MELI ZA JESHI LA IRAN ZATIA NANGA KATIKA BANDARI YA DURBAN
Posted by khamisimussa77@gmail.com at 6:33 AM
Meli za kikosi cha upelelezi cha operesheni
ya mabaharia 44 wa jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, zimewasili
katika bandari ya Durban, Afrika Kusini.
Meli hizo zinazozijumuisha meli ya ulinzi na meli ya Alvand
zinaelekea bandari ya Cape Town na bahari ya Atlantic nchini Afrika
Kusini. Kwa mujibu wa habari, balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Ira
nchini Afrika Kusini, Mohsen Movahedi Ghomi amezipokea meli hizo katika
bandari hiyo ya Durban nchini humo.
Akizungumza katika mapokezi ya msafara huo wa operesheni ya mabaharia
44 wa meli za jeshi uliopewa jina la Matumaini ya Golestan,
amezungumzia mahusiano ya kistratijia baina ya Iran na Afrika Kusini na
kusema kuwa, misafara hiyo ni yenye umuhimu wa aina yake kwa ajili ya
kuinua kiwango cha stratijia baina ya nchi mbili. Msafara wa meli za
kundi la 44 la kikosi cha baharini cha jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya
Iran na ambazo hapo awali zilitia nanga jijini Dar es Salaam, Tanzania,
ulianza mwanzoni mwa mwezi Oktoba mwaka huu kwa kupitia maji ya
kimataifa ya Ghuba ya Aden na langobahari la kistratijia la
Bab-el-Mandeb.
Jukumu la msafara huo ni kudhamini usalama wa meli za kibiashara na
mafuta za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na vitisho vyovyote vya
baharini dhidi yake. Aidha imeelezwa kuwa, hatua hiyo inalenga
kuwafikishia ujumbe wa amani na urafiki watu wa Afrika Kusini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: