Latest Articles
TAASISI YA MOYO (JKCI) YAIBUKA KIDEDEA MFANYAKAZI BORA 2024
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 8:12 AMread more
KUNDI LINGINE LENYE WANANCHI 564 LAHAMA HIFADHI YA NGORONGORO.
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 2:23 AMNa Mwandishi wetu, Ngorongoro.
RAIS WA JAMHURI YA SOMALIA MHE. HASSAN MOHAHADAIPONGEZA TAASISI YA MOYO YA JAKAYA KIKWETE (JKCI)
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:53 PMRais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akisaini kitabu cha wageni Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud tibabu ya moyo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge.
Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Moyo na Dkt. Bingwa Magonjwa ya Moyo Dkt. Peter Kisenge. mara alipoitembelea Taasisi hiyo kujionea mtambo wa Cathlab ambao ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo. Wa katikati anae shuhudia ni Waziri wa Afya Nchini Tanzania Mhe. Ummy Mwalimu wakimo viongozi wengine wa Taasisi hiyo.Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud aipongeza JKCI
Na Mwandishi Maalumu - Dar es Salaam
27/4/2024 Rais wa Jamhuri ya Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud amewapongeza wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa huduma nzuri wanayoitoa ya kuokoa maisha ya watu wenye matatizo ya moyo.
Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud alizitoa pongezi hizo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea Taasisi hiyo (JKCI) kwaajili ya kuona huduma za matibabu ya moyo zinazotolewa.
Akiwa katika Taasisi hiyo Mhe. Rais Mahamud alitembelea maeneo mbalimbali ya JKCI ikiwa ni pamoja na mtambo wa Cathlab ambayo ni maabara inayotumia mionzi maalumu kwaajili ya kufanya uchunguzi na matibabu ya moyo.
Akizungumzia kuhusu ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema JKCI ni moja ya Taasisi inayoongoza katika nchi za Afrika Mashariki na kati katika kutoa huduma za kibingwa za matibabu ya moyo.
Dkt. Kisenge alisema Rais Mohamud alitembelea Taasisi hiyo kwaajili ya kuona namna ambavyo nchi ya Somalia itawapeleka wagonjwa wa moyo JKCI kupata tiba ya matibabu ya moyo.
“Nchi ya Somalia inawapeleka wagonjwa wengi wa moyo kwenda kutibiwa katika nchi za India, Ulaya na Marekani wakati huduma hii inapatikana nchini Tanzania, na ukiangalia nchi hizi ziko karibu hivyo basi itakuwa ni rahisi kwao kuwaleta wagonjwa kuja kutibiwa hapa kwetu”.
“Kuja kwa wagonjwa hawa kutaisaidia nchi yetu kukua kiuchumi kwani pesa zitakazopatikana zitawafikia watu wengi ikiwemo wamiliki wa hoteli ambako wagonjwa watalala pamoja na wafanyabiashara watakaowauzia vyakula na mahitaji mengine”, alisema Dkt. Kisenge.
Dkt. Kisenge alimshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuzidi kuimarisha mahusiano na nchi za nje ndiyo maana watu wengi wanakuja kuwekeza hapa nchi hata Taasisi hiyo imekuwa ikiwapokea wageni mbalimbali kutoka nchi za nje.
Akiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Mhe. Rais Hassan Sheikh Mohamud pamoja na ujumbe wake aliambata na Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu.
Hafla ya kukabidhi madarasa hayo, iliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kondoa, Dkt. Khamis Mkanachi ambaye aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa pamoja na Maafisa Elimu Sekondari na Msingi.
Katika hafla zote mbili Dkt. Khamis Mkanachi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kukubali maombi ya ujenzi wa madarasa katika Wilaya ya Kondoa, ambayo yapo katika vijiji vya Kikilo na Bukulu. Huku akitoa rai kwa wanafunzi kusoma kwa bidii kwani mazingira ya shule yanaendelea kuboreshwa.
Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa, Mashauri Vicent aliyekabidhiwa madarasa hayo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya elimu pia kuahidi kuwa watahakikisha madarasa hayo yanakuwa ni sehemu ya kuchagiza ongezeko la wanufaika ambayo ni watoto kwenye jamii ya Kondoa.
Kwa upande wa Benki ya CRDB, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay aliyeongozana na Mkuu wa Kitengo cha Uwekezaji kwa Jamii pamoja na Kaimu Meneja wa Kanda ya Kati, amesema kuwa Benki ya CRDB imeweka sera ya uwekezaji kwa jamii inayolenga kuchangia maendeleo mbalimbali katika jamii hasa katika swala la Elimu, Mazingira, Afya, Vijana na Wanawake. Aidha, ametoa rai kwa wazazi wa shule hizo kuendelea kushirikiana kwa karibu na uongozi wa shule katika kuboresha miundombinu ya shule.
AGENDA YA KUTOKOMEZA MALARIA IWE YA KUDUMU KATIKA VIKAO VYA MAAMUZI
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:30 AMNa WAF, TABORA
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ameziasa Kamati za Ulinzi na Usalama nchini kuona umuhimu wakuifanya ajenda yakutokomeza Malaria iwe yakudumu kwenye vikao vya maamuzi.
Dkt. Mollel ameyasema hayo leo, Aprili 25, 2024 akiwa amemwakilisha Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu kwenye kilele cha Siku ya Malaria Duniani iliyofanyika mkoani Tabora na kusema kuwa kama nchi imeendelea kupiga hatua katika vita hivyo ikilinganishwa na miaka zaidi ya ishini iliyopita ambapo maambuki na vifo vya Malaria vilikuwa kati ya asilimia 45 hadi 50.
Aidha Dkt. Mollel amesema azma ya Serikali ni kufikia asilimia 3.5 ifikapo 2025 na kuwa na ziro Malaria 2030 huku akisisitiza kwa kusema itafikiwa endapo juhudi za Makusudi zitafanywa kwa ushirikiano baina ya Serikali na wadau
"Leo tunazungumza asilimia 8.1 kama nchi lakini miaka ya 1998, tulikuwa na kiwango cha juu sana, hivyo ili tuweze kufikia adhma yakumaliza kabisa malaria ifikapo 2030 kila mmoja wetu anawajibu wakufanya" amesema Mollel.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya Ofisi ya Rais TAMISEMI Samsoni Maella, amesema Utumiaji wa Mifumo ya GoTHOMIS na FFARS imekuwa chachu ya kukusanya takwimu sahihi kwa ajili ya ngazi ya maamuzi, hali iliyochangia kufanya maamuzi sahihi kutokana na kuwa na takwimu sahihi.
"Kama Ofisi ya Rais TAMISEMI, tumefanikiwa kuimarisha miundo mbinu ya Afya na Rasilimali watu mathalani miaka mitatu nyuma tulikuwa na Hospitali za Wilaya 77 leo hii tunazo 177 hizi zimechochea sana uimarishaji wa huduma” amesema Mahela.
Naye Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI Dkt. Hamis Kigwangala ametoa wito kwa serikali na wadau kuongeza afua za kutibu watoto Shuleni, pia wafike maeneo ya Migodi, Mashamba Makubwa na maeneo ya Wafugaji.
Awali Msimamizi wa Miradi kutoka Wizara ya Afya Dkt. Catherine Joachim, akiwa amemwakilisha Katibu Mkuu, amesema kuchaguliwa kwa mkoa wa Tabora kuwa mwenyeji wa Maadhimisho ya Wiki ya Malaria, ni pamoja na kuongeza nguvu ya afua za kupambana na Malaria kutokana na Mkoa huo kuwa na Maambukizi ya juu ya Ugonjwa huo ya asilimia 23.4 kwa sasa kutoka asilimia 11.7 kwa mwaka 2011.
AIS SAMIA AKIWA KWENYE SHEREHE ZA MIAKA 60 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 5:10 AMMKUTANO MKUU WA ALAT 2024; WAZIRI MCHENGERWA ATEMBELEA BANDA LA PSSSF
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 4:58 AMZANZIBAR