RAIS SAMIA AONGOZA SEMINA ALEKEZI KWA MAWAZIRI, NAIBU MAWAZIRI NA MAKATIBU WAKUU WA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUMGANO WA TANZANIA NA SERIKALI YA ZANZIBAR

 
Leo  nimekutana na Balozi wa Uswisi nchini Tanzania, Mhe. Nicole Providoli, ambapo tumebadilishana mawazo kuhusu namna ya kuendeleza ushirikiano katika kuimarisha sekta ya afya kwa manufaa ya wananchi wa Zanzibar.

Nimemueleza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuwekeza katika kujenga mifumo imara ya afya, kuboresha ugharamiaji wa huduma za afya na kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote ili kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora, salama na kwa usawa.


Pia nimetoa shukrani kwa Serikali ya Uswisi kwa ushirikiano wake wa muda mrefu katika sekta ya afya, hususan katika utafiti, mapambano dhidi ya malaria na kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya.


Ninaamini ushirikiano huu utaendelea kuleta matokeo chanya katika kuboresha afya na ustawi wa wananchi wetu, sambamba na kuijenga Zanzibar yenye jamii yenye afya na maendeleo endelevu.

0 comments: