Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Jasem Al-Najem na Mkuu wa Wilaya ya
Kigamboni Hashim Mgandilwa wameshiriki katika futari iliyoandaliwa na
Ubalozi wa Kuwait kwa ajili ya wananchi wa wilaya hiyo. Futari hiyo
ilifanyika katika msikiti wa Daaru Salaam Kigamboni na kuhudhuriwa na
viongozi mbalimbali wa kidini na wananchi, na kuwajumuisha wanafunzi na
mayatima wanaofadhiliwa na jumuiya za misaada za Kuwait zilizopo nchini.
Pembezoni
mwa futari hiyo iliyotumbuizwa na kasida kutoka kwa watoto, Al-Najem
alimkabidhi Mkuu wa Wilaya wa Kigamboni Hashim Mgandilwa zawadi.
Yafaa
kueleza kuwa Ubalozi wa Kuwait nchini utaendelea na program yake ya
kufuturisha katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhan katika
maeneo mbalimbali nchini.a
0 comments: