Latest Articles

MAAFISA UTAWALA NA RASILIMALIWATU 316 NCHINI WAPIMWA MAGONJWA YA MOYO

 

   Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nadia Zuberi akimpima shinikizo la damu (BP) Afisa Rasirimali Watu aliyefika katika kliniki ya JKCI wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.

  Daktari wa Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) ambayo inasimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Adda Justine akimpa ushauri Afisa Rasirimali Watu aliyefika katika kliniki ya JKCI wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.

  Baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasirimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). 

.............................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 wamepima moyo.Jumla ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu 316 nchini wamefanyiwa uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kuwawezesha kufahamu namba zao na kuwapa elimu ya namna ya kujikinga na magonjwa ya moyo.
Uchunguzi huo umefanyika kwa siku tatu wakati wa Mkutano Mkuu wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania uliomalizika jana katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC) jijini Arusha.
Akielezea kuhusu mwitikio wa maafisa hao kufanya uchunguzi wa afya Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) inayosimamiwa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Salehe Mwinchete alisema mwitikio umekuwa mkubwa na wenye tija kwa maafisa Utawala na Rasirimali Watu nchini.
“Baada ya kuwafanyia uchunguzi wa afya baadhi ya maafisa Utawala na Rasirimali Watu tumewapa rufaa kufika katika Hospitali zetu kwaajili ya uchunguzi zaidi kutokana na kuona viashiria ambavyo vinahitaji uchunguzi zaidi”, alisema Dkt. Salehe
Dkt. Salehe alisema inapotokea fursa kama hiyo ya kupima afya eneo la kazi ni vizuri watumishi wakaitumia vizuri kwani wanapokuwa katika maeneo yao ya kazi wanakosa muda wa kufika hospitali kwaajili ya kufanya uchunguzi wa afya.
“JKCI tumekuwa mstari wa mbele kuwafikishia watumishi wa umma na sekta binafsi huduma za uchunguzi wa afya wakati wa mikutano mbalimbali lakini pia hata kuwafuata katika maeneo yao ya kazi, jitihada zote hizi tunazofanya tunataka kuhakikisha kuwa tunailinda jamii na magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo”, alisema Dkt. Salehe
Nao maafisa Utawala na Rasirimali Watu walioshiriki katika mkutano huo wameiomba JKCI kuendela kutoa elimu ya magonjwa ya moyo ili kuliokoa taifa la Tanzania na changamoto ya magonjwa hayo.
Maafisa hao walisema Serikali ya Tanzania ina mchango mkubwa katika kuhakikisha watu wake wanakuwa salama ndio maana imefanya uwekezaji mkubwa katika sekta ya afya na kuhakikisha elimu kuhusu kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali inawafikia wananchi.
read more

RAIS SAMIA AAGIZA MPANGO MAALUM WA KUWAINUA WAFUNGWA WENYE UJUZI WANAPOREJEA URAIANI


Na Mwandishi wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Magereza kufanya tafiti za kina zitakazowezesha kuanzishwa kwa mfuko maalumu wa kuwasaidia wafungwa wenye ujuzi wanaporejea uraiani, ili waweze kujitegemea kiuchumi na kuepuka kurejea katika makosa ya uhalifu.

Rais Samia amesema hatua hiyo ni sehemu ya kuimarisha mfumo wa urekebishaji nchini kwa kuhakikisha wafungwa wanaopata mafunzo ya ufundi na stadi mbalimbali wakiwa magerezani wanapata mazingira rafiki ya kuanza maisha mapya baada ya kutumikia vifungo vyao.

Ametoa maelekezo hayo leo Mei 9, 2026, wakati akihutubia hafla ya kuhitimisha Mafunzo ya Uongozi Ngazi ya Juu Kozi Na. 28 pamoja na Uongozi Daraja la Pili Kozi Na. 48 iliyofanyika katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA), Ukonga jijini Dar es Salaam.

Katika hotuba yake, Rais Samia alisema wafungwa wengi wamekuwa wakipata ujuzi muhimu wakiwa magerezani kupitia mafunzo mbalimbali ya ufundi stadi, ushonaji, kilimo, useremala na shughuli nyingine za uzalishaji, lakini changamoto kubwa imekuwa ni ukosefu wa mtaji au mifumo ya kuwawezesha kuanza maisha mapya wanapotoka gerezani.

Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kutasaidia kuwapa nguvu ya kuanza upya kwa kutumia maarifa na taaluma walizozipata, jambo litakalosaidia kupunguza matukio ya kurudia makosa pamoja na kuongeza mchango wao katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

“Tunapaswa kuwapa nafasi ya pili ya maisha. Kama wamejifunza kazi na stadi mbalimbali wakiwa magerezani, basi wanapotoka wanahitaji kuungwa mkono ili waweze kujitegemea na kuwa sehemu ya maendeleo ya nchi,” alisisitiza Rais Samia.

Aidha, amemuelekeza Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Tanzania, Jeremiah Katungu kushirikiana na wadau mbalimbali kufanya tafiti za sera na mifumo bora itakayowezesha utekelezaji wa mpango huo kwa ufanisi.

Rais Samia pia alipongeza Jeshi la Magereza kwa kuendelea kuboresha mfumo wa urekebishaji wa wafungwa kwa kuwapatia elimu, maadili na stadi za maisha zinazowaandaa kuwa raia wema baada ya kumaliza vifungo vyao.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, maafisa wa Jeshi la Magereza pamoja na washiriki wa mafunzo waliohitimu kozi hizo za uongozi.





























read more

JKCI YAPOKEA MKONO MKUU WA UTUMISHI WA UMMA ARUSHA

 

 Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge tuzo ya mdhamini mkuu wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi cheti mfanyakazi bora wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Afisa Utawala Adila Lugamara wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge tuzo ya mtoa mada wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Waziri Ofisi ya Rais, Menenjiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadhamini wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

 wakifuatilia mada zinazoendelea katika Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC). Baadhi ya Maafisa Utawala na Rasilimali Watu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) 

   Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Utawala na RasilimaliWatu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati wa Mkutano wa pili Jumuishi wa Jumuiya za Wataalamu wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma Tanzania unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).
Picha na JKCI

read more

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA MGENI RASMI MKUTANO MKUU WA JUMUIYA YA WAFANYA BIASHARA KARIAKOO 2026


 

 
Mbunge wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu 2026 wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo leo Aprili 25,2026 na kuwapongeza wafanya biashara kwa ulipaji mzuri wa kodi  

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo (JWK) Severini Mushi akimkabidi Tuzo Waziri wa Viwada na Biashara Judith Kapinga leo Aprili 25,2026. Wakati wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya 2026 uliofanyika Jijini Dar es Salaam.




 

Mmoja wa Wafanya Biashara akipitia jarida lenye ratiba nzima ya maadalizi ya hafla hiyo kabla ya kuwasili Waziri wa Viwada na Biashara Judith Kapinga  wakati wa Mkutano Mkuu 2026 wa Jumuiya ya Wafanya Biashara Kariakoo leo Aprili 25,2026.
 

read more