa Prof Sharkov umeleta ari kwa vyama vya wanafunzi ambao kwa kuwa wamekuwa wakikutana naye kupitia wawakilishi wao na kupata ya kujifunza mengi kupitia kwake (Prof, Sharkov).
Kwa upande wake Prof, Sharkov ambaye alikuwa nchini na kupata fursa ya kukutana na viongozi wa TDA na Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS, aliwapongeza kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.
Pia amewahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.
Prof. Sharkov, alikutana na viongozi hao Mei 29, 2026, ambapo akiambatana na ujumbe wa TDA alitembelea MUHAS katika juhudi za kuimarisha ushirikiano katika elimu ya tiba ya meno na maendeleo ya taaluma hiyo.
Nyakati za mazungumzo na Prof. Sharkov, walihudhuria viongozi hao wa TDA, madaktari wa meno wa kada mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.
Dk. Berege akimpatia zawadi ya picha Prof Sharkov alipofika ofisi ya TDA.
Dk. Berege akimpatia zawadi ya fulana Prof Sharkov alipofika ofisi ya TDA.
Dk. Berege akimpatia maelezo kwa Prof Sharkov. kuhusu beji ya TDA kabla ya kumkabidhi.
MBUNGE KIGOMA MJINI CLAYTON CHIPANDO ATAKA KITENGO CHA ELIMULISHE
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:52 AMMbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.
JKCI YAWAGUSA WANANCHI NJOMBE KUPITIA KAMPENI YA "JUWA NAMBA ZAKO"
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 7:43 AM

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Modesta Nyagawa akimpima kiwango cha sukari kwenye damu mkazi wa Njombe aliyefika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinayotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
Mtaalamu wa vipimo vya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Sven Kamugisha akimpima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi mkazi wa Njombe aliyefika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe kwaajili ya kupata huduma ya uchunguzi na matibabu ya magonjwa mbalimbali zinazotolewa kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kilichoandaliwa na Idara ya Habari- Maelezo.
**********************************************************************************************************************************************************************************************
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) imewahimiza wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara kupitia kampeni ya “Jua Namba Zako” ili kubaini mapema vihatarishi vya magonjwa ya moyo na kupata matibabu kwa wakati.
Rai hiyo imetolewa leo na Daktari wa Taasisi hiyo Samweli Mbilinyi wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma za upimaji wa moyo zinazotolewa na JKCI kwenye Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini kinachofanyika katika Hoteli ya Agreement iliyopo mjini Njombe.
Dkt. Mbilinyi alisema wananchi wengi bado hawana uelewa wa kutosha kuhusu magonjwa ya moyo jambo linalosababisha baadhi yao kuishi na matatizo hayo bila kujitambua hadi wanapofika hospitalini wakiwa na matatizo mengine.
Alitoa mfano wa mgonjwa aliyefika katika upimaji huo ambao huduma za upimaji wa magonjwa mbalimbali zinatolewa kwajili ya matatizo ya miguu lakini baada ya kupimwa alibainika kuwa na shinikizo kubwa la damu lililozidi kiwango cha kawaida hali iliyowalazimu wataalamu wa JKCI kumfanyia vipimo vya moyo na kuanza matibabu mara moja.
“Tumegundua wananchi wengi hawajawahi kupima afya ya moyo wala kufahamu viwango vyao vya afya. Kupitia kampeni ya Jua Namba Zako tunawahamasisha wananchi wajitokeze kupima ili kujua hali zao mapema na kupata tiba stahiki”, alisema Dkt. Mbilinyi.
Dkt. Mbilinyi alisema katika upimaji unaoendelea wamebaini watu wengi wenye shinikizo la juu la damu na matatizo ya moyo ambao hawakuwahi kufanyiwa vipimo vya moyo wala kujua hali zao za afya.
Aliishukuru Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuwezesha upatikanaji wa dawa bure kwa wananchi wanaobainika kuwa na matatizo mbalimbali ya afya ikiwemo magonjwa ya moyo katika upimaji huo.
“Ninawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi kupima afya zao. Watakaobainika kuwa na changamoto watapatiwa ushauri wa kitaalamu, tiba, dawa bila malipo na rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI”, alisisitiza.
Kwa upande wao wananchi waliopata huduma hizo walieleza kufurahishwa na ujio wa wataalamu wa JKCI mkoani Njombe huku wakisema umewasaidia kupata huduma karibu na maeneo yao na kupunguza gharama za kusafiri kwenda Dar es Salaam.
