Latest Articles
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa leo, Jumatano, Machi 25, 2026, na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Lukuvi amefariki dunia majira ya saa moja asubuhi katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma.
Taarifa hiyo imebainishwa kuwa Lukuvi alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali hiyo kufuatia ugonjwa wa mshituko wa moyo uliomfika ghafla. Lukuvi amefariki akiwa bado anatumikia nafasi yake kama Mbunge wa Jimbo la Isimani na Waziri katika Baraza la Mawaziri la Rais Samia.
Rais Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, familia ya marehemu, Wananchi wa Jimbo la Ismani, Pamoja na ndugu , jamaa na Watanzania wote waliofikiwa na msiba huo mzito.
read more
TANZANIA NA AUSTRIA ZAENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIDIPLOMASIA NA USALAMA
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:35 AMHayo yameelezwa Machi 23, 2026, jijini Dar es Salaam wakati wa mazungumzo kati ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Ayoub Mahmoud (Mb), na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Austria anayeshughulikia masuala ya kisiasa, Mhe. Balozi Dkt. Hannah Liko.
Mazungumzo hayo yalijikita katika kuainisha vipaumbele vya Tanzania ndani ya Mkakati mpya wa Austria kwa Afrika (2026–2029), mkakati ambao unasisitiza ushirikiano wa usawa, ulinzi wa haki za binadamu, na utawala wa sheria kama nguzo kuu za kuelekea maendeleo endelevu.
Kuelekea utekelezaji wa mkakati huo, Mhe. Mahmoud amewasilisha vipaumbele vya Wizara vinavyolenga kuimarisha usalama na uwezo wa kukabiliana na majanga, huku mkazo mkubwa ukiwekwa katika kupambana na uhamiaji haramu, biashara haramu ya binadamu, matumizi ya dawa za kulevya, pamoja na kuzuia uhalifu wa kimtandao ambao umekuwa tishio la kimataifa.
Mhe. Mahmoud amezungumzia mfumo wa Triple-Win, unaolenga kudhibiti uhamiaji haramu huku ukifungua milango ya kisheria kwa vijana wa Kitanzania wenye ujuzi kupata ajira na mafunzo ya ufundi stadi nchini Austria, hatua inayotarajiwa kuwa suluhisho la kudumu katika kuwapatia vijana fursa za kimataifa na kupunguza utegemezi.
Aidha, Tanzania imekaribisha nia ya Austria kuwekeza katika miradi ya nishati safi na uchumi wa kijani kupitia makampuni yake, ili kusaidia mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kupitia miradi ya pamoja ya kitafiti na kiteknolojia.
Kwa upande wake, Dkt. Liko amethibitisha utayari wa Austria kuunga mkono operesheni za kikanda za kulinda amani za Umoja wa Mataifa na kuongeza kuwa Austria itaendelea kuwa mshirika wa kimkakati katika kukuza viwanda, sayansi, na utamaduni ili kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa mazingira salama kwa raia, uwekezaji, na utalii kwa manufaa ya mataifa yote mawili.
Vilevile amesema kupitia Shirika la Maendeleo la Austria (ADA), nchi hiyo imeahidi kuendelea kuwa mshirika wa kimkakati wa Tanzania katika kukuza utamaduni, sayansi, na maendeleo ya kijamii.
read more
BENKI YA NMB KATIKA UBORA WAKE KUENDELEA KUN'GARA TUZO ZA EUROMONEY 2026
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 9:09 AMUshindi huo unazidi kuakisi uimara wa benki ya NMB yenye matawi 241 nchini na zaidi ya mawakala 73,000 pamoja na wateja zaidi ya 9.9 millioni, katika kutoa huduma mahususi kwa wateja, kuimarisha usalama wa fedha na kuongoza katika utekelezaji wa mikakati ya fedha endelevu.
Mafanikio haya yanaendelea kuimarisha nafasi ya Benki ya NMB
kama kinara wa ubunifu na mshirika wa maendeleo ya uchumi Tanzania.
read more
DKT AKWILAPO AKABIDHI VIFAA TIBA KUIMARISHA HUDUMA ZA AFYA MASASI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 10:15 AMDkt. Akwilapo amekabidhi vifaa hivyo leo, Machi 9, 2026, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha huduma za afya katika Wilaya ya Masasi na maeneo jirani ya wilaya hiyo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Dkt. Akwilapo amesema utoaji wa vifaa tiba ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita kuhakikisha taasisi za huduma za jamii kama vile hospitali na shule zinakuwa na miundombinu na vifaa vinavyowawezesha wataalamu kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Amesema, serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha sekta za afya na elimu zinaimarika ili wananchi waweze kupata huduma bora karibu na maeneo yao.
“Naishukuru serikali chini ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha siyo tu inajenga majengo ya hospitali na shule, bali pia inahakikisha kunapatikana vifaa pamoja na wataalamu watakaowezesha huduma kutolewa kwa ufanisi,” amesema Dkt. Akwilapo.
Ameongeza kuwa, kupatikana kwa vifaa tiba katika Kituo cha Afya Mbonde, ikiwemo mashine maalum ya kusaidia watoto waliozaliwa kabla ya muda, kutasaidia kuokoa maisha ya watoto hao.
Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mbonde, Dkt. Mohamed Abbas, amesema, vifaa vilivyopokelewa vitasaidia kuimarisha huduma mbalimbali ikiwemo huduma kwa watoto, chumba cha upasuaji pamoja na huduma za maabara.
Kwa mujibu wa Dkt Abbas, kituo hicho cha afya Mbonde kinahudumia zaidi ya wananchi 32,000 kutoka kata tatu za Sululu, Mtawale na Mwenge Mtapika. Pia kituo kinatoa huduma kwa wagonjwa wanaotoka Halmashauri za Masasi na Nanyumbu.
Dkt. Abbas ameongeza kuwa, kituo hicho kinatoa huduma mbalimbali zikiwemo upasuaji, huduma za kulaza wagonjwa, uzazi pamoja na maabara.
Katika hatua nyingine, Mbunge huyo wa Jimbo la Masasi na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Leonard Akwilapo pia amekabidhi vitabu 3,667 kwa shule 12 za Halmashauri ya Mji Masasi kwa lengo la kusaidia shughuli za ufundishaji na ujifunzaji.
Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo Machi 9, 2026, mara baada ya kukutana na watendaji wa sekta ya elimu katika halmashauri hiyo, Dkt. Akwilapo amesema vitabu ni nyenzo muhimu katika kuboresha elimu shuleni.
“Kama tunavyojua, ufundishaji unahitaji zana, na moja ya zana muhimu ni vitabu. Hii ni awamu ya kwanza ya msaada huu na tutakuja tena na awamu ya pili, lengo ni kuwapa walimu nafasi ya kufanya kazi kwa ufanisi zaidi,” amesema.
Amesema, hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji ili kuongeza ubora wa elimu kwa wanafunzi wa shule hizo.












.jpg)































