



Na Mwandishi wetu Michuzi TV
Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao kumfanyia upasuaji wa kupandikiza mshipa wa damu wa moyo bila kusimamisha moyo mgonjwa mwenye matatizo ya mishipa ya damu kuziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) na Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI) wameahidi kuendeleza uhsirikiano na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ahadi ya ushirikiano huo ilifikiwa mwishoni mwa wiki, wakati Mkuu wa Shule Kuu ya Afya ya Kinywa na Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Ferdinand Machibya, alipokuwa akizungumza na Rais wa Shirikisho la kinywa na Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov, ambaye alitembelea MUHAS akiwa na ujumbe wake kutoka FDI kwa lengo la kuongeza ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Ziara hiyo iliwakutanisha wataalamu wa tiba ya meno, wahadhiri, pamoja na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.
Akizungumza wakati wa mkutano huo, Dk. Machibya, alimkaribisha, Prof. Nikolai Sharkov, chuoni hapo. Alieleza kuwa ziara hiyo inaonesha kuongezeka kwa ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.
Dk. Machibya alisema MUHAS inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi kupitia ufundishaji, utafiti, pamoja na huduma za ushauri wa kitaalamu. Aliongeza kuwa Shule ya Tiba ya Meno imekuwa ikivutia wanafunzi wa shahada za uzamili na wataalamu kutoka nchi mbalimbali wanaojiunga na chuo hicho kwa ajili ya mafunzo maalum na kozi fupi za afya.
Katika ziara hiyo, Prof. Sharkov aliipongeza Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS kwa mchango wake katika sayansi ya afya ya kinywa na meno, na kuisifu shule hiyo kwa kuwa Kituo Bora cha Umahiri katika Sayansi ya Afya ya Kinywa na Meno Afrika Mashariki.
Kwa upande wake, Prof. Sharkov pia aliipongeza MUHAS pamoja na Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.
Aidha, aliwahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.
Tukio hilo lilifanyika katika Shule ya Tiba ya Meno MUHAS na kuhudhuriwa na viongozi wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania, madaktari wa meno wa kanda mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS, pamoja na wanafunzi.
Mwana mama Mikel Ruffinelli(39 Kutoka nchini Marekani akipunga upepo ufukwen
Uwezi kukuta Mbwa, Panya na Msituni manyani wote wanakuwa kitoweo. Awa ni popo wamesha aandaliwa tayari kwa kitoweo Ametole...
SENSODYNE Ni Dawa ambayo iliyothibitishwa kitaalamu kwaajili ya meno yenye ganzi (UKAKASI).au maumivu makali ya muda mfupi yatokanay...
Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa WAKILI wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa amesema kwa niaba ya wananchi...
Dkt. Telesphory Kyaruzi akionyesha moja ya vifaa aliyopokea kutoka kwa Wamarekani waliofika katika Hospitali ya JK iliyopo Kigamboni Da...
Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.Magdalena Rwebangira amewakumbusha watendaji wa Uchaguzi ngazi ya Mkoa na Jimbo kushirikian...
Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi y...
Na Khamis Mussa, Muhimbili Rais wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) Dk. Gemma Berege, amesema ujio wa Rais wa Shirikisho la Madakt...
- Awataka watanzania kutoka kwa wingi kupiga kura kumchagua Dkt Samia Suluhu,Wabunge na Madiwani wanaotokana na CCM. Na Oscar Assenga,MUHE...
Leo jioni nimewasili Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ambapo nitaungana na viongozi wengine katika uzinduzi wa Global Africa Investmen...