Mmoja wa wananchi hao Farida Fredrick kutoka kijiji cha Ihalula, alisema alifika kupata huduma baada ya kusikia madaktari wa JKCI wanatoa huduma Njombe.
“Mimi ni mgonjwa wa moyo na huwa nahudhuria kliniki ya JKCI Dar es Salaam. Niliposikia madaktari wako hapa Njombe nikaona nitumie nafasi hii kupata huduma karibu na nyumbani, huduma ni nzuri sana na wananchi wengi wajitokeze kupima”, alisema Farida.
Joseph Mwakalonge mkazi wa Njombe mjini alisema alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya kichwa pamoja na uchovu wa mara kwa mara bila kufahamu chanzo chake lakini baada ya kufanyiwa uchunguzi alibainika kuwa na shinikizo la juu la damu na kupewa matibabu.
“Naishukuru sana JKCI kwa kuleta huduma hizi karibu yetu. Sikuwahi kujua kama nina tatizo la presha kubwa kiasi hiki lakini leo nimepata elimu, vipimo na dawa kitu ambacho kitanisaidia kuutunza moyo wangu mapema ili usipate madhara zaidi”,alisema Mwakalobe.
Naye Rehema Mlowe mkazi wa Makambako alisema alikuwa hajawahi kupima afya ya moyo tangu alipogundulika kuwa na changamoto ya presha miaka miwili iliyopita lakini ujio wa madaktari wa JKCI umempa nafasi ya kufanyiwa uchunguzi wa kina na kupata ushauri wa namna ya kuishi kwa kufuata mtindo bora wa maisha.
“Nimepata huduma nzuri na wataalamu wanatoa elimu kwa upendo mkubwa. Ninawaomba wananchi wenzangu watumie fursa hii kuja kupima afya zao mapema kabla hali haijawa mbaya”, alisema Rehema.
Katika upimaji huo JKCI inatoa huduma za uchunguzi wa awali wa magonjwa ya moyo, uchunguzi wa shinikizo la damu, kipimo cha kuangalia uwingi wa sukari kwenye damu, kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi, elimu ya lishe bora na mtindo sahihi wa maisha, elimu ya kujikinga na magonjwa ya moyo na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa madaktari bingwa wa moyo.
MAAFISA UTAWALA NA RASILIMALIWATU 316 NCHINI WAPIMWA MAGONJWA YA MOYO
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:27 AMUchunguzi huo umefanyika kwa siku tatu wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.
Akielezea kuhusu mwitikio wa maafisa hao kufanya uchunguzi wa afya Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete alisema mwitikio umekuwa mkubwa na wenye tija kwa maafisa Utawala na Rasirimali Watu nchini.
“Baada ya kuwafanyia uchunguzi wa afya baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu tumewapa rufaa kufika katika Hospitali zetu kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na kuona viashiria ambavyo vinahitaji uchunguzi zaidi”, alisema Dkt. Salehe
Dkt. Salehe alisema inapotokea fursa kama hiyo ya kupima afya eneo la kazi ni vizuri watumishi wakaitumia vizuri kwani wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi wanakosa muda wa kufika hospitali kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.
“JKCI tumekuwa mstari wa mbele kuwafikishia watumishi wa umma na sekta binafsi huduma za uchunguzi wa afya wakati wa mikutano mbalimbali lakini pia hata kuwafuata katika maeneo yao ya kazi, jitihada zote hizi tunazofanya tunataka kuhakikisha kuwa tunailinda jamii na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo”, alisema Dkt. Salehe
Nao maafisa Utawala na Rasirimali Watu walioshiriki katika mkutano huo wameiomba JKCI kuendela kutoa elimu ya magonjwa ya moyo ili kuliokoa taifa la Tanzania na changamoto ya magonjwa hayo.
Maafisa hao walisema Serikali ya Tanzania ina mchango mkubwa katika kuhakikisha watu wake wanakuwa salama ndio maana imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya na kuhakikisha elimu kuhusu kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali inawafikia wananchi.
RAIS SAMIA AAGIZA MPANGO MAALUM WA KUWAINUA WAFUNGWA WENYE UJUZI WANAPOREJEA URAIANI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:48 PMread more

















































