read more
Latest Articles
TAHADHARI YATOLEWA; UWEPO WA MAFUA MAKALI YA INFLUENZA, UVIKO 19, HOMA YA DENGUE NA KIPINDUPINDU
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:26 AMMARUFUKU WATUMISHI WA UMMA KUTUMIA MIFUMO ISIYO RASMI KUWEKA NYARAKA ZA SERIKALI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:44 AM![]() |
|
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete akifunga Kikao kazi cha 6 cha Serikali
mtandao kilichafanyika kwa siku Tatu Mkoani Arusha.
|
Serikali imepiga marufuku watumishi wa Uma Kutumia mitandao isiyo rasmi ambayo ni tofauti na ile iliyounganishwa na mfumo wa Serikali mtandao katika kutuma nyaraka na taarifa mbalimbali za serikali kwani si salama kwa usalama wa nchi na wananchi
Marufuku hiyo imetolewa l9 April 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete wakati akifunga kikao kazi cha 6 cha serikali mtandao kilichofanyika kwa siku Tatu mkoani Arusha nakusema kwamba watumishi wa Umma kutumia mifumo isiyo rasmi ni hatari kwani inasababisha nyaraka za siri za serikali kuonekana mtandaoni.
Bado tunao wafanyakazi wa Serikali wanatumia Mtandao binafsi kurusha taarifa za Serikali jambo ambalo siyo sawa kwa taarifa hizo za Serikali kuwekwa wazi jambo hilo liwe narufuku kuanzia Leo taarifa za Serikali kutumwa kwa Mtandao binafsi. Alisema
Kikao Kazi hicho cha siku tatu, kimewakutanisha takribani washiriki 1,000 kutoka sekta za umma na binafsi, na kimejadili kwa kina masuala muhimu yanayohusu ujenzi, uendelezaji na usimamizi wa jitihada za Serikali Mtandao. Ambapo Kupitia mijadala hiyo wamepata fursa ya: Kutathmini utekelezaji wa maazimio ya Kikao Kazi kilichopita,, Kubainisha mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa miradi ya TEHAMA Serikalini,
Pia waliweza Kujadili changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana nazo,Na kuweka maazimio mapya yatakayotuongoza katika hatua zinazofuata za kuendelea kuboresha utendaji kazi na utoaji wa huduma za umma kwa njia ya kidijitali.
Kikwete amesema amefarijika kuona kuwa, mijadala yote imejikita katika uzingatiaji wa Sheria, Kanuni,Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, jambo ambalo ni msingi muhimu wa kuhakikisha miradi ya TEHAMA Serikalini inakuwa salama, endelevu na yenye kujali Katika kikao kazi hiki,
Sambamba na hayo Serikali kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), itatoa tuzo kwa taasisi zilizofanya vizuri katika kuzingatia Sheria, Kanuni, Viwango na Miongozo ya Serikali Mtandao, kwenye utekelezajiwa miradi ya TEHAMA.ambapo amezipongeza taasisi zote zilizotunukiwa tuzo hizo na kusema Tuzo hizo si za heshima tu, bali ni chachu ya kuhamasisha ubora, uwajibikaji na uzingatiaji wa misingi ya Serikali Mtandao katika taasisi zote za umma.
read moreRAIS SAMIA AWASILI DUBAI. UMOJA WA FALME ZA KIARABU (UAE)
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:32 PMUshiriki wa Tanzania katika majukwaa haya ni kielelezo cha uthabiti wake kisiasa, na dhamira yake ya kuendelea kuvutia uwekezaji toka ndani na nje ya nchi, utakaozalisha ajira zaidi na kuchagiza maendeleo yetu. Aidha, ni utekelezaji wa Dira 2050 pamoja Sera mpya ya Mambo ya Nje katika Diplomasia ya Uchumi. NA IKULU. @Khamisi Mussa.
read more
TAIFA LIMEPATA PENGO KUONDOKEWA NA MBUNGE WA JIMBO LA PERAMIHO,RUVUMA -DKT.NCHIMBI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 1:07 PM
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema Taifa limepata pengo kuondokewa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma, marehemu Jenista Mhagama ambaye alikuwa kiongozi aliyeheshimika na kutumikia nchi katika majukumu mbalimbali ya kitaifa.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akitoa salamu za rambirambi alipowasili kuhani msiba nyumbani kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, marehemu Jenista Mhagama eneo la Itega Jijini Dodoma.
Amesema marehemu Mhagama licha ya kuwa ni alikuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, lakini pia alitoa mchango wake katika Chama Cha Mapinduzi na kusimamia maendeleo ya Mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.
Makamu wa Rais ametoa pole kwa familia na waombolezaji na kuwaombea watoto wa marehemu na ndugu wa karibu, Mungu awape ujasiri wa kukubali jambo hilo na kutambua ni njia ya watu wote.
DCI MSTAAFU BALOZI ADADI RAJAB OCTOBA 29 TUJITOKEZENI KWA WINGI KUPIGA KURA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:33 AM -Awataka watanzania kutoka kwa wingi kupiga kura kumchagua Dkt Samia Suluhu,Wabunge na Madiwani wanaotokana na CCM.
