Latest Articles

AFCON 2027 YACHOCHEA MAPINDUZI YA HUDUMA ZA AFYA ARUSHA

 
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Arusha, Paul Makonda, ameridhishwa na maboresho yanayoendelea katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Center inayotoa huduma kwa ushirikiano na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, ALMC–JKCI Arusha.

Maboresho hayo yanafanyika kwa uwezeshaji wa Global Medicare, kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma za afya, kuboresha mazingira ya matibabu, kuimarisha utalii tiba na kuiandaa hospitali kutoa huduma zinazokidhi viwango vya kimataifa kuelekea mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON 2027.

“Lengo kubwa ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kabisa na katika mazingira mazuri. Vilevile tunataka kuimarisha utalii tiba na kutengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya AFCON 2027,” alisema Makonda.

Makonda pia alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwekeza katika sekta ya afya na kuruhusu taasisi za kibingwa kama JKCI kupanua huduma zake hadi mikoani.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa JKCI ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Peter Kisenge, alisema maboresho yanayoendelea yanalenga kuibadilisha ALMC–JKCI kuwa kituo cha kisasa cha huduma za kibingwa chenye mazingira rafiki kwa wagonjwa.

Dkt. Kisenge alisema lengo ni kuhakikisha mgonjwa anapofika hospitalini anakutana na mazingira yenye usafi, utulivu, faraja na huduma zinazofanana na zinazopatikana katika hospitali kubwa za kimataifa.

“Tunataka mgonjwa anapokuja hapa asiingie katika mazingira yanayomwongezea hofu. Tunataka akute hospitali yenye mazingira mazuri, tulivu na yenye huduma zinazompa faraja,” alisema Dkt. Kisenge.

Kwa mujibu wake, skrini moja itaonyesha taarifa za wagonjwa waliopo wodini, ikiwemo mapigo ya moyo, kiwango cha oksijeni kwenye damu, shinikizo la damu na viashiria vingine muhimu vya afya.

Skrini nyingine itaunganishwa na mfumo wa Dozee, teknolojia inayowezesha mgonjwa kuendelea kufuatiliwa hata baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini.

Alisema mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji, upasuaji wa kujifungua au matibabu mengine yanayohitaji uangalizi wa siku kadhaa ataweza kufuatiliwa akiwa nyumbani, huku wauguzi na madaktari wakipokea taarifa za afya yake kwa wakati.

Dkt. Kisenge alisema mfumo huo utasaidia kugundua mapema mabadiliko ya hali ya mgonjwa na kuwawezesha wataalamu wa afya kuchukua hatua kabla hali haijawa mbaya.

Alisema vyumba vya wagonjwa vitawekewa vifaa vya kisasa vya ufuatiliaji, televisheni na mifumo ya kidijitali ya kuhifadhi historia ya mgonjwa, uchunguzi, dawa na matibabu yote anayopatiwa.

Dkt. Kisenge alisema hospitali pia inaandaa wodi maalumu ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu baada ya kutoka katika chumba cha wagonjwa mahututi, inayojulikana kama High Dependency Unit.

Dkt. Kisenge alisema mashine ya Cath Lab yenye thamani ya takribani shilingi bilioni tatu inatarajiwa kuwekwa katika hospitali hiyo kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya matatizo ya mishipa ya moyo.

Mkurugenzi wa Huduma za Kliniki wa ALMC–JKCI Arusha, ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Dkt. Sakeh Mwishete, alisema uongozi wa hospitali umeweka mkakati wa kuhakikisha wagonjwa wenye mahitaji tofauti wanapata huduma zinazowafaa.

Dkt. Mwishete alieleza kuwa vyumba vya VIP vimewekewa vifaa vinavyowezesha kubadilishwa haraka kuwa vyumba vya uangalizi maalumu au ICU endapo hali ya mgonjwa itabadilika.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mji

“Hiki ni chumba cha VIP, lakini kimewekewa vifaa maalumu. Endapo hali ya mgonjwa itabadilika, kinaweza kupandishwa hadhi na kutoa huduma za dharura au huduma zinazohitajika katika ICU bila kuchelewa,” alisema Dkt. Mwishete.

Naye, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Dharura katika ALMC–JKCI Arusha, Dkt. Farida Abdallah, alisema kitengo cha dharura kinaendelea kupokea wagonjwa kutoka Arusha, Manyara, Singida na maeneo mengine ya Kanda ya Kaskazini.