WAKILI MAHAKAMA KUU YA TANZANIA KUFUNGUA KESI KWA NIABA YA WANANCHI KUHUSU TOZO DARAJA LA KIGAMBONI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:40 AM
Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa
WAKILI wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mohamed Majaliwa amesema kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni anakwenda kufungua kesi ya Kikatiba kuomba Mahakama itoe tamko kwamba kulipa tozo la Daraja la Kigamboni ni kinyume cha Katiba.
Wakili Majaliwa amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusiana na mchakato wa kufungua shauri la Kikatiba Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam.
Amesema wamefikia hatua hiyo, baada ya kutumia mbinu mbalimbali ya kumaliza tatizo hilo lakini imeshindikana, wameamua kwenda kisheria zaidi ili kuondoa changamoto hiyo.
"Tunakwenda kufungua kesi kwa kuomba Mahakama itoe tamko tu kwamba kitendo cha wananchi wa Kigamboni au mwananchi yeyote kutoka nje ya Kigamboni kutaka kuvuka kuingia kulazimika kulipa tozo ya daraja ni kinyume na Katiba,"
"Na hasa kuzingatia juzi wastani wa mwezi mmoja umepita nilikuwa nimefuatilia uzinduzi wa Dira ya Maendeleo ya miaka 25 mbele sijaona nafuu kwa watu wa Kigamboni kuondosha tozo zile, "Amesema Wakili Majaliwa.
Amesema utaratibu unaoendelea wa tozo hizo, unakizana na sheria zenyewe, sheria ambazo zinatumika kutoza tozo zipo za aina mbili, The Road Tolls (Fees) Regulations, 1985 (Kanuni ya tozo za barabara) na The Road and Fuel Tolls Act (Sheria ya tozo za barabara na mafuta).
"Ukizisoma sheria hizi mbili kwa pamoja kwa ujumla wake, mimi mwananchi wa Kigamboni nikitumia daraja kwa kuvuka kwa daladala au gari yangu binafsi naangukia katika kulipa kodi mara mbili,"amesema
read moreMGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ametoa rai kwa vijana nchini wasikubali kudanganyika ili kuchafua amani ya nchi.
Akizungumza leo katika viwanja vya TANESCO -Buza villivyopo Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam akihitimisha mikutano yake ya kampeni za uchaguzi mkuu, Dk. Samia ametumia nafasi kuwaeleza vijana umuhimu wa kutunza amani iliyopo nchini.
Amesisitiza kwamba Tanzania ni eneo sahihi kwa vijana kuishi tofauti na maeneo mengine Afrika, hivyo amewataka wasikubali kufanganywa kwa namna yeyote ili kuvuruga amani ya nchi yao.
"Hapa mpo kwenye nchi yenye jina, yenye sifa zake, yenye kuendeleza watu wake. Msidanganywe wale ambao wapo nje wasiwadanganye.
“Hapa mpo pazuri kweli kweli.Niwahakikishie vijana wa Tanzania, hawa wazee wenzangu wanaelewa. Vijana wa Kitanzania msidanganywe, ukichukua Afrika Mashariki, Kusini na Kati, Tanzania ni pepo.Nchi yetu iko salama”
Akisisitiza zaidi Mgombea Urais Dk.Samia amesema "Mkipata fursa kuingia kwa majirani zetu, mtaona vijana wenzenu wanavyokula ngumu. Mtasema mnataka kurudi kwenu."
Amewakumbusha kuwa vijana ndio wanategemewa kukabidhiwa nchi kuiendesha kama inavyoendeshwa bila kudanganywa.”Katika kuongoza nchi, taifa limeweka mifumo mizuri ya kidemokrasia kwa kuchaguana kila baada ya miaka mitano.”
"Tulizeni munkali, nchi hii ni mali yenu, hakuna mwenye cheti anayesema nchii hii ni mali yangu. Sisi tunawakilisha wananchi, wananchi ndiyo nyinyi.Hakuna mwenye miliki ya wananchi, wananchi ndiyo nyinyi.
“Tumepeana tu majukumu, niwaombe sana vijana msiharibu nchi yenu. Fuateni serikali yenu inavyowaambia, fuateni katiba yenu inavyowaelekeza," amesema Dk.Samia.
Pamoja na hayo ametoa mwito kwa vijana kujitokeza kwa wingi kupigakura kwani ndiyo haki ya msingi kidemokrasi.
“Hakuna mfumo uliowekwa kuhusu siasa safi kwani siasa safi ni kuhakikisha nchi na wananchi wapo salama ikiwemo kujumuishwa katika maamuzi.
“Serikali imekuwa ikiunda kamati kukusanya maoni kuhusu masuala mbalimbali yenye kuhusu maendeleo ya nchi.Hata panapotokea mazonge kwenye nchi tunaunda tume kuja kuwauliza, mnatoa maoni yenu. Hiyo ndiyo siasa safi.”
Ameongeza kuwa “Mnapokerana mnaitana kuzungumza, tuyazungumze, tuelewane, twende pamoja hiyo ndiyo siasa safi.”Amesema Dk.Samia na kuongeza hayo ndiyo mambo Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere aliyokuwa akiyasimamia ambapo serikali zote za CCM zimekuwa zikitekeleza.



