“Lengo letu kubwa ni kuhakikisha mgonjwa wa dharura anapata huduma kwa wakati ili kuzuia madhara ya kudumu au kupoteza maisha. Mimi pamoja na timu yangu tunafanya kazi saa 24 kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma za haraka,” alisema Dkt. Farida.




read more

GREDA LAACHA NJIA DEREVA AFANIKIWA KURUKA

Wafanyakazi wa Shandom wakifuatilia jinsi Gleda lilivyoacha njia jioni ya leo Julay 19,2026 eneo la Bondeni baada ya kupita Lugalo na hii nimepata Taarifa kutoka chanzo cha kuamika ni mara ya pili na ukiripoti tatizo unaambiea acha kazi. Muumba ameepusha hakuna majeruhi na Dereva alipoona Breck zimefeli aliruka


read more

JKT YAREJEA WITO KWA VIJANA WALIOCHELEWA KURIPOTI MAKAMBINI, WARUHUSIWA KURIPOTI HADI JUNI 15, 2026

 Na Mwandishi wetu Michuzi TV


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetoa nafasi ya mwisho kwa vijana waliohitimu elimu ya sekondari ngazi ya Kidato cha Sita mwaka 2026 na kuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, lakini bado hawajaripoti katika makambi waliyopangiwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Juni 12, 2026, jijini Dodoma na Makao Makuu ya JKT, vijana hao wametakiwa kuripoti kuanzia leo hadi Juni 15, 2026 ili kuendelea na mafunzo yao.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo JKT, Peter Mnyani, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Rajabu Nduku Mabele.

JKT imeeleza kuwa vijana ambao hawakufanikiwa kufika katika makambi waliyoelekezwa awali wanapaswa kuripoti katika kambi za JKT zilizo karibu na maeneo wanayoishi ili kurahisisha usajili na kuendelea na mafunzo.

Hata hivyo, Jeshi hilo limefafanua kuwa utaratibu huo hauhusishi vijana wanaotakiwa kuripoti katika Kambi ya Makutupora JKT Camp, Kambi ya Ruvu JKT Camp pamoja na Kambi ya Chuo cha Uongozi Kimbiji, ambazo hazijajumuishwa katika mwongozo huo wa kuripoti kwenye kambi zilizo karibu.

JKT imewasisitiza vijana wote husika kutumia fursa hiyo ya nyongeza ya muda kuhakikisha wanaripoti ndani ya kipindi kilichotolewa ili kutimiza wajibu wao wa kujiunga na mafunzo kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

read more

KIKWETE AKUTANA NA MSHARI WA TRUMP PEMBEZONI MWA MKUTANO WA OSLO FORUM

  


Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Massad Boulos, mwanadiplomasia na Mshauri Mwandamizi wa Rais Donald Trump kuhusu masuala ya Afrika, nchi za Kiarabu na Mashariki ya Kati, baada ya kufanya mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa Oslo Forum unaofanyika Oslo, Norway.


Mkutano huo, unaofanyika kuanzia tarehe 10 hadi 12 Juni, 2026, umewakutanisha viongozi, wanadiplomasia waandamizi na wadau wa masuala ya amani, diplomasia na usuluhishi kutoka nchi mbalimbali zenye ushawishi duniani.
read more

WAGONJWA NANE WENYE MISHIPA YA DAMU ILIYOZIBA KUFANYIWA UPASUAJI WA MOYO

 

Wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakishirikiana na mwenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao kumfanyia upasuaji wa kupandikiza mshipa wa damu wa moyo bila kusimamisha moyo mgonjwa mwenye matatizo ya mishipa ya damu kuziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao akitoa mafunzo kwa wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) namna ya kutoa huduma kwa wagonjwa ambao mshipa yao ya damu imeziba wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.


Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao akiangalia taarifa za mgonjwa aliyelazwa katika wodi ya uangalizi maalumu (ICU) mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza mshipa wa damu wa moyo bila kusimamisha moyo wakati wa kambi maalumu ya siku nane inayofanyika katika Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
***************************************************************************************************
Wagonjwa nane wenye matatizo ya mishipa ya damu ya moyo iliyoziba (coronary artery disease) kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo (off Pump CABG).

Upasuaji huo unafanyika katika kambi maalumu ya siku nane inayofanywa na watalaamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Upasuaji wa Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya alisema wagonjwa wenye matatizo ya mishipa ya damu ya moyo iliyoziba watumie kambi hiyo kupata matibabu na kupunguza gharama ambazo wangetumia kusafiri nje ya nchi kwaajili ya matibabu.

“Upasuaji huu unafaida kubwa kwa wagonjwa ambao wamekuwa wakitumia dawa kwa muda mrefu kwa kupata matibabu kwani unafanyika bila kusimamisha moyo na unamsaidia mgonjwa kupona kwa muda mfupi na kuendelea na shughuli zake za kawaida”, alisema Dkt. Angela.

Dkt. Angela alibainisha kuwa kupitia kambi hiyo wataalumu wa JKCI watapata fursa ya kujengewa uwezo na kubadilishana uzoefu na wenzao kutoka India jambo mbalo litasaidia kuimarisha zaidi huduma za upasuaji na mishipa ya moyo nchini.

“Tayari tumemfanyia upasuaji mgonjwa mmoja ambaye mishipa mitatu ya moyo ilikuwa imeziba kwa mafanikio makubwa na tunatarajia kuwafanyia upasuaji wagonjwa nane katika kambi hii”, alisema Dkt. Angela.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Moyo na Mishipa ya Damu kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India Upendra Bhalerao alisema upasuaji huo unafanyika kwa ufanisi mkubwa kutokana na uwekezaji mkubwa wa vifaa tiba uliofanywa na Serikali ya Tanzania kupitia JKCI.

“Tumekuwa tukija Tanzania mara kwa mara kutokana na ushirikiano mzuri wa kitabibu uliopo kati ya India na Tanzania na kuwasaidia wagonjwa ambao wanatumia gharama kubwa kufuata matibabu India hivyo uwepo wetu hapa umekuwa ukiwapunguzia adha wagonjwa wenye matatizo ya mishipa yad amu ya moyo iliyoziba”, alisema Bhalerao.

Kambi hiyo maamulu ya upasuaji wa mishipa ya damu ya moyo iliyoziba inatarajiwa kumalizika mapema tarehe 15 mwezi Juni mwaka huu.

read more

RAIS WA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MADAKTARI WA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) DR. NIKOLAI SHARKOV ATEMBELEA MABANDA MAONESHO YA PILI YA BIDHAA ZA KINYWA NA MENO ZA KIMATAIFA (DENTAL EXPO)

 

Rais wa Shirika la Kimataifa la madaktari wa Afya ya Kinywa  na Meno Duniani (FDI) Prof. Dr. Nikolai sharkov akizungumza na washiriki wakati wa Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Kinywa na Meno za Kimataifa (Dental EXPO) leo Mei 28 Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Mei 30,2026.

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Edna Kajuna akizungumza na Rais wa Shirika la Kimataifa la madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Duniani (FDI) Prof. Dr. Nikolai sharkov alipotembelea Banda la Taasisi hiyo katika Ukumbi wa Mlimani City wakati wa Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Kinywa na Meno za Kimataifa (Dental EXPO) leo Mei 28 Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Mei 30,2026.

Washiriki wakimsikiliza Rais wa Shirika la Kimataifa la madaktari wa Afya ya Kinywa  na Meno Duniani (FDI) Prof. Dr. Nikolai sharkov alipokuwa akizungumza wakati wa Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Kinywa na Meno za Kimataifa ( Dental EXPO) leo Mei 28 Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Mei 30,2026.

Wasanii wa Kikundi cha Kusa Bendi wakinogesha Maonesho ya Pili ya Bidhaa za Kinywa na Meno za Kimataifa (Dental EXPO) leo Mei 28 katika Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam ambayo yanatarajiwa kumalizika Mei 30,2026.

read more

TDA NA SHIRIKISHO LA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI (FDI) WAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA MUHAS

 Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania (TDA) na Shirikisho la Madaktari wa Meno Duniani (FDI) wameahidi kuendeleza uhsirikiano na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.


Ahadi ya ushirikiano huo ilifikiwa mwishoni mwa wiki, wakati Mkuu wa Shule Kuu ya Afya ya Kinywa na Meno, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Dkt. Ferdinand Machibya, alipokuwa akizungumza na Rais wa Shirikisho la kinywa na Meno Duniani (FDI), Prof. Nikolai Sharkov, ambaye alitembelea MUHAS akiwa na ujumbe wake kutoka FDI kwa lengo la kuongeza ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.

Ziara hiyo iliwakutanisha wataalamu wa tiba ya meno, wahadhiri, pamoja na wanafunzi kwa ajili ya kujadili fursa za ushirikiano katika mafunzo, utafiti, na kujengeana uwezo ndani ya sekta ya afya ya meno.

Akizungumza wakati wa mkutano huo, Dk. Machibya, alimkaribisha, Prof. Nikolai Sharkov, chuoni hapo. Alieleza kuwa ziara hiyo inaonesha kuongezeka kwa ushirikiano kati ya MUHAS na washirika wa kimataifa katika kuendeleza elimu ya tiba ya meno na huduma za afya.

Dk. Machibya alisema MUHAS inaendelea kuwa na mchango mkubwa katika kuzalisha wataalamu wenye ujuzi kupitia ufundishaji, utafiti, pamoja na huduma za ushauri wa kitaalamu. Aliongeza kuwa Shule ya Tiba ya Meno imekuwa ikivutia wanafunzi wa shahada za uzamili na wataalamu kutoka nchi mbalimbali wanaojiunga na chuo hicho kwa ajili ya mafunzo maalum na kozi fupi za afya.

Katika ziara hiyo, Prof. Sharkov aliipongeza Shule ya Tiba ya Meno ya MUHAS kwa mchango wake katika sayansi ya afya ya kinywa na meno, na kuisifu shule hiyo kwa kuwa Kituo Bora cha Umahiri katika Sayansi ya Afya ya Kinywa na Meno Afrika Mashariki.

Kwa upande wake, Prof. Sharkov pia aliipongeza MUHAS pamoja na Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania kwa mchango wao katika kuimarisha huduma za afya ya meno na kuzalisha wataalamu wenye sifa nchini Tanzania.

Aidha, aliwahimiza wanafunzi wa tiba ya meno kuendelea kuwa makini katika masomo yao na kukuza taaluma zao ili waweze kuchangia ipasavyo katika mustakabali wa huduma za afya ya kinywa na meno.

Tukio hilo lilifanyika katika Shule ya Tiba ya Meno MUHAS na kuhudhuriwa na viongozi wa Chama cha Madaktari wa Meno Tanzania, madaktari wa meno wa kanda mbalimbali, wahadhiri wa MUHAS, pamoja na wanafunzi. 

read more